< Kutoka 36 >
1 Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
“Bezalel e Oholiab trabalharão com todo homem sábio, em quem Javé colocou sabedoria e compreensão para saber fazer todo o trabalho para o serviço do santuário, de acordo com tudo o que Javé ordenou”.
2 Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
Moisés chamou Bezalel e Oholiab, e todo homem sábio, em cujo coração Javé tinha colocado sabedoria, até mesmo todos cujo coração o agitava para vir ao trabalho para fazê-lo.
3 Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
Eles receberam de Moisés toda a oferta que os filhos de Israel haviam trazido para a obra do serviço do santuário, com a qual o faziam. Eles continuavam trazendo ofertas de livre vontade a ele todas as manhãs.
4 Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
Todos os sábios, que executaram todo o trabalho do santuário, cada um veio de seu trabalho que ele fez.
5 wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
Eles falaram com Moisés, dizendo: “O povo trouxe muito mais do que o suficiente para o serviço da obra que Javé mandou fazer”.
6 Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
Moisés deu um mandamento, e eles fizeram com que ele fosse proclamado em todo o campo, dizendo: “Que nem o homem nem a mulher façam outra coisa pela oferta para o santuário”. Assim, o povo foi impedido de trazer.
7 kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
Pelo material que tinham era suficiente para fazer todo o trabalho, e demais.
8 Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Todos os homens de coração sábio entre aqueles que fizeram o trabalho fizeram o tabernáculo com dez cortinas de linho fino torcido, azul, roxo e escarlate. Eles os fizeram com querubins, o trabalho de um artesão habilidoso.
9 Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
O comprimento de cada cortina era de vinte e oito cúbitos, e a largura de cada cortina de quatro cúbitos. Todas as cortinas tinham uma medida.
10 Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Ele acoplou cinco cortinas umas às outras, e as outras cinco cortinas ele acoplou umas às outras.
11 Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
Ele fez laçadas de azul na borda de uma cortina a partir da borda do acoplamento. Da mesma forma, ele fez na borda da cortina que estava mais externa no segundo acoplamento.
12 Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
Ele fez cinqüenta voltas na borda de uma cortina, e fez cinqüenta voltas na borda da cortina que estava no segundo acoplamento. As alças eram opostas umas às outras.
13 Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
Ele fez cinqüenta presilhas de ouro, e acoplou as cortinas umas às outras com as presilhas: assim, o tabernáculo era uma unidade.
14 Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Ele fez cortinas de cabelo de cabra para uma cobertura sobre o tabernáculo. Ele as fez onze cortinas.
15 Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
O comprimento de cada cortina era de trinta cúbitos, e quatro cúbitos a largura de cada cortina. As onze cortinas tinham uma medida.
16 Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
Ele acoplou cinco cortinas por si só, e seis cortinas por si só.
17 Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Ele fez cinqüenta laçadas na borda da cortina que estava mais externa no acoplamento, e fez cinqüenta laçadas na borda da cortina que estava mais externa no segundo acoplamento.
18 Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Ele fez cinqüenta presilhas de bronze para unir a tenda, para que ela pudesse ser uma unidade.
19 Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Ele fez uma cobertura para a tenda de peles de carneiros tingidas de vermelho, e uma cobertura de peles de vaca do mar acima.
20 Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Ele fez as tábuas para o tabernáculo de madeira de acácia, de pé.
21 Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
Dez côvados era o comprimento de uma tábua, e um côvado e meio da largura de cada tábua.
22 zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Cada tábua tinha duas tábua, unidas uma à outra. Ele fez todas as tábuas do tabernáculo desta maneira.
23 Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
Ele fez as tábuas para o tabernáculo, vinte tábuas para o lado sul.
24 na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
Ele fez quarenta bases de prata sob as vinte tábuas: duas bases sob uma tábua para seus dois encaixes, e duas bases sob outra tábua para seus dois encaixes.
25 Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
Para o segundo lado do tabernáculo, no lado norte, ele fez vinte tábuas
26 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
e suas quarenta bases de prata: duas bases debaixo de uma tábua, e duas bases debaixo de outra tábua.
27 Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Para a parte mais distante do tabernáculo, no lado oeste, ele fez seis tábuas.
28 na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
Ele fez duas tábuas para os cantos do tabernáculo, na parte mais distante.
29 Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
Estavam dobradas por baixo e, da mesma forma, estavam até o topo do tabernáculo com um anel. Ele fez isso com as duas nos dois cantos.
30 Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Havia oito placas e suas soquetes de prata, dezesseis soquetes - sob cada placa duas soquetes.
31 Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
Ele fez barras de madeira de acácia: cinco para as tábuas de um lado do tabernáculo,
32 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
e cinco barras para as tábuas do outro lado do tabernáculo, e cinco barras para as tábuas do tabernáculo para a parte de trás para o oeste.
33 Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
Ele fez a barra do meio para passar no meio das tábuas de uma extremidade à outra.
34 Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
Ele cobriu as tábuas com ouro, e fez seus anéis de ouro como lugares para as barras, e cobriu as barras com ouro.
35 Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Ele fez o véu de azul, roxo, escarlate, e linho fino torcido, com querubim. Ele fez dele o trabalho de um artesão habilidoso.
36 Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
Ele fez quatro pilares de acácia para ele, e os revestiu com ouro. Seus ganchos eram de ouro. Ele lançou quatro soquetes de prata para eles.
37 Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Ele fez uma tela para a porta da tenda, de azul, roxo, escarlate e linho fino torcido, obra de um bordador;
38 Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.
e os cinco pilares da mesma com seus ganchos. Ele cobriu suas capitéis e seus filetes com ouro, e suas cinco bases eram de bronze.