< Kutoka 38 >

1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
He made also the auter of brent sacrifice of the trees of Sechym, of fyue cubitis bi square, and of thre cubitis in heiythe;
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
whose hornes camen forth of the corneris, and he hilide it with platis of bras.
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
And in to vsis therof he made redi of bras dyuerse vessels, caudruns, tongis, fleischhokis, hokis, and `resseittis of firis.
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
He made also the brasun gridile therof, `bi the maner of a net, and a `panne for colis vndur it, in the myddis of the auter.
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
And he yetide foure ryngis, by so many endis of the gridile, to putte in the barris to bere;
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
and he made tho same barris of the trees of Sechym, and hilide with platis of bras.
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
And ledde in to the serclis that stonden forth in the sidis of the auter. Forsothe thilke auter was not sad, but holowe of the bildyngis of tablis, and voide with ynne.
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
He made also a `greet waischyng vessel of bras, with his foundement, of the myrours of wymmen that wakiden in the `greet street of the tabernacle.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
And he made the greet street, in whose south coost weren tentis of bijs foldid ayen, of an hundrid cubitis, twenti brasun pilers with her foundementis,
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
the heedis of pilers, and al the grauyng of the werk, weren of siluer;
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
euenli at the north coost the tentis, pilers, and foundementis and heedis of pilers, weren of the same mesure, and werk, and metal.
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Forsothe in that coost that biholdith the west weren tentis of fyfty cubitis, ten brasun pilers with her foundementis, and the `heedis of pilers, and al the grauyng of werk, weren of siluer.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
Sotheli ayens the eest he made redi tentis of fifti cubitis,
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
of whiche tentis o side helde fiftene cubitis of thre pilers with her foundementis; and in the tother side,
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
for he made the entryng of the tabernacle bitwixe euer either, weren tentis euenli of fiftene cubitis, thre pilers, and so many foundementis.
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
Bijs foldid ayen hilide alle the tentis of the greet street.
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
The foundementis of pilers weren of bras; forsothe the heedis of tho pilers, with alle her grauyngis, weren of siluer; but also he clothide with siluer tho pilers of the greet street.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
And in the entryng therof he made a tente, bi `werk of broiderie, of iacynt, purpur, vermyloun, and of bijs foldid ayen, which tente hadde twenti cubitis in lengthe, and the heiythe was of fyue cubitis, bi the mesure which alle the tentis of the greet street hadden.
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
Forsothe the pylers in the entryng weren foure, with brasun foundementis, and the heedis of tho pilers and grauyngis weren of siluer;
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
and he made brasun stakis of the tabernacle, and of the greet street, bi cumpas.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
These ben the instrumentis of the tabernacle of witnessyng, that ben noumbrid, bi the comaundement of Moises, in the cerymonyes of Leuytis, bi the hond of Ithamar, sone of Aaron, preest.
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
Whiche instrumentis Beseleel, sone of Huri, sone of Hur, of the lynage of Juda, fillide; for the Lord comaundide bi Moises,
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
while Ooliab, sone of Achysameth, of the lynage of Dan, was ioyned felowe to hym, and he hym silf was a noble crafti man of trees, and a tapesere and a broderere of iacynt, purpur, vermyloun and bijs.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Al the gold that was spendid in the werk of seyntuarie, and that was offrid in yiftis, was of `nyne and twenti talentis, and of seuene hundrid and thretti siclis, at the mesure of seyntuarie.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Forsothe it was offrid of hem that passiden to noumbre fro twenti yeer and aboue, of sixe hundrid and thre thousand, and fyue hundrid and fifty of armed men.
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
Ferthermore, an hundrid talentis of siluer weren, of whiche the foundementis of the seyntuarie weren yotun togidere, and of the entryng, where the veil hangith;
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
an hundrid foundementis weren maad of an hundrid talentis, and for ech foundement was ordeyned o talent.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
Forsothe of a thousynde seuene hundrid and `thre scoor and fiftene siclis he made the heedis of pilers, and he `clothide tho same pilers with siluer.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
Also of bras weren offrid `thre scoor and twelue thousynde talentis, and foure hundrid siclis ouer.
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
Of whiche the foundementis in the entryng of the tabernacle of witnessyng weren yotun, and the brasun auter, with his gridele, and al the vessels that perteynen to the vss therof,
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
and the foundementis of the greet street, as wel in the cumpas, as in the entryng therof, and the stakis of the tabernacle, and of the greet street bi cumpas.

< Kutoka 38 >