< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Avec les étoffes teintes en bleu, en pourpre et en cramoisi, on fit les vêtements d’office pour le service dans le sanctuaire, et on fit les vêtements sacrés pour Aaron, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
On fit l’éphod d’or, de fil bleu, pourpre et cramoisi, et de fin lin retors.
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
On étendit des lames d’or, et on les coupa en fils, que l’on entrelaça dans les étoffes teintes en bleu, en pourpre et en cramoisi, et dans le fin lin; il était artistement travaillé.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
On y fit des épaulettes qui le joignaient, et c’est ainsi qu’il était joint par ses deux extrémités.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
La ceinture était du même travail que l’éphod et fixée sur lui; elle était d’or, de fil bleu, pourpre et cramoisi, et de fin lin retors, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
On entoura de montures d’or des pierres d’onyx, sur lesquelles on grava les noms des fils d’Israël, comme on grave les cachets.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
On les mit sur les épaulettes de l’éphod, en souvenir des fils d’Israël, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
On fit le pectoral, artistement travaillé, du même travail que l’éphod, d’or, de fil bleu, pourpre et cramoisi, et de fin lin retors.
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
Il était carré; on fit le pectoral double: sa longueur était d’un empan, et sa largeur d’un empan; il était double.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
On le garnit de quatre rangées de pierres: première rangée, une sardoine, une topaze, une émeraude;
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
seconde rangée, une escarboucle, un saphir, un diamant;
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
troisième rangée, une opale, une agate, une améthyste;
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
quatrième rangée, une chrysolithe, un onyx, un jaspe. Ces pierres étaient enchâssées dans leurs montures d’or.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Il y en avait douze, d’après les noms des fils d’Israël; elles étaient gravées comme des cachets, chacune avec le nom de l’une des douze tribus.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
On fit sur le pectoral des chaînettes d’or pur, tressées en forme de cordons.
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
On fit deux montures d’or et deux anneaux d’or, et on mit les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
On passa les deux cordons d’or dans les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral;
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
on arrêta par devant les bouts des deux cordons aux deux montures placées sur les épaulettes de l’éphod.
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
On fit encore deux anneaux d’or, que l’on mit aux deux extrémités du pectoral, sur le bord intérieur appliqué contre l’éphod.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
On fit deux autres anneaux d’or, que l’on mit au bas des deux épaulettes de l’éphod, sur le devant, près de la jointure, au-dessus de la ceinture de l’éphod.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
On attacha le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l’éphod avec un cordon bleu, afin que le pectoral fût au-dessus de la ceinture de l’éphod et qu’il ne pût pas se séparer de l’éphod, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
On fit la robe de l’éphod, tissée entièrement d’étoffe bleue.
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
Il y avait, au milieu de la robe, une ouverture comme l’ouverture d’une cotte de mailles, et cette ouverture était bordée tout autour, afin que la robe ne se déchirât pas.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
On mit sur la bordure de la robe des grenades de couleur bleue, pourpre et cramoisi, en fil retors;
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
on fit des clochettes d’or pur, et on mit les clochettes entre les grenades, sur tout le tour de la bordure de la robe, entre les grenades:
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
une clochette et une grenade, une clochette et une grenade, sur tout le tour de la bordure de la robe, pour le service, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
On fit les tuniques de fin lin, tissées, pour Aaron et pour ses fils;
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
la tiare de fin lin, et les bonnets de fin lin servant de parure; les caleçons de lin, de fin lin retors;
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
la ceinture de fin lin retors, brodée, et de couleur bleue, pourpre et cramoisi, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
On fit d’or pur la lame, diadème sacré, et l’on y écrivit, comme on grave un cachet: Sainteté à l’Éternel.
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
On l’attacha avec un cordon bleu à la tiare, en haut, comme l’Éternel l’avait ordonné à Moïse.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
Ainsi furent achevés tous les ouvrages du tabernacle, de la tente d’assignation. Les enfants d’Israël firent tout ce que l’Éternel avait ordonné à Moïse; ils firent ainsi.
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
On amena le tabernacle à Moïse: la tente et tout ce qui en dépendait, les agrafes, les planches, les barres, les colonnes et les bases;
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
la couverture de peaux de béliers teintes en rouge, la couverture de peaux de dauphins, et le voile de séparation;
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
l’arche du témoignage et ses barres, et le propitiatoire;
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
la table, tous ses ustensiles, et les pains de proposition;
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
le chandelier d’or pur, ses lampes, les lampes préparées, tous ses ustensiles, et l’huile pour le chandelier;
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
l’autel d’or, l’huile d’onction et le parfum odoriférant, et le rideau de l’entrée de la tente;
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
l’autel d’airain, sa grille d’airain, ses barres, et tous ses ustensiles; la cuve avec sa base;
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
les toiles du parvis, ses colonnes, ses bases, et le rideau de la porte du parvis, ses cordages, ses pieux, et tous les ustensiles pour le service du tabernacle, pour la tente d’assignation;
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
les vêtements d’office pour le sanctuaire, les vêtements sacrés pour le sacrificateur Aaron, et les vêtements de ses fils pour les fonctions du sacerdoce.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
Les enfants d’Israël firent tous ces ouvrages, en se conformant à tous les ordres que l’Éternel avait donnés à Moïse.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
Moïse examina tout le travail; et voici, ils l’avaient fait comme l’Éternel l’avait ordonné, ils l’avaient fait ainsi. Et Moïse les bénit.

< Kutoka 39 >