< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and from [the] blue and [the] purple and worm [the] scarlet to make garment braiding to/for to minister in/on/with Holy Place and to make [obj] garment [the] Holy Place which to/for Aaron like/as as which to command LORD [obj] Moses
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
and to make [obj] [the] ephod gold blue and purple and worm scarlet and linen to twist
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
and to beat [obj] plate [the] gold and to cut cord to/for to make: do in/on/with midst [the] blue and in/on/with midst [the] purple and in/on/with midst worm [the] scarlet and in/on/with midst [the] linen deed: work to devise: design
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
shoulder to make to/for him to unite upon two (end his *Q(K)*) to unite
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and artwork ephod his which upon him from him he/she/it like/as deed: work his gold blue and purple and worm scarlet and linen to twist like/as as which to command LORD [obj] Moses
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
and to make [obj] stone [the] onyx to turn: surround filigree gold to engrave engraving signet upon name son: child Israel
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and to set: make [obj] them upon shoulder [the] ephod stone memorial to/for son: child Israel like/as as which to command LORD [obj] Moses
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
and to make [obj] [the] breastpiece deed: work to devise: design like/as deed: work ephod gold blue and purple and worm scarlet and linen to twist
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
to square to be to double to make [obj] [the] breastpiece span length his and span width his to double
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
and to fill in/on/with him four row stone row sardius topaz and gem [the] row [the] one
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
and [the] row [the] second emerald sapphire and jasper
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
and [the] row [the] third jacinth agate and amethyst
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
and [the] row [the] fourth jasper onyx and jasper to turn: surround filigree gold in/on/with setting their
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
and [the] stone upon name son: child Israel they(fem.) two ten upon name their engraving signet man: anyone upon name his to/for two ten tribe
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
and to make upon [the] breastpiece chain twists deed: work cord gold pure
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
and to make two filigree gold and two ring gold and to give: put [obj] two [the] ring upon two end [the] breastpiece
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
and to give: put two [the] cord [the] gold upon two [the] ring upon end [the] breastpiece
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
and [obj] two end two [the] cord to give: put upon two [the] filigree and to give: put them upon shoulder [the] ephod to(wards) opposite face: before his
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
and to make two ring gold and to set: put upon two end [the] breastpiece upon lip: edge his which to(wards) side: beside [the] ephod house: inside [to]
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
and to make two ring gold and to give: put them upon two shoulder [the] ephod from to/for beneath from opposite face: before his to/for close joining his from above to/for artwork [the] ephod
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and to bind [obj] [the] breastpiece from ring his to(wards) ring [the] ephod in/on/with cord blue to/for to be upon artwork [the] ephod and not to remove [the] breastpiece from upon [the] ephod like/as as which to command LORD [obj] Moses
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
and to make [obj] robe [the] ephod deed: work to weave entire blue
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
and lip: opening [the] robe in/on/with midst his like/as lip: opening breastplate lip: edge to/for lip: opening his around not to tear
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
and to make upon hem [the] robe pomegranate blue and purple and worm scarlet to twist
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
and to make bell gold pure and to give: put [obj] [the] bell in/on/with midst [the] pomegranate upon hem [the] robe around in/on/with midst [the] pomegranate
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
bell and pomegranate bell and pomegranate upon hem [the] robe around to/for to minister like/as as which to command LORD [obj] Moses
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
and to make [obj] [the] tunic linen deed: work to weave to/for Aaron and to/for son: child his
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
and [obj] [the] turban linen and [obj] headdress [the] headgear linen and [obj] undergarment [the] linen linen to twist
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and [obj] [the] girdle linen to twist and blue and purple and worm scarlet deed: work to weave like/as as which to command LORD [obj] Moses
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
and to make [obj] flower consecration: crown [the] holiness gold pure and to write upon him writing engraving signet holiness to/for LORD
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and to give: put upon him cord blue to/for to give: put upon [the] turban from to/for above [to] like/as as which to command LORD [obj] Moses
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
and to end: finish all service: work tabernacle tent meeting and to make: do son: descendant/people Israel like/as all which to command LORD [obj] Moses so to make: do
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
and to come (in): bring [obj] [the] tabernacle to(wards) Moses [obj] [the] tent and [obj] all article/utensil his clasp his board his (bar his *Q(K)*) and pillar his and socket his
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
and [obj] covering skin [the] ram [the] to redden and [obj] covering skin [the] leather and [obj] curtain [the] covering
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
[obj] ark [the] testimony and [obj] alone: pole his and [obj] [the] mercy seat
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
[obj] [the] table [obj] all article/utensil his and [obj] food: bread [the] face
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
[obj] [the] lampstand [the] pure [obj] lamp her lamp [the] rank and [obj] all article/utensil her and [obj] oil [the] light
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
and [obj] altar [the] gold and [obj] oil [the] anointing and [obj] incense [the] spice and [obj] covering entrance [the] tent
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
[obj] altar [the] bronze and [obj] grate [the] bronze which to/for him [obj] alone: pole his and [obj] all article/utensil his [obj] [the] basin and [obj] stand his
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
[obj] curtain [the] court [obj] pillar her and [obj] socket her and [obj] [the] covering to/for gate [the] court [obj] cord his and peg her and [obj] all article/utensil service: ministry [the] tabernacle to/for tent meeting
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
[obj] garment [the] braiding to/for to minister in/on/with Holy Place [obj] garment [the] Holy Place to/for Aaron [the] priest and [obj] garment son: child his to/for to minister
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
like/as all which to command LORD [obj] Moses so to make: do son: descendant/people Israel [obj] all [the] service: work
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
and to see: see Moses [obj] all [the] work and behold to make: do [obj] her like/as as which to command LORD so to make: do and to bless [obj] them Moses

< Kutoka 39 >