< Kutoka 40 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Then spake Yahweh unto Moses, saying—
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
On the first day of the month, in the first month, shalt thou rear the habitation, of the tent of meeting;
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
and thou shalt put therein, the ark of the testimony, —and shalt screen the ark with the veil;
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
and thou shalt bring in the table, and set in order what is to be arranged thereupon, —and thou shalt bring in the lampstand, and mount the lamps thereof;
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
and thou shalt place the altar of gold for incense, before the ark of the testimony, —and put up the screen for the opening of the habitation;
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
and thou shalt place the altar for the ascending-sacrifice, —before the opening of the habitation of the tent of meeting;
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
and thou shalt place the laver between the tent of meeting, and the altar, and shalt put therein water,
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
And thou shalt put up the court round about, and hang up the screen of the gate of the court.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
And thou shalt take the oil of anointing, and anoint the habitation and all that is therein, —and shalt hallow it. and all the furniture thereof so shall it be holy.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
And thou shalt anoint the altar of ascending sacrifice, and all its utensils, —and hallow the altar, so shall the altar be most holy:
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
and thou shalt anoint the laver and its stand, —and shalt hallow it.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And thou shalt bring near Aaron and his sons, unto the opening of the tent of meeting, —and shalt bathe them in the water;
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
and thou shalt clothe Aaron with the holy garments, —and shalt anoint him and hallow him so shall he minister as priest unto me.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
His sons also, shalt thou bring near, —and shalt clothe them with tunics;
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
and shalt anoint them as thou didst anoint their father, and they shall minister as priests unto me, —so shall their anointing remain to them for an age-abiding priesthood, to their generations.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses did, —according to all that Yahweh had commanded him, so did he.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Thus came it to pass, in the first month, in the second year, on the first of the month, that the habitation was reared.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
Yea Moses reared the habitation, and placed its sockets, and fixed its boards, and fastened its bars, —and reared its pillars.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Then spread he abroad the tent upon the habitation, and put the covering of the tent upon it, above, —As Yahweh commanded Moses.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he took and placed the testimony within the ark, and put the staves upon the ark, —and placed the propitiatory upon the ark, above;
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
and brought in the ark into the habitation, and put up the screening veil, and screened over the ark of the testimony, —As Yahweh commanded Moses.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he placed the table in the tent of meeting, —on the side of the habitation northward, —outside the veil;
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and set in order thereupon the arrangement of bread before Yahweh, —As Yahweh commanded Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
And he put the lampstand, in the tent of meeting, over against the table, —on the side of the habitation southward;
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and mounted the lamps before Yahweh, —As Yahweh commanded Moses.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
And he put the altar of gold in the tent of meeting, —before the veil;
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and burned thereupon the fragrant incense, —As Yahweh commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
And he put up the screen of the entrance pertaining to the habitation;
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
and, the altar of ascending-sacrifice, put he at the entrance of the habitation of the tent of meeting, —and he caused to ascend thereupon the ascending-sacrifice, and the meal-offering, —As Yahweh commanded Moses.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
And he put the laver, between the tent of meeting, and the altar, —and put therein water for bathing;
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
and Moses and Aaron and his sons thenceforth bathed thereat, —their hands and their feet;
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
when they were entering into the tent of meeting, and when they were drawing near unto the altar, then used they to bathe, —As Yahweh commanded Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
And he reared the court round about to the habitation and to the altar, and put up the screen of the gate of the court, —and Moses finished the work.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Then did the cloud cover the tent of meeting, —and, the glory of Yahweh, filled the habitation;
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
and Moses was not able to enter into the tent of meeting, because the cloud had made its habitation thereupon, —and the glory of Yahweh, filled the habitation.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
And whensoever the cloud ascended from off the habitation, then did the sons of Israel set forward, in all their journeyings;
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
but if the cloud did not ascend, then did they not set forward—until the day when it did ascend.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For, the cloud of Yahweh, was upon the habitation by day, and, a fire, came to be by night therein, —in the sight of all the house of Israel in all their journeyings.