< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Men af det gula silket, skarlakanet och rosenrödt, gjorde de Aaron ämbetskläder, till att tjena i helgedomenom; såsom Herren hade budit Mose.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
Och han gjorde lifkjortelen af guld, gult silke, skarlakan, rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke;
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
Och utslog guldet, och skar det i trådar, så att man kunde konsteliga virka det in med det gula silket, skarlakan, rosenrödt, och hvita silket;
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
Och gjorde så, att man sammanfogade honom på båda axlar, och band honom tillhopa på båda sidor.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Och bältet var af samma konst och verk, af guld, gult silke, skarlakan, rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke; såsom Herren hade budit Mose.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
Och de tillredde två onichinerstenar, omfattade i guld; utgrafna af stensnidare med Israels barnas namn;
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Och fäste dem på axlarna af lifkjortelen, att de skulle vara åminnelsestenar till Israels barn; såsom Herren Mose budit hade.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Och de gjorde skölden efter den konst och verk, som lifkjortelen var, af guld, gult silke, skarlakan, rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke;
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
Så att han var fyrakant och tvefald, en hand lång och bred;
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Och fyllde honom med fyra radar stenar. Den första raden var en sarder, topaz och smaragd;
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
Den andra, en rubin, saphir och diamant;
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
Den tredje, en lyncurer, achat och amethist;
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
Den fjerde, en turkos, onicher och jaspis; omfattade i guld i alla radarna.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Och stenarna stodo grafne af stensnidarena, efter de tolf Israels barnas namn; hvardera af sitt namn, efter de tolf slägten.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Och de gjorde till skölden kedjor uppåt af klart guld;
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Och tu gyldene spänner, och två gyldene ringar; och fäste de två ringar vid tu hörnen af skölden.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Och de två gyldene kedjorna satte de uti de två ringar på hörnen af skölden.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Men de två ändar af de gyldene kedjor läto de komma intill de tu spännen; och hakade dem intill hörnen af lifkjortelen tvärtemot hvartannat;
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Och gjorde två andra gyldene ringar, och knäppte dem vid de andra tu hörnen af skölden nedantill, så att han låg hardt inpå lifkjortelen;
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Och gjorde två andra gyldene ringar; dem gjorde de på tu hörnen nedantill på lifkjortelen, tvärtemot hvarannan, der lifkjortelen nedantill sammangår.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Och vardt skölden med sina ringar knäppt intill lifkjortelens ringar med ett gult snöre, så att det låg hardt intill lifkjortelen, och icke for löst ifrå lifkjortelen; såsom Herren hade budit Mose.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
Och han gjorde silkeskjortelen under lifkjortelen, den all virkad var med gult silke;
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
Och hans hufvudsmog midt ofvanuppå, och en borda omkring hufvudsmoget fållad, att det icke skulle gå sönder.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
Och de gjorde på hans fåll granatäple af gult silke, skarlakan, rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke:
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
Och gjorde bjellror af klart guld; dem satte de emellan de granatäplen allt omkring på fållen af den silkeskjortelen;
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Ju ett granatäple, och en bjellra allt omkring, till att tjena deruti; såsom Herren hade budit Mose;
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
Och gjorde desslikes den trånga kjortelen, virkad af hvitt silke, till Aaron och hans söner;
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
Och hatten af hvitt silke, och sköna hufvor af hvitt silke, och nederklädet af tvinnadt hvitt linne;
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Och det stickade bältet af tvinnadt hvitt silke, gult silke, skarlakan, rosenrödt; såsom Herren hade budit Mose.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
De gjorde ock ännespannet på den helga kronona af klart guld, och grofvo skrift deruppå: Herrans HELIGHET;
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Och bundo ett gult snöre dervid, att det måtte knäppas ofvanpå hatten; såsom Herren hade budit Mose.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
Alltså vardt fullbordadt hela verket till vittnesbördsens tabernakels boning. Och Israels barn gjorde allt det Herren hade budit Mose;
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
Och hade boningen till Mose, tabernaklet och all dess redskap, spänner, bräder, skottstänger, stolpar, fötter;
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
Täckelset af rödlett vädurskinn; täckelset af tackskinn, och förlåten;
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
Vittnesbördsens ark med sina stänger; nådastolen;
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
Bordet med all dess redskap, och skådobröden;
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
Den sköna ljusastakan, tillreddan med lamporna, och all sin redskap, och oljo till lysning;
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
Gyldene altaret och smörjelsen, och godt rökverk; klädet i tabernaklets dörr;
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
Kopparaltaret och dess koppargallrar, med sina stänger, och all sin redskap; tvättekaret med sin fot;
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
Bonaden till gården med sina stolpar och fötter, klädet till ingången åt gårdenom med sin tåg och pålar, och all redskap som behöfdes till boningenes tjenst, vittnesbördsens tabernakels;
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
Aarons Prestens ämbetskläder till att tjena i helgedomenom; och hans söners kläder, till att de skulle göra Prestaämbetet.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
All ting, såsom Herren hade budit Mose, gjorde Israels barn till alla denna tjenstena.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
Och Mose såg på allt detta verket, att de gjorde såsom Herren budit hade, och välsignade dem.

< Kutoka 39 >