< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
After this, Bezaleel made the Arke of Shittim wood, two cubites and an halfe long and a cubite and an halfe broade, and a cubite and an halfe hie:
2 Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
And ouerlayde it with fine golde within and without, and made a crowne of golde to it rounde about,
3 Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
And cast for it foure rings of golde for the foure corners of it: that is, two rings for the one side of it, and two rings for the other side thereof.
4 Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Also he made barres of Shittim wood, and couered them with golde,
5 Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
And put the barres in the rings by the sides of the Arke, to beare the Arke.
6 Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
And he made the Merciseate of pure golde: two cubites and an halfe was the length thereof, and one cubite and an halfe the breadth thereof.
7 Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
And he made two Cherubims of gold, vpon the two endes of the Merciseate: euen of worke beaten with the hammer made he them.
8 Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
One Cherub on the one ende, and another Cherub on the other ende: of the Merciseate made he the Cherubims, at ye two endes thereof.
9 Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
And the Cherubims spread out their wings on hie, and couered the Merciseat with their wings, and their faces were one towards another: towarde the Merciseat were the faces of the Cherubims.
10 Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Also he made ye Table of Shittim wood: two cubites was the length thereof, and a cubite the breadth thereof, and a cubite and an halfe the height of it.
11 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
And hee ouerlayde it with fine golde, and made thereto a crowne of golde round about.
12 Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Also he made thereto a border of an hand breadth round about, and made vpon the border a crowne of golde round about.
13 Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
And he cast for it foure rings of gold, and put the rings in the foure corners that were in the foure feete thereof.
14 Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
Against the border were the rings, as places for the barres to beare the Table.
15 Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
And he made the barres of Shittim wood, and couered them with golde to beare the Table.
16 Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
Also he made the instruments for the Table of pure golde: dishes for it, and incense cuppes for it, and goblets for it, and couerings for it, wherewith it should be couered.
17 Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
Likewise he made the Candlesticke of pure golde: of worke beaten out with the hammer made he the Candlesticke: and his shaft, and his branche, his bolles, his knops, and his floures were of one piece.
18 Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
And sixe branches came out of the sides thereof: three branches of the Candlesticke out of the one side of it, and three branches of the Candlesticke out of the other side of it.
19 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
In one branche three bolles made like almondes, a knop and a floure: and in another branch three bolles made like almondes, a knop and a floure: and so throughout the sixe branches that proceeded out of the Candlesticke.
20 Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
And vpon the Candlesticke were foure bolles after the facion of almondes, the knoppes thereof and the floures thereof:
21 Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
That is, vnder euery two branches a knop made thereof, and a knop vnder the second branch thereof, and a knop vnder the thirde branche thereof, according to the sixe branches comming out of it.
22 Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
Their knops and their branches were of the same: it was all one beaten worke of pure gold.
23 Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
And he made for it seuen lampes with the snuffers, and snufdishes thereof of pure golde.
24 Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
Of a talent of pure golde made he it with all the instruments thereof.
25 Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
Furthermore he made the perfume altar of Shittim wood: the length of it was a cubite, and the breadth of it a cubite (it was square) and two cubites hie, and the hornes thereof were of ye same.
26 Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
And he couered it with pure gold, both the top and the sides thereof rounde about, and the hornes of it, and made vnto it a crowne of golde round about.
27 Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
And he made two rings of gold for it, vnder the crowne thereof in the two corners of the two sides thereof, to put barres in for to beare it therewith.
28 Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Also he made the barres of Shittim wood, and ouerlayde them with golde.
29 Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.
And he made the holy anointing oyle, and the sweete pure incense after ye apothecaries arte.

< Kutoka 37 >