< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
in/on/with day [the] month [the] first in/on/with one to/for month to arise: raise [obj] tabernacle tent meeting
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
and to set: put there [obj] ark [the] testimony and to cover upon [the] ark [obj] [the] curtain
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
and to come (in): bring [obj] [the] table and to arrange [obj] valuation his and to come (in): bring [obj] [the] lampstand and to ascend: establish [obj] lamp her
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
and to give: put [obj] altar [the] gold to/for incense to/for face: before ark [the] testimony and to set: make [obj] covering [the] entrance to/for tabernacle
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
and to give: put [obj] altar [the] burnt offering to/for face: before entrance tabernacle tent meeting
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
and to give: put [obj] [the] basin between tent meeting and between [the] altar and to give: put there water
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
and to set: make [obj] [the] court around and to give: put [obj] covering gate [the] court
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
and to take: take [obj] oil [the] anointing and to anoint [obj] [the] tabernacle and [obj] all which in/on/with him and to consecrate: consecate [obj] him and [obj] all article/utensil his and to be holiness
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
and to anoint [obj] altar [the] burnt offering and [obj] all article/utensil his and to consecrate: consecate [obj] [the] altar and to be [the] altar holiness holiness
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
and to anoint [obj] [the] basin and [obj] stand his and to consecrate: consecate [obj] him
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
and to present: bring [obj] Aaron and [obj] son: child his to(wards) entrance tent meeting and to wash: wash [obj] them in/on/with water
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
and to clothe [obj] Aaron [obj] garment [the] holiness and to anoint [obj] him and to consecrate: consecate [obj] him and to minister to/for me
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
and [obj] son: child his to present: bring and to clothe [obj] them tunic
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
and to anoint [obj] them like/as as which to anoint [obj] father their and to minister to/for me and to be to/for to be to/for them anointing their to/for priesthood forever: enduring to/for generation their
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
and to make: do Moses like/as all which to command LORD [obj] him so to make: do
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
and to be in/on/with month [the] first in/on/with year [the] second in/on/with one to/for month to arise: raise [the] tabernacle
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
and to arise: raise Moses [obj] [the] tabernacle and to give: put [obj] socket his and to set: make [obj] board his and to give: put [obj] bar his and to arise: raise [obj] pillar his
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
and to spread [obj] [the] tent upon [the] tabernacle and to set: put [obj] covering [the] tent upon him from to/for above [to] like/as as which to command LORD [obj] Moses
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
and to take: take and to give: put [obj] [the] testimony to(wards) [the] ark and to set: make [obj] [the] alone: pole upon [the] ark and to give: put [obj] [the] mercy seat upon [the] ark from to/for above [to]
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
and to come (in): bring [obj] [the] ark to(wards) [the] tabernacle and to set: make [obj] curtain [the] covering and to cover upon ark [the] testimony like/as as which to command LORD [obj] Moses
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
and to give: put [obj] [the] table in/on/with tent meeting upon thigh [the] tabernacle north [to] from outside to/for curtain
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and to arrange upon him valuation food: bread to/for face: before LORD like/as as which to command LORD [obj] Moses
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
and to set: put [obj] [the] lampstand in/on/with tent meeting before [the] table upon thigh [the] tabernacle south [to]
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and to ascend: establish [the] lamp to/for face: before LORD like/as as which to command LORD [obj] Moses
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
and to set: put [obj] altar [the] gold in/on/with tent meeting to/for face: before [the] curtain
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and to offer: burn upon him incense spice like/as as which to command LORD [obj] Moses
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
and to set: put [obj] covering [the] entrance to/for tabernacle
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
and [obj] altar [the] burnt offering to set: make entrance tabernacle tent meeting and to ascend: offer up upon him [obj] [the] burnt offering and [obj] [the] offering like/as as which to command LORD [obj] Moses
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
and to set: make [obj] [the] basin between tent meeting and between [the] altar and to give: put there [to] water to/for to wash: wash
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
and to wash: wash from him Moses and Aaron and son: child his [obj] hand their and [obj] foot their
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
in/on/with to come (in): come they to(wards) tent meeting and in/on/with to present: come they to(wards) [the] altar to wash: wash like/as as which to command LORD [obj] Moses
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
and to arise: raise [obj] [the] court around to/for tabernacle and to/for altar and to give: put [obj] covering gate [the] court and to end: finish Moses [obj] [the] work
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
and to cover [the] cloud [obj] tent meeting and glory LORD to fill [obj] [the] tabernacle
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
and not be able Moses to/for to come (in): come to(wards) tent meeting for to dwell upon him [the] cloud and glory LORD to fill [obj] [the] tabernacle
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
and in/on/with to ascend: establish [the] cloud from upon [the] tabernacle to set out son: descendant/people Israel in/on/with all journey their
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
and if not to ascend: establish [the] cloud and not to set out till day to ascend: establish he
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
for cloud LORD upon [the] tabernacle by day and fire to be night in/on/with him to/for eye: seeing all house: household Israel in/on/with all journey their

< Kutoka 40 >