< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And YHWH speaks to Moses, saying,
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
“On the first day of the month, in the first month, you raise up the Dwelling Place of the Tent of Meeting,
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
and have set the Ark of the Testimony [in] there, and have covered over the Ark with the veil,
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
and have brought in the table, and set its arrangement in order, and have brought in the lampstand, and caused its lamps to go up.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
And you have put the golden altar for incense before the Ark of the Testimony, and have put the covering of the opening to the Dwelling Place,
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
and have put the altar of the burnt-offering before the opening of the Dwelling Place of the Tent of Meeting,
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
and have put the laver between the Tent of Meeting and the altar, and have put water [in] there.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
And you have set the court all around, and have placed the covering of the gate of the court,
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
and have taken the anointing oil, and anointed the Dwelling Place, and all that [is] in it, and hallowed it, and all its vessels, and it has been holy;
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
and you have anointed the altar of the burnt-offering, and all its vessels, and sanctified the altar, and the altar has been most holy;
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
and you have anointed the laver and its base, and sanctified it.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And you have brought Aaron and his sons near to the opening of the Tent of Meeting, and have bathed them with water;
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
and you have clothed Aaron with the holy garments, and anointed him, and sanctified him, and he has acted as priest to Me.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
And you bring his sons near, and have clothed them with coats,
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
and anointed them as you have anointed their father, and they have acted as priests to Me, and their anointing has been to them for a continuous priesthood throughout their generations.”
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses does according to all that YHWH has commanded him; so he has done.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
And it comes to pass, in the first month, in the second year, on the first of the month, the Dwelling Place has been raised up;
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
and Moses raises up the Dwelling Place, and sets its sockets, and places its boards, and places its bars, and raises its pillars,
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
and spreads the tent over the Dwelling Place, and puts the covering of the tent on it above, as YHWH has commanded Moses.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he takes and puts the Testimony into the Ark, and sets the poles on the Ark, and puts the propitiatory covering on the Ark above;
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
and brings the Ark into the Dwelling Place, and places the veil of the covering, and covers over the Ark of the Testimony, as YHWH has commanded Moses.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he puts the table in the Tent of Meeting, on the side of the Dwelling Place northward, at the outside of the veil,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and sets in order the arrangement of bread on it, before YHWH, as YHWH has commanded Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
And he puts the lampstand in the Tent of Meeting, opposite the table, on the side of the Dwelling Place southward,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and causes the lamps to go up before YHWH, as YHWH has commanded Moses.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
And he sets the golden altar in the Tent of Meeting, before the veil,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and makes incense on it—spice-incense—as YHWH has commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
And he sets the covering [at] the opening of the Dwelling Place,
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
and he has set the altar of the burnt-offering [at] the opening of the Dwelling Place of the Tent of Meeting, and causes the burnt-offering to go up on it, and the present, as YHWH has commanded Moses.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
And he puts the laver between the Tent of Meeting and the altar, and puts water [in] there for washing,
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
and Moses and Aaron and his sons have washed their hands and their feet at the same;
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
in their going into the Tent of Meeting, and in their drawing near to the altar, they wash, as YHWH has commanded Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
And he raises up the court all around the Dwelling Place, and around the altar, and places the covering of the gate of the court; and Moses completes the work.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
And the cloud covers the Tent of Meeting, and the glory of YHWH has filled the Dwelling Place;
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
and Moses has not been able to go into the Tent of Meeting, for the cloud has dwelt on it, and the glory of YHWH has filled the Dwelling Place.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
And in the going up of the cloud from off the Dwelling Place the sons of Israel journey in all their journeys;
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
and if the cloud does not go up then they do not journey, until the day of its going up.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For the cloud of YHWH [is] on the Dwelling Place by day, and fire is in it by night, before the eyes of all the house of Israel in all their journeys.

< Kutoka 40 >