< Kutoka 40 >
1 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Then the LORD said to Moses,
2 “Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
“On the first day of the first month you are to set up the tabernacle, the Tent of Meeting.
3 Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
Put the ark of the Testimony in it and screen off the ark with the veil.
4 Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
Then bring in the table and set out its arrangement; bring in the lampstand as well, and set up its lamps.
5 Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
Place the gold altar of incense in front of the ark of the Testimony, and hang the curtain at the entrance to the tabernacle.
6 “Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
Place the altar of burnt offering in front of the entrance to the tabernacle, the Tent of Meeting.
7 weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
And place the basin between the Tent of Meeting and the altar, and put water in it.
8 Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
Set up the surrounding courtyard and hang the curtain for the entrance to the courtyard.
9 “Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
Take the anointing oil and anoint the tabernacle and everything in it; consecrate it along with all its furnishings, and it shall be holy.
10 Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
Anoint the altar of burnt offering and all its utensils; consecrate the altar, and it shall be most holy.
11 Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
Anoint the basin and its stand and consecrate them.
12 “Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Then bring Aaron and his sons to the entrance to the Tent of Meeting and wash them with water.
13 Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
And you are to clothe Aaron with the holy garments, anoint him, and consecrate him, so that he may serve Me as a priest.
14 Walete wanawe na uwavike makoti.
Bring his sons forward and clothe them with tunics.
15 Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
Anoint them just as you anointed their father, so that they may also serve Me as priests. Their anointing will qualify them for a permanent priesthood throughout their generations.”
16 Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
Moses did everything just as the LORD had commanded him.
17 Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
So the tabernacle was set up on the first day of the first month of the second year.
18 Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
When Moses set up the tabernacle, he laid its bases, positioned its frames, inserted its crossbars, and set up its posts.
19 Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
Then he spread the tent over the tabernacle and put the covering over the tent, just as the LORD had commanded him.
20 Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
Moses took the Testimony and placed it in the ark, attaching the poles to the ark; and he set the mercy seat atop the ark.
21 Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
Then he brought the ark into the tabernacle, put up the veil for the screen, and shielded off the ark of the Testimony, just as the LORD had commanded him.
22 Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
Moses placed the table in the Tent of Meeting on the north side of the tabernacle, outside the veil.
23 na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
He arranged the bread on it before the LORD, just as the LORD had commanded him.
24 Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
He also placed the lampstand in the Tent of Meeting opposite the table on the south side of the tabernacle
25 na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
and set up the lamps before the LORD, just as the LORD had commanded him.
26 Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
Moses placed the gold altar in the Tent of Meeting, in front of the veil,
27 na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
and he burned fragrant incense on it, just as the LORD had commanded him.
28 Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
Then he put up the curtain at the entrance to the tabernacle.
29 Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
He placed the altar of burnt offering near the entrance to the tabernacle, the Tent of Meeting, and offered on it the burnt offering and the grain offering, just as the LORD had commanded him.
30 Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
He placed the basin between the Tent of Meeting and the altar and put water in it for washing;
31 Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
and from it Moses, Aaron, and his sons washed their hands and feet.
32 Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
They washed whenever they entered the Tent of Meeting or approached the altar, just as the LORD had commanded Moses.
33 Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
And Moses set up the courtyard around the tabernacle and the altar, and he hung the curtain for the entrance to the courtyard. So Moses finished the work.
34 Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Then the cloud covered the Tent of Meeting, and the glory of the LORD filled the tabernacle.
35 Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
Moses was unable to enter the Tent of Meeting because the cloud had settled on it, and the glory of the LORD filled the tabernacle.
36 Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
Whenever the cloud was lifted from above the tabernacle, the Israelites would set out through all the stages of their journey.
37 lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
If the cloud was not lifted, they would not set out until the day it was taken up.
38 Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.
For the cloud of the LORD was over the tabernacle by day, and fire was in the cloud by night, in the sight of all the house of Israel through all their journeys.