< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
Béseléel fit l’arche de bois d’acacia; sa longueur était de deux coudées et demie, sa largeur d’une coudée et demie, et sa hauteur d’une coudée et demie.
2 Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
Il la revêtit d’or pur, en dedans et en dehors, et il y fit une guirlande d’or tout autour.
3 Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Il fondit pour elle quatre anneaux d’or, qu’il mit à ses quatre pieds, deux anneaux d’un côté et deux anneaux de l’autre.
4 Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Il fit des barres de bois d’acacia et les revêtit d’or.
5 Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Il passa les barres dans les anneaux sur les côtés de l’arche, pour la porter.
6 Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
Il fit un propitiatoire d’or pur; sa longueur était de deux coudées et demie, sa largeur d’une coudée et demie.
7 Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Il fit deux chérubins d’or; il les fit d’or battu, aux deux extrémités du propitiatoire,
8 Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
un chérubin à l’une des extrémités et un chérubin à l’autre extrémité; il fit les chérubins sortant du propitiatoire à ses deux extrémités.
9 Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
Les chérubins avaient leurs ailes déployées vers le haut, couvrant de leurs ailes le propitiatoire, et se faisant face l’un à l’autre; les faces des chérubins étaient tournées vers le propitiatoire.
10 Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Il fit la table de bois d’acacia; sa longueur était de deux coudées, sa largeur d’une coudée, et sa hauteur d’une coudée et demie.
11 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Il la revêtit d’or pur, et y mit une guirlande d’or tout autour.
12 Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Il lui fit à l’entour un châssis d’une palme, et il fit une guirlande d’or au châssis tout autour.
13 Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Il fondit pour la table quatre anneaux d’or, et il mit les anneaux aux quatre coins, qui sont à ses quatre pieds.
14 Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
Les anneaux étaient près du châssis pour recevoir les barres qui doivent porter la table.
15 Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
Il fit les barres de bois d’acacia et les revêtit d’or; elles servaient à porter la table.
16 Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
Il fit les ustensiles qu’on devait mettre sur la table, ses plats, ses cassolettes, ses coupes et ses tasses pour servir aux libations; il les fit d’or pur.
17 Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
Il fit le chandelier d’or pur; il fit d’or battu le chandelier, avec son pied et sa tige; ses calices, ses boutons et ses fleurs étaient d’une même pièce.
18 Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches sortaient de ses côtés; trois branches du chandelier de l’un de ses côtés, et trois branches du chandelier du second de ses côtés.
19 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Il y avait sur la première branche trois calices en fleurs d’amandier, bouton et fleur, et sur la seconde branche trois calices en fleurs d’amandiers, bouton et fleur; il en était de même pour les six branches partant du chandelier.
20 Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
A la tige du chandelier, il y avait quatre calices, en fleurs d’amandier, avec leurs boutons et leurs fleurs.
21 Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
Il y avait un bouton sous les deux premières branches partant de la tige du chandelier, un bouton sous les deux branches suivantes partant de la tige du chandelier, et un bouton sous les deux dernières branches partant de la tige du chandelier, selon les six branches sortant du chandelier.
22 Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
Ces boutons et ces branches étaient d’une même pièce avec le chandelier; le tout était une masse d’or battu, d’or pur.
23 Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
Il fit ses lampes au nombre de sept, ses mouchettes et ses vases à cendre, en or pur.
24 Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
On employa un talent d’or pur pour faire le chandelier avec tous ses ustensiles.
25 Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
Il fit l’autel des parfums de bois d’acacia; sa longueur était d’une coudée, et sa largeur d’une coudée; il était carré, et sa hauteur était de deux coudées; ses cornes faisaient corps avec lui.
26 Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
Il le revêtit d’or pur, le dessus, les côtés tout autour et les cornes, et il y fit une guirlande d’or tout autour.
27 Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
Il fit pour lui deux anneaux d’or, au-dessous de sa guirlande, sur ses deux arêtes; il les fit aux deux côtés, pour recevoir les barres qui servaient à le porter.
28 Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Il fit les barres de bois d’acacia et les revêtit d’or.
29 Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.
Il fit l’huile pour l’onction sainte, et le parfum pour l’encensement, composé selon l’art du parfumeur.

< Kutoka 37 >