< Kutoka 38 >

1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
Zrobił również ołtarz do całopalenia z drewna akacjowego, na pięć łokci długi i na pięć łokci szeroki, kwadratowy, na trzy łokcie wysoki.
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
I zrobił rogi na jego czterech narożnikach, rogi wychodziły z niego. I pokrył go miedzią.
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
Zrobił też wszystkie naczynia do ołtarza, kociołki, szufle, miednice, widełki i łopaty [na rozżarzone węgle]. Wszystkie naczynia do niego zrobił z miedzi.
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
Zrobił także do ołtarza miedzianą kratę na kształt sieci pod obramowaniem, od spodu aż do połowy wysokości.
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
I odlał cztery pierścienie na czterech rogach miedzianej kraty jako uchwyty na drążki.
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
Porobił również drążki z drewna akacjowego i pokrył je miedzią.
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
I włożył drążki w te pierścienie po obu bokach ołtarza, aby był na nich noszony; zrobił go z desek, [wewnątrz był] pusty.
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
Zrobił też kadź z miedzi i do niej miedzianą podstawę ze zwierciadeł [kobiet], które gromadnie przychodziły przed wejście do Namiotu Zgromadzenia.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
Zrobił także dziedziniec: na południu po prawej stronie zasłony dziedzińca [były] ze skręconego bisioru, na sto łokci;
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Do nich dwadzieścia słupów, a do nich dwadzieścia miedzianych podstawek; haki na słupach i ich klamry ze srebra.
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Także po stronie północnej [zasłony] na sto łokci; do nich dwadzieścia słupów i do nich dwadzieścia miedzianych podstawek; haki na słupach i ich klamry ze srebra.
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
A od zachodniej strony [były] zasłony na pięćdziesiąt łokci; do nich dziesięć słupów i do nich dziesięć podstawek; haki na słupach i ich klamry ze srebra.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
A z przodu po stronie wschodniej były [zasłony] na pięćdziesiąt łokci.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Zasłony na piętnaście łokci [były] po [jednej] stronie, do nich trzy słupy i trzy podstawki.
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
I po drugiej stronie bramy dziedzińca, z jednej i z drugiej strony, piętnaście łokci zasłon, do nich trzy słupy i trzy podstawki.
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
Wszystkie zasłony dziedzińca wokoło [były] ze skręconego bisioru;
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
A podstawki słupów z miedzi, haki na słupach i klamry ze srebra, także pokrycia ich głowic ze srebra; wszystkie słupy dziedzińca były oklamrowane srebrem.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
Zasłona do bramy dziedzińca [była] haftowana, z błękitnej [tkaniny], purpury, karmazynu i skręconego bisioru; długa na dwadzieścia łokci, wysoka na pięć łokci jak inne zasłony dziedzińca.
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
A do nich cztery słupy i cztery miedziane podstawki; haki do nich [były] ze srebra, pokrycia ich głowic i klamry też były ze srebra.
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
Wszystkie kołki przybytku i dziedzińca wokoło [były] z miedzi.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
Oto obliczenie rzeczy do przybytku, [do] Przybytku Świadectwa, które zostały obliczone na rozkaz Mojżesza przez Itamara, syna kapłana Aarona, do służby Lewitów.
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
A Besalel, syn Uriego, syna Chura, z pokolenia Judy, zrobił wszystko, co PAN rozkazał Mojżeszowi;
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
A z nim Oholiab, syn Achisamaka, z pokolenia Dana, rytownik, wybitny rzemieślnik i haftujący na błękitnej [tkaninie], na purpurze, na karmazynie i na bisiorze.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Całego złota zużytego na wykonanie wszelkich robót świątyni – złota z darów – [było] dwadzieścia dziewięć talentów i siedemset trzydzieści syklów według sykla świątynnego.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Srebra zaś od przeliczonych spośród zgromadzenia [było] sto talentów i tysiąc siedemset siedemdziesiąt pięć syklów według sykla świątynnego.
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
Od każdej głowy pół sykla według sykla świątynnego, od wszystkich, którzy zostali policzeni, od dwudziestu lat i wyżej, a [ludzi tych] było sześćset trzy tysiące pięciuset pięćdziesięciu.
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
A było sto talentów srebra do odlewania podstawek świątyni i podstawek zasłony; sto podstawek ze stu talentów; talent na podstawkę.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
A z tysiąca siedmiuset siedemdziesięciu pięciu [syklów] zrobił haki na słupy i pokrył ich głowice, i oklamrował je.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
Miedzi zaś złożonej w ofierze [było] siedemdziesiąt talentów i dwa tysiące czterysta syklów.
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
I odlał z niej podstawki do wejścia do Namiotu Zgromadzenia i miedziany ołtarz, i do niego miedzianą kratę oraz wszystkie naczynia [do] ołtarza.
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
I podstawki do dziedzińca wokoło, podstawki do bramy dziedzińca, wszystkie kołki przybytku oraz kołki dziedzińca wokoło.

< Kutoka 38 >