< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And of the blue, and purple, and scarlet yarn, they made the cloths of service, to do the service in the holy place; and they made the holy garments which were for Aaron, as the Lord had commanded Moses.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
And he made the ephod, of gold, blue, and purple, and scarlet yarn, and twisted linen;
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
And they did heat the gold into thin plates, and cut it into wires, to work it in the blue, and in the purple, and in the scarlet yarn, and in the linen, with weaver's work.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
They made shoulder-pieces for it, joined on; on both its edges was it thus joined together.
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And the belt for girding it on, that was upon it, was of the same piece with itself, of the same make: of gold, blue, and purple, and scarlet yarn, and twisted linen; as the Lord had commanded Moses.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
And they wrought the onyx stones enclosed in casings of gold, engraved with the engraving of a signet, after the names of the children of Israel.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And he put them on the shoulder-pieces of the ephod, as stones of memorial to the children of Israel; as the Lord had commanded Moses.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
And he made the breastplate with weaver's work, like the work of the ephod: of gold, blue, and purple, and scarlet yarn, and twisted linen.
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
It was foursquare, double did they make the breastplate: it was a span in length, and a span in breadth, double.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
And they set in it four rows of stones: the first row, a sardius, a topaz, and an emerald; this was the first row.
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
And the second row, a carbuncle, a sapphire, and a diamond.
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
And the third row, an opal, a turquoise, and an amethyst.
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
And the fourth row, a chrysolite, an onyx, and a jasper: they were fitted in golden casings when they were set in.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
And the stones were according to the names of the children of Israel, twelve, according to their names, [engraved] with the engraving of a signet, every one according to his name, for the twelve tribes.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
And they made upon the breastplate chains with knots at the ends, of wreathed work, of pure gold.
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
And they made two casings of gold, and two golden rings; and they put the two rings on the two ends of the breastplate.
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
And they put the two wreathed chains of gold in the two rings on the ends of the breastplate.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
And the two ends of the two wreathed chains they fastened on the two casings, and they put them on the shoulder-pieces of the ephod, on the outside thereof.
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
And they made two golden rings, and put them on the two ends of the breastplate, on its border, which was on the opposite side of the ephod, inward.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
And they made two more golden rings, and put them on the two shoulder-pieces of the ephod underneath, toward its front part, close by its seam, above the girdle of the ephod.
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And they fastened the breastplate by its rings unto the rings of the ephod with a lace of blue, that it might remain on the girdle of the ephod, and that the breastplate might not be loosed from the ephod; as the Lord had commanded Moses.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
And he made the robe of the ephod of woven work, altogether of blue woolen yarn.
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
And there was an opening in the midst of the robe, as the opening of a habergeon, with a binding round about the opening, that it should not be rent.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
And they made upon the lower hem of the robe pomegranates of blue, and purple, and scarlet yarn, twisted.
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
And they made bells of pure gold; and they put the bells between the pomegranates upon the lower hem of the robe, round about, between the pomegranates;
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
A bell and a pomegranate, a bell and a pomegranate, round about the lower hem of the robe, to minister therein; as the Lord had commanded Moses.
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
And they made the coats of linen, of woven work, for Aaron and for his sons,
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
And the mitre of linen, and the goodly bonnets of linen, and linen breeches of twisted linen thread.
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And the girdle of twisted linen, and blue, and purple, and scarlet yarn, the work of the embroiderer; as the Lord had commanded Moses.
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
And they made the plate of the holy crown of pure gold, and wrote upon it a writing, like the engrafting of a signet, Holy to the Lord.
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And they put on it a lace of blue, to place it upon the mitre above; as the Lord had commanded Moses.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
Thus was finished all the work of the tabernacle of the tent of the congregation; and the children of Israel had made it in accordance with all that the Lord had commanded Moses, so had they made it.
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
And they brought the tabernacle unto Moses, the tent, and all its vessels, its hooks, its boards, its bars, and its pillars, and its sockets,
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
And the covering of rams' skins dyed red, and the covering of badgers' skins, and the vail of the separation:
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
The ark of the testimony, and its staves, and the mercy-seat;
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
The table, and all its vessels, and the showbread;
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
The pure candlestick, with its lamps, the lamps to be set in order thereupon, and all its vessels, and the oil for the lighting,
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
And the golden altar, and the anointing oil, and the incense of spices, and the hanging for the door of the tabernacle;
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
The copper altar, and the grating of copper which belonged to it, its staves, and all its vessels, the laver and its foot;
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
The hangings of the court, its pillars and its sockets, and the hanging for the court-gate, its cords, and its pins, and all the vessels of the service of the tabernacle, for the tent of the congregation;
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
The cloths of service to do the service in the holy place, and the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister therein.
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
All, just as the Lord had commanded Moses, so had the children of Israel done all the work.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
And Moses did look over all the work, and, behold, they had done it as the Lord had commanded, even so had they done it: and Moses blessed them.

< Kutoka 39 >