< Kutoka 40 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And the Lord spoke to Moses, saying,
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
On the first day of the first month, at the new moon, thou shalt set up the tabernacle of witness,
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
and thou shalt place [in it] the ark of the testimony, and shalt cover the ark with the veil,
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
and thou shalt bring in the table and shalt set forth that which is to be set forth on it; and thou shalt bring in the candlestick and place its lamps on it.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
And thou shalt place the golden altar, to burn incense before the ark; and thou shalt put a covering of a veil on the door of the tabernacle of witness.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
And thou shalt put the altar of burnt-offerings by the doors of the tabernacle of witness, and thou shalt set up the tabernacle round about, and thou shalt hallow all that belongs to it round about.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
And thou shalt take the anointing oil, and shalt anoint the tabernacle, and all things in it; and shalt sanctify it, and all its furniture, and it shall be holy.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
And thou shalt anoint the altar of burnt-offerings, and all its furniture; and thou shalt hallow the altar, and the altar shall be most holy.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And thou shalt bring Aaron and his sons to the doors of the tabernacle of witness, and thou shalt wash them with water.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
And thou shalt put on Aaron the holy garments, and thou shalt anoint him, and thou shalt sanctify him, and he shall minister to me as priest.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
And thou shalt bring up his sons, and shalt put garments on them.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
And thou shalt anoint them as thou didst anoint their father, and they shall minister to me as priests; and it shall be that they shall have an everlasting anointing of priesthood, throughout their generations.
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
And Moses did all things whatsoever the Lord commanded him, so did he.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
And it came to pass in the first month, in the second year after their going forth out of Egypt, at the new moon, that the tabernacle was set up.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
And Moses set up the tabernacle, and put on the chapiters, and put the bars into their places, and set up the posts.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
And he stretched out the curtains over the tabernacle, and put the veil of the tabernacle on it above as the Lord commanded Moses.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
And he took the testimonies, and put them into the ark; and he put the staves by the sides of the ark.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
And he brought the ark into the tabernacle, and put on [it] the covering of the veil, and covered the ark of the testimony, as the Lord commanded Moses.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
And he put the table in the tabernacle of witness, on the north side without the veil of the tabernacle.
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
And he put on it the shewbread before the Lord, as the Lord commanded Moses.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
And he put the candlestick into the tabernacle of witness, on the side of the tabernacle toward the south.
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
And he put on it its lamps before the Lord, as the Lord had commanded Moses.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
And he put the golden altar in the tabernacle of witness before the veil;
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and he burnt on it incense of composition, as the Lord commanded Moses.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
And he put the altar of the burnt-offerings by the doors of the tabernacle.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
And he set up the court round about the tabernacle and the altar; and Moses accomplished all the works.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
And the cloud covered the tabernacle of witness, and the tabernacle was filled with the glory of the Lord.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
And Moses was not able to enter into the tabernacle of testimony, because the cloud overshadowed it, and the tabernacle was filled with the glory of the Lord.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
And when the cloud went up from the tabernacle, the children of Israel prepared to depart with their baggage.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
And if the cloud went not up, they did not prepare to depart, till the day when the cloud went up.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For a cloud was on the tabernacle by day, and fire was on it by night before all Israel, in all their journeyings.

< Kutoka 40 >