< Kutoka 4 >

1 Mose akamjibu, “Itakuwaje kama hawataniamini au kunisikiliza, waseme, ‘Bwana hakukutokea’?”
Odpověděl pak Mojžíš, a řekl: Aj, neuvěří mi, ani uposlechnou hlasu mého; nebo řeknou: Neukázalť se tobě Hospodin.
2 Ndipo Bwana akamwambia, “Ni nini hicho kilicho mkononi mwako?” Akajibu, “Fimbo.”
Tedy řekl jemu Hospodin: Co jest to v ruce tvé? Odpověděl: Hůl.
3 Bwana akasema, “Itupe chini.” Mose akaitupa chini hiyo fimbo nayo ikawa nyoka, naye akaikimbia.
I řekl: Vrz ji na zem. I povrhl ji na zem, a obrácena jest v hada; a utíkal Mojžíš před ním.
4 Kisha Bwana akamwambia, “Nyoosha mkono wako umkamate mkiani.” Basi Mose akanyoosha mkono akamkamata yule nyoka, naye akabadilika tena kuwa fimbo mkononi mwake.
Tedy řekl Hospodin Mojžíšovi: Vztáhni ruku svou, a chyť ho za ocas. Kterýžto vztáh ruku svou, chytil jej, a obrácen jest v hůl v rukou jeho.
5 Bwana akasema, “Hivi ndivyo Waisraeli watakavyoamini kuwa Bwana, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo, amekutokea wewe.”
Aby věřili, že se ukázal tobě Hospodin, Bůh otců jejich, Bůh Abrahamův, Bůh Izákův a Bůh Jákobův.
6 Kisha Bwana akamwambia, “Weka mkono wako ndani ya joho lako.” Basi Mose akaweka mkono wake ndani ya joho lake, naye alipoutoa, ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
Potom zase řekl jemu Hospodin: Vlož nyní ruku svou za ňadra svá. I vložil ruku svou za ňadra svá; a vyňal ji, a aj, ruka jeho byla malomocná, bílá jako sníh.
7 Mungu akamwambia, “Sasa urudishe tena huo mkono ndani ya joho lako.” Basi Mose akaurudisha mkono wake ndani ya joho lake na alipoutoa, ulikuwa mzima, kama sehemu zingine za mwili wake.
Řekl opět: Vlož ruku svou zase v ňadra svá. Kterýž vložil ruku svou zase v ňadra svá; a vyňal ji z ňader svých, a aj, učiněna jest zase jako jiné tělo jeho.
8 Ndipo Bwana akamwambia, “Kama hawatakuamini wewe, au kutojali ishara ya kwanza, wataamini ishara ya pili.
I budeť, jestliže neuvěří tobě, a neposlechnou hlasu a znamení prvního, uvěří hlasu a znamení druhému.
9 Lakini kama hawataamini ishara hizi mbili au hawatawasikiliza ninyi, chukua kiasi cha maji kutoka Mto Naili uyamimine juu ya ardhi kavu. Maji mtakayotoa mtoni yatakuwa damu juu ya ardhi.”
A pakli neuvěří ani těm dvěma znamením, a neuposlechnou hlasu tvého, tedy nabereš vody z řeky, a vyliješ ji na zem; a promění se vody, kteréž vezmeš z řeky, a obrátí se v krev na zemi.
10 Mose akamwambia Bwana, “Ee Bwana, kamwe sijapata kuwa msemaji kwa ufasaha wakati uliopita wala tangu ulipoanza kuzungumza na mtumishi wako. Ulimi wangu ni mzito kuzungumza.”
I řekl Mojžíš Hospodinu: Prosím, Pane, nejsem muž výmluvný, aniž prvé, ani jakž jsi mluvil s služebníkem svým; nebo zpozdilých úst a neohbitého jazyku jsem.
11 Bwana akamwambia, “Ni nani aliyempa mwanadamu kinywa? Ni nani aliyemfanya mtu kuwa kiziwi au bubu? Ni nani anayempa mtu kuona au upofu? Je, si mimi, Bwana?
Jemuž odpověděl Hospodin: Kdo dal ústa člověku? Aneb kdo může učiniti němého, neb hluchého, vidoucího, neb slepého? Zdali ne já Hospodin?
12 Sasa nenda, nitakusaidia kusema, nami nitakufundisha jambo la kusema.”
Nyní tedy jdi, a já budu v ústech tvých, a naučím tě, co bys mluviti měl.
13 Lakini Mose akasema, “Ee Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine kufanya kazi hiyo.”
I řekl: Slyš mne, Pane, pošli, prosím, toho, kteréhož poslati máš.
14 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Mose, akamwambia, “Vipi kuhusu ndugu yako, Aroni Mlawi? Ninajua yeye anaweza kuzungumza vizuri. Naye yuko tayari njiani kukulaki, na moyo wake utafurahi wakati atakapokuona.
A rozhněvav se velmi Hospodin na Mojžíše, řekl: Zdaliž nemáš Arona bratra svého z pokolení Léví? Vím, že on výmluvný jest; ano aj, sám vyjde v cestu tobě, a vida tebe, radovati se bude v srdci svém.
15 Utazungumza naye na kuweka maneno kinywani mwake. Nitawasaidia ninyi wawili kusema, nami nitawafundisha jambo la kufanya.
Ty mluviti budeš k němu, a vložíš slova v ústa jeho; a já budu v ústech tvých a v ústech jeho, a naučím vás, co byste měli činiti.
16 Aroni ataongea na watu badala yako na itakuwa kwamba yeye amekuwa kinywa chako nawe utakuwa kama Mungu kwake.
A on mluviti bude za tebe k lidu; a bude tobě on za ústa, a ty budeš jemu za Boha.
17 Lakini chukua fimbo hii mkononi mwako ili uweze kuitumia kufanya ishara hizo za ajabu.”
Hůl pak tuto vezmeš v ruku svou, kterouž činiti budeš ta znamení.
18 Kisha Mose akarudi kwa Yethro mkwewe akamwambia, “Niruhusu nirudi kwa watu wangu Misri kuona kama yuko hata mmoja wao ambaye bado anaishi.” Yethro akamwambia, “Nenda, nami nakutakia mema.”
Tedy odšed Mojžíš, navrátil se k Jetrovi tchánu svému, a řekl jemu: Nechť jdu nyní, a navrátím se k bratřím svým, kteříž jsou v Egyptě, a pohledím, jsou-li ještě živi. I řekl Jetro Mojžíšovi: Jdi v pokoji.
19 Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose huko Midiani, “Rudi Misri kwa maana watu wote waliotaka kukuua wamekufa.”
Nebo řekl byl Hospodin Mojžíšovi v zemi Madianské: Jdi, navrať se do Egypta; nebo zemřeli jsou všickni muži, kteříž hledali bezživotí tvého.
20 Basi Mose akamchukua mkewe na wanawe, akawapandisha juu ya punda na kuanza safari kurudi Misri. Naye akaichukua ile fimbo ya Mungu mkononi mwake.
A vzav Mojžíš ženu svou, a syny své, vsadil je na osla, aby se navrátil do země Egyptské; vzal také Mojžíš hůl Boží v ruku svou.
21 Bwana akamwambia Mose, “Utakaporudi Misri, hakikisha kwamba utafanya mbele ya Farao maajabu yote niliyokupa uwezo wa kuyafanya. Lakini nitafanya moyo wake kuwa mgumu ili kwamba asiwaruhusu watu waende.
I řekl Hospodin Mojžíšovi: Když půjdeš a navrátíš se do Egypta, hleď, abys všecky zázraky, kteréž jsem složil v ruce tvé, činil před Faraonem. Jáť pak zatvrdím srdce jeho, aby nepropustil lidu.
22 Kisha mwambie Farao, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Israeli ni mwanangu mzaliwa wa kwanza,
Protož díš Faraonovi: Toto praví Hospodin: Syn můj, prvorozený můj jest Izrael.
23 nami nilikuambia, “Ruhusu mwanangu aondoke, ili aweze kuniabudu mimi.” Lakini ukakataa kumruhusu kwenda, basi nitaua mwana wako mzaliwa wa kwanza.’”
I řekl jsem tobě: Propusť syna mého, ať slouží mi; a nechtěl jsi ho propustiti. Aj, já zabiji syna tvého, prvorozeného tvého.
24 Mose alipokuwa mahali pa kulala wageni akiwa njiani kurudi Misri, Bwana akakutana naye, akataka kumuua.
I stalo se, když byl Mojžíš na cestě v hospodě, že se obořil na něj Hospodin, a hledal ho usmrtiti.
25 Lakini Sipora akachukua jiwe gumu, akakata govi la mwanawe na kugusa nalo miguu ya Mose. Sipora akasema, “Hakika wewe ni bwana arusi wa damu kwangu.”
Tedy vzala Zefora nůž ostrý, a obřezala neobřízku syna svého, kteroužto vrhla k nohám jeho, řkuci: Zajisté ženich krví jsi mi.
26 Sipora alipomwita Mose, “Bwana arusi wa damu,” alikuwa anamaanisha ile tohara. Baada ya hayo Bwana akamwacha.
I nechal ho. Ona pak nazvala ho tehdáž ženichem krví pro obřezání.
27 Bwana akamwambia Aroni, “Nenda jangwani ukamlaki Mose.” Basi akakutana na Mose kwenye mlima wa Mungu, akambusu.
Řekl také Hospodin Aronovi: Jdi vstříc Mojžíšovi na poušť. I šel a potkal se s ním na hoře Boží, a políbil ho.
28 Kisha Mose akamwambia Aroni kila kitu Bwana alichomtuma kusema, vilevile habari za ishara na maajabu alizokuwa amemwamuru kufanya.
A vypravoval Mojžíš Aronovi všecka slova Hospodinova, kterýž ho poslal, i o všech znameních, kteráž přikázal jemu.
29 Mose na Aroni wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli,
Tedy šel Mojžíš s Aronem, a shromáždili všecky starší synů Izraelských.
30 naye Aroni akawaambia kila kitu Bwana alichokuwa amemwambia Mose. Pia akafanya ishara mbele ya watu,
I mluvil Aron všecka slova, kteráž byl mluvil Hospodin k Mojžíšovi, a činil znamení před očima lidu.
31 nao wakaamini. Nao waliposikia kuwa Bwana anajishughulisha nao, na kwamba ameona mateso yao, walisujudu na kuabudu.
A uvěřil lid, když uslyšeli, že navštívil Hospodin syny Izraelské, a že viděl ssoužení jejich. A sklonivše se, poklonu učinili.

< Kutoka 4 >