< Kutoka 38 >

1 Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu; nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano
He also made the altar of holocaust from setim wood: five cubits square, and three in height,
2 Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba.
the horns of which proceeded from the corners. And he covered it with layers of brass.
3 Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto.
And for its uses, he prepared diverse vessels out of brass: kettles, forceps, little hooks, larger hooks, and receptacles for the fire.
4 Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
And he made its grating of brass, in the manner of a net, and under it, in the midst of the altar, its base,
5 Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba.
casting four rings at the four ends of the net in order to set the bars, so as to carry it.
6 Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba.
These bars he also made of setim wood, and he covered them with layers of brass.
7 Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.
And he drew them through the rings, which projected from the sides of the altar. But the altar itself was not solid, but hollow, made from panels and empty inside.
8 Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.
He also made the washtub of brass, with its base made from the mirrors of the women who kept watch at the door of the tabernacle.
9 Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
He also made the atrium, at the south side of which were hangings of fine twisted linen of one hundred cubits and
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
twenty columns of brass with their bases. The heads of the columns and all of the engraving work were of silver.
11 Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Equally, at the northern area, the hangings, the columns, and the bases and heads of the columns were of the same measure and work and metal.
12 Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Yet truly, on that side which looks out toward the west, there were hangings of fifty cubits, and ten columns with their bases of brass. And the heads of the columns and all of the engraving work were of silver.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini.
Furthermore, toward the east, he prepared hangings of fifty cubits:
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
of which, there were fifteen cubits, among three columns with their bases, holding up one side,
15 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
and on the other side, (for between the two he made the entrance of the tabernacle) there were equally hangings of fifteen cubits, and three pillars, and the same number of bases.
16 Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri.
All the hangings of the atrium were woven from fine twisted linen.
17 Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.
The bases of the columns were of brass, but their heads with all of their engravings were of silver. Now he also overlaid the columns of the atrium themselves with silver.
18 Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano,
And he made, at its entrance, a hanging, wrought with embroidery, of hyacinth, purple, vermillion, and fine twisted linen, which held twenty cubits in length, yet truly it was five cubits in height, as with the measure of all the hangings of the atrium.
19 likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha.
Now the columns at the entrance were four, with bases of brass, and their heads and engravings were of silver.
20 Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.
Likewise, the tent pegs of the tabernacle and the atrium all around he made of brass.
21 Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni.
These are the instruments of the tabernacle of the testimony, which were enumerated according to the instruction of Moses, with the ceremonies of the Levites, by the hand of Ithamar, the son of Aaron the priest,
22 (Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose,
which Bezalel, the son of Uri, the son of Hur from the tribe of Judah, had completed, just as the Lord decreed through Moses.
23 akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.)
He was joined by his associate, Oholiab, the son of Ahisamach, from the tribe of Dan, who himself was also an exceptional artisan of wood, and of weaving, as well as of embroidery, with hyacinth, purple, vermillion, and fine linen.
24 Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
All of the gold that was expended in the work of the Sanctuary, and that was offered in donation, was twenty-nine talents and seven hundred thirty shekels, according to the measure of the Sanctuary.
25 Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Now it was offered by those who were past the numbering of twenty years and above: from six hundred and three thousand, five hundred and fifty men able to bear arms.
26 Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550.
There were, beyond that, one hundred talents of silver, from which were cast the bases for the Sanctuary and for the entrance where the veil hangs.
27 Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako.
One hundred bases were made from one hundred talents, a single talent being counted for each base.
28 Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.
But from one thousand seven hundred and seventy-five, he made the heads of the columns, which he also clothed with silver.
29 Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.
Likewise, of brass, there was offered seventy-two thousand talents, and four hundred more shekels,
30 Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote,
from which were cast the bases at the entrance of the tabernacle of the testimony, and the altar of brass with its grating, and the vessels which pertain to its use,
31 vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.
and the bases of the atrium, as much at the circumference as at its entrance, and the tent pegs of the tabernacle and of the atrium all round.

< Kutoka 38 >