< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
Or Béséléel fit aussi l’arche de bois de sétim, ayant deux coudées et demie en longueur, et une coudée et demie en largeur; la hauteur aussi était d’une coudée et demie; et il la revêtit d’un or très pur au dedans et au dehors.
2 Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
Et il y fit une couronne d’or tout autour,
3 Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Jetant en fonte quatre anneaux d’or pour les quatre coins de l’arche, deux à un côté et deux à l’autre.
4 Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Il fit aussi des leviers de bois de sétim, qu’il revêtit d’or,
5 Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Et qu’il passa dans les anneaux qui étaient aux côtés de l’arche pour la porter.
6 Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
Il fit encore un propitiatoire, c’est-à-dire un oracle, d’or très pur, de deux coudées et demie en longueur, et d’une coudée et demie en largeur;
7 Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Et aussi deux chérubins d’un or ductile, qu’il posa des deux côtés du propitiatoire:
8 Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Un chérubin à la sommité d’un côté, et l’autre chérubin à la sommité de l’autre côté: chacun des deux chérubins à chacune des sommités du propitiatoire,
9 Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
Etendant leurs ailes et couvrant le propitiatoire, et se regardant l’un l’autre, et le propitiatoire.
10 Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Il fit de plus la table de bois de sétim, qui avait en longueur deux coudées, en largeur une coudée, et en hauteur une coudée et demie.
11 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Et il la revêtit d’un or très pur, et il y fit une bordure d’or tout autour;
12 Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Et à la bordure elle-même, une couronne d’or de sculpture à jour de quatre doigts, et audessus de celle-ci une autre couronne d’or.
13 Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Il fondit aussi quatre anneaux d’or qu’il posa aux quatre côtés, un à chaque pied de la table,
14 Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
Contre la couronne; et il y passa les leviers, afin que la table pût être portée.
15 Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
Il fit aussi les leviers eux-mêmes de bois de sétim, et il les revêtit d’or;
16 Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
Et de plus les vases d’un or pur pour les divers usages de la table, les plats, les patères, les encensoirs et les tasses dans lesquelles doivent être offertes les libations.
17 Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
Il fit encore le chandelier ductile d’un or très pur. De sa tige sortaient les branches, les coupes, les pommes et les lis:
18 Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches sortaient aux deux côtés, trois d’un côté, et trois de l’autre.
19 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Il y avait trois coupes en forme de noix à une branche, ainsi que des pommes et des lis, et trois coupes en forme de noix à une autre branche, ainsi que des pommes et des lis. C’était le même travail pour les six branches qui sortaient de la tige du chandelier.
20 Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
Mais à la tige elle-même étaient quatre coupes en forme de noix, et des pommes à chacune, ainsi que des lis,
21 Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
Et des pommes en trois endroits sous les deux branches, qui font ensemble six branches sortant d’une seule tige.
22 Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
Ainsi, et les pommes et les branches sortaient du chandelier lui-même, toutes ductiles d’un or très pur.
23 Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
Il fit aussi d’un or très pur les sept lampes, avec leurs mouchettes, et les vases où doivent s’éteindre les lumignons,
24 Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
Le chandelier avec tous ses vases pesait un talent d’or.
25 Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
Il fit encore l’autel du parfum à brûler de bois de sétim, lequel avait en carré une coudée, et en hauteur deux: de ses angles sortaient les cornes.
26 Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
Et il le revêtit d’un or très pur, avec la grille, les parois et les cornes.
27 Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
Et il y fit une couronne tout autour, et deux anneaux dor sous la couronne à chaque côté, pour qu’on y passât des leviers, et que l’autel pût être porté.
28 Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Mais les leviers eux-mêmes, il les fit de bois de sétim, et les couvrit de lames d’or.
29 Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.
Il composa aussi l’huile pour les onctions de consécration et le parfum à brûler, composé d’aromates très purs, selon l’art d’un parfumeur.

< Kutoka 37 >