< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
Beçalel exécuta l’arche en bois de chittîm. Elle avait deux coudées et demie de long, une coudée et demie de large, une coudée et demie de haut.
2 Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
Il la revêtit d’or pur, par dedans et par dehors et il l’entoura d’une corniche en or.
3 Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Il moula quatre anneaux d’or pour ses quatre angles; savoir, deux anneaux pour l’une de ses faces, deux anneaux pour la face opposée.
4 Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Il fit des barres en bois de chittîm et les recouvrit d’or.
5 Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Il introduisit ces barres dans les anneaux, aux côtés de l’arche, pour qu’on pût la transporter.
6 Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
Il confectionna un propitiatoire d’or pur, ayant deux coudées et demie de longueur, une coudée et demie de largeur.
7 Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Il fabriqua deux chérubins d’or, qu’il fit d’une seule pièce, ressortant des deux bouts du propitiatoire.
8 Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Un chérubin à l’un des bouts, un chérubin au bout opposé; c’est du propitiatoire même qu’il-fit saillir ces chérubins, à ses deux extrémités.
9 Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
Les chérubins, dont les ailes étaient déployées en avant, dominaient de leurs ailes le propitiatoire; et leurs visages, tournés l’un vers l’autre, s’inclinaient vers le propitiatoire.
10 Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Puis il fit la table en bois de chittîm; deux coudées formaient sa longueur, une coudée sa largeur, une coudée et demie sa hauteur.
11 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
II la revêtit d’or pur et il l’entoura d’une bordure d’or.
12 Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Il y ajusta, à l’entour, un châssis large d’un palme qu’il entoura d’une bordure d’or.
13 Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Il moula pour cette table quatre anneaux d’or et fixa ces anneaux aux quatre extrémités formées par les quatre pieds.
14 Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
C’Est en regard du châssis que se trouvaient ces anneaux, où devaient passer les barres destinées à porter la table.
15 Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
Il fit ces barres de bois de chittîm et les recouvrit d’or; elles servirent à porter la table.
16 Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
Il confectionna encore les ustensiles relatifs à la table: ses sébiles, ses cuillers et ses demi-tubes, ainsi que les montants dont elle devait être garnie; le tout en or pur.
17 Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
II exécuta le candélabre en or pur. Il le fit tout d’une pièce, avec sa base et son fût; ses calices, ses boutons et ses fleurs faisaient corps avec lui.
18 Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches sortaient de ses côtés: trois branches d’un côté, trois branches du côté opposé.
19 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Trois calices amygdaloïdes à l’une des branches, avec bouton et fleur et trois calices amygdaloïdes à une autre branche, avec bouton et fleur; même disposition pour les six branches qui partaient du candélabre.
20 Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
Le fût du candélabre même portait quatre calices amygdaloïdes, avec ses boutons et ses fleurs,
21 Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
savoir, un bouton à l’origine d’une de ses paires de branches, un bouton à l’origine de la seconde paire de branches, un bouton à l’origine de la troisième paire: ainsi, pour les six branches qui en ressortaient."
22 Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
Boutons et branches faisaient corps avec lui: il formait tout entier une seule masse d’or pur.
23 Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
Il en fabriqua aussi les lampes au nombre de sept, puis les mouchettes et les godets, le tout en or pur.
24 Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
Il employa un kikkar d’or pur à le confectionner avec tous ses accessoires.
25 Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
Il construisit l’autel du parfum en bois de chittîm, long d’une coudée, large d’une coudée, conséquemment carré, et haut de deux coudées; ses cornes faisaient corps avec lui.
26 Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
Il le revêtit d’or pur, sa plate-forme, ses parois tout autour et ses cornes et il l’entoura d’un bordure d’or.
27 Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
Il y adapta deux anneaux d’or au-dessous de la bordure, à ses deux parois, de part et d’autre, pour recevoir des barres destinées à le porter.
28 Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Il fit ces barres de bois de chittîm et les recouvrit d’or.
29 Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.
II composa aussi l’huile d’onction sainte et le parfum aromatique pur, selon l’art du parfumeur.

< Kutoka 37 >