< Kutoka 39 >
1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Avec la pourpre, l'écarlate et le cramoisi ils firent les vêtements du service, pour faire le service dans le sanctuaire, et ils firent les vêtements sacrés qui étaient pour Aaron, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
On fit donc l'éphod d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors.
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
On étendit des lames d'or, et on les coupa en fils pour les mêler à la pourpre, à l'écarlate, au cramoisi et au fin lin, en ouvrage d'art.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
On fit à l'éphod des épaulettes qui se joignaient; il se joignait ainsi par ses deux extrémités.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et la ceinture pour l'attacher, qui se trouvait par-dessus, était de la même pièce et du même ouvrage: d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
Et l'on enchâssa dans des chatons d'or, les pierres d'onyx, portant les noms des enfants d'Israël gravés en gravure de cachet.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et on les mit sur les épaulettes de l'éphod, pour être des pierres de mémorial pour les enfants d'Israël, comme l' Éternel l'avait commandé à Moïse.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
On fit aussi le pectoral en ouvrage d'art, comme l'ouvrage de l'éphod: or, pourpre, écarlate, cramoisi et fin lin retors.
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
Il était carré. L'on fit le pectoral double; sa longueur était d'un empan, et sa largeur d'un empan, en double.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Et on le garnit de quatre rangs de pierres: au premier rang, une sardoine, une topaze et une émeraude;
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
Au second rang, une escarboucle, un saphir et une calcédoine;
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
Au troisième rang, une opale, une agate et une améthyste;
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
Au quatrième rang, un chrysolithe, un onyx et un jaspe. Ces pierres furent entourées de chatons d'or dans leurs montures.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Et les pierres, selon les noms des enfants d'Israël, étaient au nombre de douze, d'après leurs noms; elles portaient, en gravure de cachet, chacune le nom d'une des douze tribus.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Puis l'on fit sur le pectoral des chaînettes tordues en façon de cordons en or pur.
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
On fit aussi deux agrafes d'or et deux anneaux d'or, et on mit les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Et l'on mit les deux cordons aux deux anneaux, aux extrémités du pectoral.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Et l'on mit les deux extrémités des deux cordons aux deux agrafes, sur les épaulettes de l'éphod, sur le devant.
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
On fit aussi deux autres anneaux d'or, et on les mit aux deux autres extrémités du pectoral sur le bord, qui était du côté de l'éphod, en dedans.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
On fit encore deux autres anneaux d'or, et on les mit aux deux épaulettes de l'éphod par le bas, sur le devant, à côté de l'endroit où il se joint, au-dessus de la ceinture de l'éphod.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et on attacha le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l'éphod, avec un cordon de pourpre, afin qu'il tînt sur la ceinture de l'éphod, et que le pectoral ne se détachât pas de l'éphod, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
On fit aussi la robe de l'éphod en tissu simple, entièrement de pourpre.
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
Et l'ouverture pour passer la tête, au milieu de la robe, était comme l'ouverture d'une cotte d'armes; il y avait une bordure à son ouverture, tout autour, afin qu'elle ne se déchirât point.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
Et l'on mit aux bords de la robe des grenades de pourpre, d'écarlate et de cramoisi, en fil retors.
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
On fit aussi des clochettes d'or pur; et l'on mit les clochettes entre les grenades aux bords de la robe, tout autour, entre les grenades:
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Une clochette et une grenade, une clochette et une grenade, aux bords de la robe, tout autour, pour faire le service, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
On fit aussi les tuniques de fin lin, en tissu simple, pour Aaron et pour ses fils.
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
Et la tiare de fin lin, et les ornements des mitres de fin lin, et les caleçons de lin, de fin lin retors;
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et la ceinture de fin lin retors, de pourpre, d'écarlate et de cramoisi, en tissu de broderie, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
On fit aussi d'or pur la lame, la couronne sainte, et l'on y écrivit, d'une écriture en gravure de cachet: SAINTETÉ A L'ÉTERNEL.
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et on y mit un cordon de pourpre, pour la mettre sur la tiare, en haut, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
Ainsi fut achevé tout l'ouvrage de la Demeure, du tabernacle d'assignation; et les enfants d'Israël firent selon tout ce que l'Éternel avait commandé à Moïse; ils firent ainsi.
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
Et ils apportèrent la Demeure à Moïse, le tabernacle, et tous ses ustensiles, ses crochets, ses planches, ses traverses, ses colonnes et ses soubassements;
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
La couverture de peaux de béliers teintes en rouge, et la couverture de peaux de couleur d'hyacinthe, et le voile de tenture;
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
L'arche du Témoignage et ses barres, et le propitiatoire;
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
La table avec tous ses ustensiles, et le pain de proposition,
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
Le chandelier pur, avec les lampes, les lampes arrangées, et tous ses ustensiles, et l'huile du luminaire;
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
L'autel d'or, l'huile de l'onction, le parfum d'aromates, et la tapisserie de l'entrée du tabernacle,
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
L'autel d'airain et sa grille d'airain, avec ses barres, et tous ses ustensiles, la cuve et sa base,
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
Les tentures du parvis, ses colonnes, ses soubassements, la tapisserie pour la porte du parvis, ses cordes, ses pieux, et tous les ustensiles du service de la Demeure, pour le tabernacle d'assignation;
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
Les vêtements du service, pour faire le service dans le sanctuaire, les vêtements sacrés pour Aaron le sacrificateur, et les vêtements de ses fils pour exercer la sacrificature.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
Les enfants d'Israël avaient fait toute la tâche, suivant tout ce que l'Éternel avait commandé à Moïse.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
Et Moïse vit tout l'ouvrage, et voici, ils l'avaient fait tel que l'Éternel l'avait commandé; ils l'avaient fait ainsi; et Moïse les bénit.