< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Et l'Éternel parla à Moïse, en disant:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
Au premier jour du premier mois, tu dresseras la Demeure du tabernacle d'assignation;
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Et tu y mettras l'arche du Témoignage, et tu couvriras l'arche avec le voile.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Tu apporteras aussi la table, et tu y arrangeras ce qui doit y être arrangé; tu apporteras aussi le chandelier, et tu allumeras ses lampes.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Et tu mettras l'autel d'or pour le parfum devant l'arche du Témoignage, et tu poseras la tapisserie de l'entrée de la Demeure.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Et tu mettras l'autel de l'holocauste devant l'entrée de la Demeure du tabernacle d'assignation.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
Et tu mettras la cuve entre le tabernacle d'assignation et l'autel, et tu y mettras de l'eau.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Et tu placeras le parvis tout autour, et tu mettras la tapisserie à la porte du parvis.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Puis tu prendras l'huile de l'onction, et tu oindras la Demeure et tout ce qui y est, et tu la consacreras, avec tous ses ustensiles; et elle sera sainte.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Tu oindras aussi l'autel de l'holocauste et tous ses ustensiles, et tu consacreras l'autel; et l'autel sera très saint.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Tu oindras aussi la cuve et sa base, et tu la consacreras.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Puis tu feras avancer Aaron et ses fils à l'entrée du tabernacle d'assignation, et tu les laveras dans l'eau.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Et tu revêtiras Aaron des vêtements sacrés, et tu l'oindras, et tu le consacreras, et il exercera devant moi la sacrificature.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Et tu feras avancer ses fils, et tu les revêtiras de tuniques;
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
Et tu les oindras, comme tu auras oint leur père, et ils exerceront devant moi la sacrificature; et leur onction leur conférera une sacrificature perpétuelle, d'âge en âge.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Et Moïse fit selon tout ce que l'Éternel lui avait commandé; il fit ainsi.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Et au premier jour du premier mois, dans la seconde année, la Demeure fut dressée.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Et Moïse dressa la Demeure, et mit ses soubassements, et posa ses planches, et mit ses traverses, et dressa ses colonnes.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il étendit le tabernacle sur la Demeure, et il posa la couverture du tabernacle par-dessus, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Puis il prit aussi et mit le Témoignage dans l'arche, et il plaça les barres à l'arche, et il mit le propitiatoire sur l'arche, par-dessus.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il porta l'arche dans la Demeure, et posa le voile destiné à cacher le lieu très-saint, et couvrit l'arche du Témoignage, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Il mit aussi la table dans le tabernacle d'assignation, au côté Nord de la Demeure, en dehors du voile;
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il arrangea sur elle une rangée de pains, devant l'Éternel, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
Il plaça aussi le chandelier dans le tabernacle d'assignation, vis-à-vis de la table, au côté Sud de la Demeure.
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il alluma les lampes devant l'Éternel, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Il plaça aussi l'autel d'or dans le tabernacle d'assignation, devant le voile;
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
Et il y fit fumer le parfum d'aromates, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Il posa aussi la tapisserie de l'entrée de la Demeure.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
Puis il plaça l'autel de l'holocauste à l'entrée de la Demeure du tabernacle d'assignation, et il y offrit l'holocauste et l'oblation, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Il plaça aussi la cuve entre le tabernacle d'assignation et l'autel, et il y mit de l'eau pour laver;
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
Et Moïse et Aaron et ses fils en lavaient leurs mains et leurs pieds.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Quand ils entraient au tabernacle d'assignation, et qu'ils s'avançaient vers l'autel, ils se lavaient, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Il dressa aussi le parvis tout autour de la Demeure et de l'autel, et il mit la tapisserie à la porte du parvis. Ainsi Moïse acheva l'ouvrage.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Et la nuée couvrit le tabernacle d'assignation, et la gloire de l'Éternel remplit la Demeure;
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
De sorte que Moïse ne put entrer dans le tabernacle d'assignation, car la nuée se tenait dessus, et la gloire de l'Éternel remplissait la Demeure.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Or, pendant toutes leurs marches, quand la nuée s'élevait de dessus la Demeure, les enfants d'Israël partaient;
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
Mais si la nuée ne s'élevait point, ils ne partaient point, jusqu'au jour où elle s'élevait.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Car la nuée de l'Éternel était sur la Demeure pendant le jour, et le feu y était la nuit, aux yeux de toute la maison d'Israël, pendant toutes leurs marches.

< Kutoka 40 >