< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و از لاجورد و ارغوان و قرمز رختهای بافته شده ساختند، برای خدمت کردن در قدس، و رختهای مقدس برای هارون ساختند، چنانکه خداوند به موسی‌امر نموده بود.۱
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
و ایفود را از طلا و لاجورد و ارغوان و قرمزو کتان نازک تابیده شده، ساخت.۲
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
و تنگه های نازک از طلا ساختند و تارها کشیدند تا آنها را درمیان لاجورد و ارغوان و قرمز و کتان نازک به صنعت نساج ماهر ببافند.۳
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
و کتفهای پیوسته شده برایش ساختند، که بر دو کنار پیوسته شد.۴
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و زنار بسته شده‌ای که بر آن بود از همان پارچه واز همان صنعت بود، از طلا و لاجورد و ارغوان وقرمز و کتان نازک تابیده شده، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود.۵
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
و سنگهای جزع مرصع در دو طوق طلا، و منقوش به نقش خاتم، موافق نامهای بنی‌اسرائیل درست کردند.۶
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
آنها را بر کتفهای ایفود نصب کرد، تا سنگهای یادگاری برای بنی‌اسرائیل باشد، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود.۷
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
و سینه بند را موافق کار ایفود از صنعت نساج ماهر ساخت، از طلا و لاجورد و ارغوان وقرمز و کتان نازک تابیده شده.۸
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
و آن مربع بود وسینه بند را دولا ساختند طولش یک وجب وعرضش یک وجب دولا.۹
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
و در آن چهار رسته سنگ نصب کردند، رسته‌ای از عقیق سرخ ویاقوت زرد و زمرد. این بود رسته اول.۱۰
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
و رسته دوم از بهرمان و یاقوت کبود و عقیق سفید.۱۱
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
ورسته سوم از عین الهر و یشم و جمست.۱۲
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
ورسته چهارم از زبرجد و جزع و یشب در ترصیعه خود که به دیوارهای طلا احاطه شده بود.۱۳
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
وسنگها موافق نامهای بنی‌اسرائیل دوازده بود، مطابق اسامی ایشان، مثل نقش خاتم، هر یکی به اسم خود برای دوازده سبط.۱۴
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
و بر سینه بندزنجیرهای تابیده شده، مثل کار طنابها از طلای خالص ساختند.۱۵
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
و دو طوق زرین و دو حلقه زرین ساختند و دو حلقه را بر دو سر سینه بندگذاشتند.۱۶
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
و آن دو زنجیر تابیده شده زرین رادر دو حلقه‌ای که بر سرهای سینه بند بود، گذاشتند.۱۷
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
و دو سر دیگر آن دو زنجیر را بر دوطوق گذاشتند، و آنها را بر دو کتف ایفود در‌پیش نصب کردند.۱۸
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
و دو حلقه زرین ساختند، آنها رابر دو سر سینه بند گذاشتند، بر کناری که بر طرف اندرونی‌ایفود بود.۱۹
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
و دو حلقه زرین دیگرساختند، و آنها را بر دو کتف ایفود، به طرف پایین، از جانب پیش، مقابل پیوستگیش بالای زنار ایفود گذاشتند.۲۰
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و سینه بند را به حلقه هایش با حلقه های ایفود به نوار لاجوردی بستند، تا بالای زنار ایفود باشد. و سینه بند از ایفود جدا نشود، چنانکه خداوند به موسی‌امرفرموده بود.۲۱
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
و ردای ایفود را از صنعت نساج، تمام لاجوردی ساخت.۲۲
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
و دهنه‌ای در وسط ردابود، مثل دهنه زره با حاشیه‌ای گرداگرد دهنه تادریده نشود.۲۳
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
و بر دامن ردا، انارها از لاجورد وارغوان و قرمز و کتان تابیده شده ساختند.۲۴
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
وزنگوله‌ها از طلای خالص ساختند. و زنگوله‌ها رادر میان انارها بر دامن ردا گذاشتند، گرداگردش درمیان انارها.۲۵
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و زنگوله‌ای و اناری، و زنگوله‌ای واناری گرداگرد دامن ردا برای خدمت کردن، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود.۲۶
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
وپیراهنها را برای هارون و پسرانش از کتان نازک ازصنعت نساج ساختند.۲۷
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
و عمامه را از کتان نازک و دستارهای زیبا را از کتان نازک، و زیرجامهای کتانی را از کتان نازک تابیده شده.۲۸
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و کمربند رااز کتان نازک تابیده شده، و لاجورد و ارغوان وقرمز از صنعت طراز، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود.۲۹
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
و تنگه افسر مقدس را ازطلای خالص ساختند، و بر آن کتابتی مثل نقش خاتم مرقوم داشتند: قدوسیت برای یهوه.۳۰
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
و برآن نواری لاجوردی بستند تا آن را بالای عمامه ببندند، چنانکه خداوند به موسی‌امر فرموده بود.۳۱
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
پس همه کار مسکن خیمه اجتماع تمام شد، و بنی‌اسرائیل ساختند. موافق آنچه خداوندبه موسی‌امر فرموده بود، عمل نمودند.۳۲
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
ومسکن خیمه را نزد موسی آوردند، با همه اسبابش و تکمه‌ها و تخته‌ها و پشت بندها وستونها و پایه هایش.۳۳
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
و پوشش از پوست قوچ سرخ شده و پوشش از پوست خز و حجاب ستر.۳۴
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
و تابوت شهادت و عصاهایش و کرسی رحمت.۳۵
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
و خوان و همه اسبابش و نان تقدمه.۳۶
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
و چراغدان طاهر و چراغهایش، چراغهای آراسته شده و همه اسبابش، و روغن برای روشنایی.۳۷
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
و مذبح زرین و روغن مسح و بخورمعطر و پرده برای دروازه خیمه.۳۸
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
و مذبح برنجین و شبکه برنجین آن، و عصاهایش و همه اسبابش و حوض و پایه‌اش.۳۹
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
و پرده های صحن و ستونها و پایه هایش و پرده دروازه صحن، وطنابهایش و میخهایش و همه اسباب خدمت مسکن برای خیمه اجتماع.۴۰
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
و رختهای بافته شده برای خدمت قدس، و رخت مقدس برای هارون کاهن، و رختها برای پسرانش تا کهانت نمایند.۴۱
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
موافق آنچه خداوند به موسی‌امرفرموده بود، بنی‌اسرائیل همچنین تمام کار راساختند.۴۲
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
و موسی تمام کارها را ملاحظه کرد، و اینک موافق آنچه خداوند امر فرموده بودساخته بودند، همچنین کرده بودند. و موسی ایشان را برکت داد.۴۳

< Kutoka 39 >