< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
" Le premier jour du premier mois, tu dresseras la Demeure, la tente de réunion.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Tu y placeras l'arche du témoignage, et tu couvriras l'arche avec le voile.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Tu apporteras la table et tu y disposeras ce qui doit la garnir. Tu apporteras le chandelier et tu poseras dessus ses lampes.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Tu placeras l'autel d'or pour le parfum devant l'arche du témoignage, et tu mettras le voile à l'entrée de la Demeure.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Tu placeras l'autel des holocaustes devant l'entrée de la Demeure, de la tente de réunion.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
Tu placeras la cuve entre la tente de réunion et l'autel, et tu y mettras de l'eau.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Tu dresseras le parvis à l'entour, et tu mettras la tenture à la porte du parvis.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
" Tu prendras l'huile d'onction, tu en oindras la Demeure et tout ce qu'elle renferme; tu la consacreras avec tous ses ustensiles, et elle sera sainte.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Tu oindras l'autel des holocaustes et tous ses ustensiles; tu consacreras l'autel, et l'autel sera très saint.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Tu oindras la cuve avec sa base, et tu la consacreras.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
" Tu feras avancer Aaron et ses fils près de l'entrée de la tente de réunion, et tu les laveras avec de l'eau.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Puis tu revêtiras Aaron des vêtements sacrés, tu l'oindras et tu le consacreras, et il sera prêtre à mon service.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Tu feras approcher ses fils et, les ayant revêtus des tuniques,
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
tu les oindras comme tu auras oint leur père, et ils seront prêtres à mon service. Cette onction leur conférera le sacerdoce à perpétuité parmi leurs descendants. "
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Moïse fit tout ce que Yahweh lui avait ordonné; il fit ainsi.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Le premier jour du premier mois de la seconde année, la Demeure fut dressée.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Moïse dressa la Demeure; il en posa les socles, il en plaça les planches et les traverses, en dressa les colonnes.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Il étendit la tente sur la Demeure, et mit par-dessus la couverture de la tente, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Il prit le témoignage et le plaça dans l'arche; il mit les barres à l'arche et posa le propitiatoire au-dessus de l'arche.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Il porta l'arche dans la Demeure; et, ayant mis le voile de séparation, il en couvrit l'arche du témoignage, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Il plaça la table dans la tente de réunion, au côté septentrional de la Demeure, en dehors du voile,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
et il y disposa les pains devant Yahweh, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
Il plaça le chandelier dans la tente de réunion, vis-à-vis de la table, au côté méridional de la Demeure,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
et il y posa les lampes devant Yahweh, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Il plaça l'autel d'or dans la tente de réunion, devant le voile,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
et il y fit brûler l'encens, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Il plaça le rideau à l'entrée de la Demeure.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
Il plaça l'autel des holocaustes à l'entrée de la Demeure, de la tente de réunion, et il y offrit l'holocauste et l'oblation, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Il plaça la cuve entre la tente de réunion et l'autel, et il y mit de l'eau pour les ablutions;
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
Moïse, Aaron et ses fils s'y lavèrent les mains et les pieds.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Lorsqu'ils entraient dans la tente de réunion et qu'ils s'approchaient de l'autel, ils se lavaient, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Il dressa le parvis autour de la Demeure et de l'autel, et il mit la tenture à la porte du parvis. Ce fut ainsi que Moïse acheva cette œuvre.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Alors la nuée couvrit la tente de réunion, et la gloire de Yahweh remplit la Demeure.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Et Moïse ne pouvait plus entrer dans la tente de réunion, parce que la nuée restait dessus, et que la gloire de Yahweh remplissait la Demeure.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Tant que durèrent leurs marches, les enfants d'Israël partaient lorsque la nuée s'élevait de dessus la Demeure;
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
et si la nuée ne s'élevait pas, ils ne partaient pas, jusqu'au jour où elle s'élevait.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Car la nuée de Yahweh reposait pendant le jour sur la Demeure, et, pendant la nuit, il y avait du feu dans la nuée, aux yeux de toute la maison d'Israël, tant que durèrent leurs marches.

< Kutoka 40 >