< Kutoka 40 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Then Yahweh said to Moses/me,
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
“On the first day of the first month next year, [tell the people to] set up the Sacred Tent.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Put inside it the sacred chest [that contains the stone slabs on which are engraved] the Ten Commandments, and hang the curtain in front of it.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Bring the table into the Sacred Tent, and place on it all the things that are to be used with it. Bring in the lampstand and fasten the lamps to it.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Put the gold altar for [burning] incense in front of the sacred chest, and set up the curtain at the entrance of the Sacred Tent.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Put the altar for burning sacrifices in front of the Sacred Tent.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
Put the washbasin between the Sacred Tent and the altar, and fill it with water.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Hang the curtains that will surround the courtyard, and hang the curtain at its entrance.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Then take the oil for anointing, and anoint the Sacred Tent and everything that is in it, to (set it apart/dedicate it) to me. Then it will be holy/sacred.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Also anoint the altar for offering sacrifices that will be completely burned, and all the things that will be used with it, and set it apart. Then it also will be holy/sacred.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Also anoint the washbasin and its base, to set it apart.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Then bring Aaron and his sons to the entrance of the Sacred Tent, and wash them [ritually] with water.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
Then put on Aaron his sacred clothes to (set him apart/dedicate him), in order that he can serve me as a priest.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Also bring his sons there. Put their sacred tunics/gowns on them
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
and anoint them just as you anointed their father, in order that they also may serve me by working as priests. By anointing them [and their descendants], you will cause them and their descendants to be priests throughout all coming generations.”
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Moses/I did all these things exactly as Yahweh had commanded him/me.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
On the first day of the first month of the next year (OR, second year [after they/we left Egypt]), the people set up the Sacred Tent.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Following Moses’/my instructions, they set up the Sacred Tent and its bases, set up the frames, attached the crossbars, and put up the posts [for the curtains].
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Then they spread out the coverings over the Sacred Tent, exactly as Yahweh had commanded.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Then he/I took the two stone slabs [on which the commandments were written] and put them in the sacred chest. He/I put the carrying poles [in the rings] on the chest and put the lid on top of the chest.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Then he/I took the chest into [the Very Holy Place inside] the Sacred Tent and hung the curtain. In that way, he/I prevented the people who were outside from seeing the chest. He/I did all this exactly as Yahweh had commanded him/me.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
He/I set the table inside the Sacred Tent, on the north side, outside the curtain.
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
He/I placed on the table the bread that was offered to Yahweh, exactly as Yahweh had commanded.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
He/I set the lampstand inside the Sacred Tent, on the south side, opposite the table.
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Then he/I fastened the lamps to the lampstand in Yahweh’s presence, exactly as Yahweh had commanded.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
He/I set the golden altar for burning incense inside the Sacred Tent, in front of the curtain [that separated the Holy Place from the Very Holy Place],
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and he/I burned some sweet-smelling incense on it, exactly as Yahweh had commanded him/me.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
He/I hung the curtain at the entrance to the Sacred Tent.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
At the entrance to the Sacred Tent, he/I set the altar for offering sacrifices that were to be burned completely. Then he/I offered on it the meat that was to be burned completely and the grain offering, exactly as Yahweh had commanded him/me.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
He/I set the washbasin between the Sacred Tent and the [bronze] altar, and he/I filled the washbasin with water.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
Every time Moses/I and Aaron and his sons went into the Sacred Tent or went to the altar, they/we washed their/our hands and feet [ritually], exactly as Yahweh had commanded Moses/me.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
Following Moses’/my instructions, they hung the curtains that surrounded the courtyard and the altar, and they hung the curtain at the entrance to the courtyard. So Moses/I finished that work.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Then the [tall bright] cloud covered the Sacred Tent, and Yahweh’s (glory/brilliant light) filled the Sacred Tent.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Because that light was very bright, Moses/I was not able to enter the Sacred Tent.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
From that day, whenever the Israeli people wanted to move to another place, they went only when the bright cloud rose from above the Sacred Tent.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
If the cloud did not rise, they stayed where they were and did not go on until the cloud rose.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Wherever they traveled, the bright cloud that [indicated] Yahweh’s [presence] was above the Sacred Tent during the day, and a [bright] fire was inside the cloud at night, with the result that all the Israeli people [MTY] could see it [at any time].