< Kutoka 40 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
The first month, the first day of the month, thou shalt set up the tabernacle of the testimony,
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
And shalt put the ark in it, and shalt let down the veil before it:
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
And thou shalt bring in the table, and set upon it the things that are commanded according to the rite. The candlestick shall stand with its lamps,
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
And the altar of gold whereon the incense is burnt, before the ark of the testimony. Thou shalt put the hanging in the entry of the tabernacle,
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
And before it the altar of holocaust:
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
The laver between the altar and the tabernacle, and thou shalt fill it with water.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
And thou shalt encompass the court with hangings, and the entry thereof.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
And thou shalt take the oil of unction and anoint the tabernacle with its vessels, that they may be sanctified:
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
The altar of holocaust and all its vessels:
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
The laver with its foot: thou shalt consecrate all with the oil of unction, that they may be most holy.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And thou shalt bring Aaron and his sons to the door of the tabernacle of the testimony, and having washed them with water,
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
Thou shalt put on them the holy vestments, that they may minister to me, and that the unction of them may prosper to an everlasting priesthood.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses did all that the Lord had commanded.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
So in the first month of the second year, the first day of the month, the tabernacle was set up.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
And Moses reared it up, and placed the boards and the sockets and the bars, and set up the pillars,
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
And spread the roof over the tabernacle, putting over it a cover, as the Lord had commanded.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he put the testimony in the ark, thrusting bars underneath, and the oracle above.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
And when he had brought the ark into the tabernacle, he drew the veil before it to fulfill the commandment of the Lord.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he set the table in the tabernacle of the testimony at the north side without the veil,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Setting there in order the loaves of proposition, as the Lord had commanded Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
He set the candlestick also in the tabernacle of the testimony over against the table on the south side,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
Placing the lamps in order, according to the precept of the Lord.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
He set also the altar of gold under the roof of the testimony over against the veil,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
And burnt upon it the incense of spices, as the Lord had commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
And he put also the hanging in the entry of the tabernacle of the testimony,
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
And the altar of holocaust of the entry of the testimony, offering the holocaust, and the sacrifices upon it, as the Lord had commanded.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
And he set the laver between the tabernacle of the testimony and the altar, filling it with water.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
And Moses and Aaron, and his sons washed their hands and feet,
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
When they went into the tabernacle of the covenant, and went to the altar, as the Lord had commanded Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
He set up also the court round about the tabernacle and the altar, drawing the hanging in the entry thereof. After all things were perfected,
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
The cloud covered the tabernacle of the testimony, and the glory of the Lord filled it.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Neither could Moses go into the tabernacle of the covenant, the cloud covering all things and the majesty of the Lord shining, for the cloud had covered all.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
If at any time the cloud removed from the tabernacle, the children of Israel went forward by their troops:
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
If it hung over, they remained in the same place.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For the cloud of the Lord hung over the tabernacle by day, and a fire by night, in the sight of all the children of Israel throughout all their mansions.