< Kutoka 39 >

1 Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Truly, from hyacinth and purple, vermillion and fine linen, he made the vestments with which Aaron was clothed when he ministered in the holy places, just as the Lord instructed Moses.
2 Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
And so he made an ephod of gold, hyacinth, and purple, and twice-dyed scarlet, and fine twisted linen,
3 Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
wrought with embroidery. And he cut thin strips of gold and drew them into threads, so that they could be twisted into the weave of the first colors.
4 Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
And he made two edges, coupled to one another at the top of both sides,
5 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and a wide belt from the same colors, just as the Lord had instructed Moses.
6 Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
He also prepared two onyx stones, set and enclosed in gold, and engraved with the skill of a jeweler, with the names of the sons of Israel.
7 Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And he set them in the sides of the ephod, as a memorial to the sons of Israel, just as the Lord had instructed Moses.
8 Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
He also made a breastplate, wrought with embroidery, according to the work of the ephod, from gold, hyacinth, purple, and twice-dyed scarlet, and fine twisted linen:
9 Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
with four equal sides, doubled, of the measure of the palm of a hand.
10 Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
And he set four rows of gems in it. In the first row was a sardius stone, a topaz, an emerald;
11 safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
in the second was a garnet, a sapphire, and a jasper;
12 safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
in the third was a zircon, an agate, and an amethyst;
13 katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
in the fourth was a chrysolite, an onyx, and a beryl, surrounded and enclosed in gold by their rows.
14 Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
And these twelve stones were engraved with the names of the twelve tribes of Israel, each one with a single name.
15 Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
They also made, in the breastplate, little chains linked to one another, from the purest gold,
16 Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
and two hooks, and the same number of gold rings. Moreover, they set the rings at both sides of the breastplate,
17 Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
from which two golden chains would hang, which they connected with the hooks that projected from the corners of the ephod.
18 nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
These were both in front and in back so that they met one another, and so that the ephod and the breastplate were woven together,
19 Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
being fastened to the wide belt and strongly coupled with rings, to which a hyacinth band was joined, lest they should shake loose and be moved away from one another, just as the Lord instructed Moses.
20 Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
They also made the tunic of the ephod entirely from hyacinth,
21 Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
with the head in the upper part at the middle, and a woven edge all around the head.
22 Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
Then, at the feet below, they also made pomegranates from hyacinth, purple, vermillion, and fine twisted linen,
23 na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
and little bells from the purest gold, which they set between the pomegranates at the very bottom of the tunic all around.
24 Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
So then, the high priest approached, adorned with gold bell and pomegranate, when he performed his ministry, just as the Lord had instructed Moses.
25 Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
They also made fine linen tunics with woven work, for Aaron and his sons,
26 Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
and headdresses with their little crowns of fine linen,
27 Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
and also linen undergarments of fine linen.
28 na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
Truly, they also made a wide band of fine twisted linen, hyacinth, purple, as well as vermillion, twice-dyed, with skillful embroidery, just as the Lord had instructed Moses.
29 Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
They also made the plate of sacred veneration from the purest gold, and they wrote on it, with the skill of a jeweler: “Holy to the Lord.”
30 Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
And they fastened it to the headdress with a hyacinth band, just as the Lord had instructed Moses.
31 Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
And so all the work of the tabernacle and of the covering of the testimony was completed. And the sons of Israel did all that the Lord had instructed Moses.
32 Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
And they offered the tabernacle, and the covering, and all of the articles: the rings, the panels, the bars, the columns and bases,
33 Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
the cover of the skins of rams, dyed red, and the other cover of violet skins,
34 kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
the veil, the ark, the bars, the propitiatory,
35 Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
the table, with its vessels and the bread of the presence,
36 meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
the lampstand, the lamps, and their utensils with the oil,
37 kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
the altar of gold, and the ointment, and the incense of aromatics,
38 madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
and the tent at the entrance of the tabernacle,
39 madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
the altar of brass, the grating, the bars, and all of its vessels, the washtub with its base, the hangings of the atrium, and the columns with their bases,
40 mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
the hanging at the entrance of the atrium, and their little cords and pegs. Nothing was lacking of the articles that were commanded to be made for the ministry of the tabernacle and for the covering of the covenant.
41 na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
Likewise, the vestments, which the priests, namely, Aaron and his sons, make use of use in the Sanctuary,
42 Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
the sons of Israel offered, just as the Lord had instructed.
43 Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.
After this, when Moses saw that everything was completed, he blessed them.

< Kutoka 39 >