< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
“In the first month, on the first day of the month, you shall raise the tabernacle of the testimony,
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
and you shall place the ark in it, and you shall release the veil before it.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
And having brought in the table, you shall place the things which were solemnly commanded upon it. The lampstand shall stand with its lamps,
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
and the altar of gold, in which the incense is burned, shall stand before the ark of the testimony. You shall place the tent at the entrance of the tabernacle,
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
and before it, the altar of holocaust.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
The washtub shall stand between the altar and the tabernacle, and you shall fill it with water.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
And you shall encompass the atrium and its entrance with hangings.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
And, having taken up the oil of unction, you shall anoint the tabernacle along with its articles, so that they may be sanctified.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
The altar of holocaust and all its vessels,
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
the washtub with its base, and all things, you shall consecrate with the oil of unction, so that they may be the Holy of holies.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And you shall bring forward Aaron and his sons to the entrance of the tabernacle of the testimony, and, having washed them with water,
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
you shall clothe them in the holy vestments, so that they may minister to me, and so that their unction may accomplish an everlasting priesthood.”
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses did all that the Lord had instructed.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
Therefore, in the first month of the second year, on the first day of the month, the tabernacle was put in place.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
And Moses raised it up, and he positioned the panels as well as the bases and the bars, and he set up the columns,
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
and he stretched out the roof over the tabernacle, imposing a cover above it, just as the Lord had decreed.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he placed the testimony in the ark, applying the bars beneath, and the oracle above.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
And when he had brought the ark into the tabernacle, he drew the veil before it, in order to fulfill the commandment of the Lord.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he placed the table in the tabernacle of the testimony, at the north side, beyond the veil,
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
arranging before it the bread of the presence, just as the Lord had instructed Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
And he placed the lampstand in the tabernacle of the testimony, away from the table, on the south side,
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
setting the lamps in order, according to the precept of the Lord.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
He also positioned the altar of gold under the roof of the testimony, opposite the veil,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and he heaped upon it the incense of aromatics, just as the Lord had commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
And he positioned the tent at the entrance of the tabernacle of the testimony,
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
and the altar of holocaust in the vestibule of the testimony, offering the holocaust and the sacrifices upon it, just as the Lord had decreed.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
Likewise, he stationed the washtub between the tabernacle of the testimony and the altar, filling it with water.
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
And Moses and Aaron, along with his sons, washed their hands and feet,
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
whenever they would enter the covering of the covenant, and when they approached to the altar, just as the Lord had instructed Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
And he raised up the atrium around the tabernacle and the altar, drawing the hanging at its entrance. After all these things were perfected,
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
the cloud covered the tabernacle of the testimony, and the glory of the Lord filled it.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Neither could Moses enter the covering of the covenant: the cloud was covering all things, and the majesty of the Lord was flashing. For the cloud had covered everything.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Whenever the cloud departed from the tabernacle, the sons of Israel set out by their companies.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
But if it remained hanging over it, they remained in the same place.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
Certainly, the cloud of the Lord lay over the tabernacle by day, and the fire by night, being seen by all the people of Israel throughout all their resting places.

< Kutoka 40 >