< Kutoka 36 >

1 Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
Béséléel donc et Ooliab et tous les hommes sages auxquels le Seigneur avait donné la sagesse et l’intelligence, pour qu’ils sussent exécuter habilement, firent ce qui était nécessaire aux usages du sanctuaire, et ce qu’avait ordonné le Seigneur.
2 Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
Car lorsque Moïse les eut appelés avec tous les hommes habiles auxquels le Seigneur avait donné la sagesse et qui de leur propre mouvement s’étaient offerts pour faire l’ouvrage,
3 Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
Il leur livra tous les dons des enfants d’Israël. Pendant qu’ils s’appliquaient avec ardeur à l’ouvrage, chaque jour au matin le peuple offrait des présents votifs.
4 Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
C’est pourquoi les ouvriers forcés de venir,
5 wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
Dirent à Moïse: Le peuple offre plus qu’il n’est nécessaire.
6 Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
Moïse commanda donc qu’il fût publié par la voix du hérault: Que ni homme ni femme n’offre plus rien pour l’ouvrage du sanctuaire. Et ainsi on cessa d’offrir des présents,
7 kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
Parce que ceux qui avaient été offerts suffisaient et surabondaient.
8 Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Et tous les sages de cœur pour accomplir l’ouvrage du tabernacle, dix rideaux de fin lin retors, d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte, d’un travail varié, et selon l’art de la tissure en diverses couleurs.
9 Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
Un des rideaux avait en longueur vingt-huit coudées, et en largeur quatre; il y avait une seule mesure pour tous les rideaux.
10 Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Il joignit cinq rideaux l’un à l’autre, et il attacha les cinq autres ensemble.
11 Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
il fit aussi des lacs d’hyacinthe au bord d’un rideau des deux côtés, et pareillement au bord d’un autre rideau,
12 Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
Afin que les lacs vinssent l’un contre l’autre, et qu’ils se joignissent ensemble.
13 Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
C’est pourquoi il fondit aussi cinquante anneaux d’or qui devaient attacher les lacs des rideaux, afin qu’il se fît un seul tabernacle.
14 Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Il fit encore onze couvertures de poils de chèvre pour couvrir le toit du tabernacle.
15 Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
Une couverture avait en longueur trente coudées, et en largeur, quatre coudées: toutes les couvertures étaient d’une seule mesure.
16 Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
Il en joignit cinq à part et les six autres séparément;
17 Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Et il fit cinquante lacs au bord d’une couverture et cinquante au bord d’une autre couverture, afin qu’elles fussent jointes ensemble;
18 Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Et de plus cinquante boucles d’airain par lesquelles devait être attaché le toit, afin que de toutes les couvertures, il se fît une seule couverture.
19 Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Il fit encore une couverture du tabernacle, de peaux de béliers, teintes en rouge, et par-dessus une autre couverture de peaux violettes.
20 Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Il fit aussi de bois de sétim les ais du tabernacle, qui se tenaient debout.
21 Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
La longueur d’un ais était de dix coudées; et la largeur tenait une coudée et demie,
22 zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Il y avait deux emboîtements à chaque ais, afin que l’un fût joint à l’autre. Ainsi fit-il pour tous les ais du tabernacle.
23 Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
De ces ais vingt étaient du côté méridional contre le vent du midi,
24 na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
Avec quarante soubassements d’argent. Deux soubassements étaient posés sous un seul ais des deux côtés des angles, où l’emboîtement des côtés se termine dans les angles.
25 Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
Et aussi pour le côté du tabernacle, qui regarde l’aquilon, il fit vingt ais,
26 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Avec quarante soubassements d’argent, deux soubassements pour chaque ais,
27 Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Mais contre l’occident, c’est-à-dire, vers cette partie du tabernacle qui regarde la mer, il fit six ais,
28 na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
Et deux autres à chaque angle du tabernacle, par derrière;
29 Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
Lesquels étaient joints depuis le bas jusqu’au haut, et formaient un seul assemblage. Ainsi fit-il des deux côtés pour chaque angle;
30 Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
De manière à ce que huit ais fussent ensemble, et qu’ils eussent seize soubassements d’argent; c’est-à-dire, deux soubassements sous chaque ais.
31 Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
Il fit encore des leviers de bois de sétim, cinq pour maintenir les ais d’un côté du tabernacle,
32 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
Et cinq autres pour assujettir les ais de l’autre côté; et outre ceux-là, cinq autres leviers au côté occidental du tabernacle contre la mer.
33 Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
Il fit aussi un autre levier qui passait par le milieu des ais depuis un angle jusqu’à l’autre angle.
34 Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
Mais les cloisons elles-mêmes des ais, il les dora, leurs soubassements d’argent ayant été fondus. Et il fit leurs cercles d’or, par lesquels les leviers pussent passer, et qu’il couvrit aussi de lames d’or.
35 Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Il fit de plus le voile d’hyacinthe et de pourpre, d’écarlate et de fin Un retors, d’un ouvrage de tisseur en diverses couleurs, varié et parsemé,
36 Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
Et quatre colonnes de bois de sétim, lesquelles il dora avec leurs chapiteaux, leurs soubassements d’argent ayant été fondus.
37 Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Il fit encore à l’entrée du tabernacle un voile d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate, de fin lin retors, en ouvrage de brodeur,
38 Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.
Et cinq colonnes avec leurs chapiteaux, lesquelles il couvrit d’or, et il fondit leurs bases d’airain.

< Kutoka 36 >