< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
On the day of the first month, on the first of the month, shalt thou set up the tabernacle of the tent of meeting.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
And thou shalt put in it the ark of the testimony, and shalt cover the ark with the veil.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
And thou shalt bring in the table, and set in order the things that are to be set in order upon it. And thou shalt bring in the candlestick and light its lamps.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
And thou shalt set the golden altar for the incense before the ark of the testimony; and hang up the curtain of the entrance to the tabernacle.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
And thou shalt set the altar of burnt-offering before the entrance of the tabernacle of the tent of meeting.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
And thou shalt set the laver between the tent of meeting and the altar, and shalt put water in it.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
And thou shalt fix the court round about, and hang up the curtain at the gate of the court.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
And thou shalt take the anointing oil, and anoint the tabernacle, and all that is in it, and shalt hallow it, and all its utensils; and it shall be holy.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
And thou shalt anoint the altar of burnt-offering, and all its utensils; and thou shalt hallow the altar, and the altar shall be most holy.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
And thou shalt anoint the laver and its stand, and hallow it.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And thou shalt bring Aaron and his sons near, at the entrance of the tent of meeting, and bathe them with water.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
And thou shalt clothe Aaron with the holy garments, and anoint him, and hallow him, that he may serve me as priest.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
And thou shalt bring his sons near, and clothe them with vests.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
And thou shalt anoint them, as thou didst anoint their father, that they may serve me as priests. And their anointing shall be to them an everlasting priesthood throughout their generations.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses did so: as Jehovah had commanded him, so did he.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
And it came to pass in the first month in the second year, on the first of the month, that the tabernacle was set up.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
And Moses set up the tabernacle, and put in its bases, and fixed its boards, and put in its bars, and set up its pillars.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
And he spread the tent over the tabernacle, and put the covering of the tent above over it; as Jehovah had commanded Moses.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he took and put the testimony into the ark, and put the staves in the ark, and put the mercy-seat above on the ark.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
And he brought the ark into the tabernacle, and hung up the veil of separation, and covered the ark of the testimony; as Jehovah had commanded Moses.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he put the table in the tent of meeting, on the side of the tabernacle northward, outside the veil,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and arranged the bread in order upon it before Jehovah; as Jehovah had commanded Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
And he put the candlestick in the tent of meeting, opposite to the table, on the side of the tabernacle southward.
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
And he lighted the lamps before Jehovah; as Jehovah had commanded Moses.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
And he put the golden altar in the tent of meeting before the veil.
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
And he burnt on it fragrant incense; as Jehovah had commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
And he hung up the curtain of the entrance to the tabernacle.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
And he put the altar of burnt-offering at the entrance to the tabernacle of the tent of meeting, and offered on it the burnt-offering and the oblation; as Jehovah had commanded Moses.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
And he set the laver between the tent of meeting and the altar, and put water in it for washing.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
And Moses and Aaron and his sons washed their hands and their feet out of it:
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
when they went into the tent of meeting, and when they drew near to the altar, they washed; as Jehovah had commanded Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
And he set up the court round about the tabernacle and the altar, and hung up the curtain of the gate of the court. And so Moses finished the work.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
And the cloud covered the tent of meeting, and the glory of Jehovah filled the tabernacle.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
And Moses could not enter into the tent of meeting, for the cloud abode on it, and the glory of Jehovah filled the tabernacle.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
And when the cloud was taken up from over the tabernacle, the children of Israel journeyed in all their journeys.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
And if the cloud were not taken up, then they did not journey until the day that it was taken up.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For the cloud of Jehovah was on the tabernacle by day, and fire was in it by night, before the eyes of all the house of Israel, throughout all their journeys.

< Kutoka 40 >