< Kutoka 36 >

1 Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
Béseléel, Ooliab et tous les hommes intelligents en qui Yahweh a mis de l'intelligence et de l'habileté pour savoir faire tous les ouvrages destinés au service du sanctuaire, les exécuteront selon tout ce que Yahweh a commandé. "
2 Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
Moïse appela Béseléel, Ooliab et tous les hommes intelligents dans le cœur desquels Yahweh avait mis de l'intelligence, tous ceux que leur cœur poussait à s'appliquer à cette œuvre pour l'exécuter.
3 Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
Ils prirent de devant Moïse toute l'offrande qu'avaient apportée les enfants d'Israël pour exécuter les ouvrages destinés au service du sanctuaire; et chaque matin le peuple continuait à apporter à Moïse des offrandes volontaires.
4 Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
Alors tous les hommes habiles qui exécutaient tous les ouvrages du sanctuaire, quittant chacun l'ouvrage qu'ils faisaient,
5 wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
vinrent dire à Moïse: " Le peuple apporte beaucoup plus qu'il ne faut pour l'exécution des ouvrages que Yahweh a ordonné de faire. "
6 Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
Moïse donna un ordre et on fit cette proclamation dans le camp: " Que personne, homme ou femme, ne s'occupe plus de l'offrande pour le sanctuaire ". Et on empêcha le peuple d'en apporter davantage.
7 kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
Les objets préparés suffisaient, et au delà, pour tous les ouvrages à exécuter.
8 Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Tous les hommes habiles parmi ceux qui travaillaient à l'œuvre firent la Demeure de dix tentures; ils les firent de lin retors, de pourpre violette, de pourpre écarlate et de cramoisi, avec des chérubins, ouvrage d'habile tisseur.
9 Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
La longueur d'une tenture était de vingt-huit coudées, et la largeur d'une tenture était de quatre coudées; la dimension était la même pour toutes les tentures.
10 Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Cinq de ces tentures furent jointes ensemble; les cinq autres furent aussi jointes ensemble.
11 Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
On mit des lacets de pourpre violette au bord de la tenture terminant le premier assemblage; on fit de même au bord de la tenture terminant le second assemblage.
12 Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
On fit cinquante lacets à la première tenture, et on fit cinquante lacets au bord de la tenture terminant le second assemblage, et ces lacets se correspondaient les uns aux autres.
13 Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
On fit cinquante agrafes d'or, avec lesquelles on joignit les tentures l'une à l'autre, en sorte que la Demeure forma un seul tout.
14 Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
On fit des tentures de poil de chèvre pour former une tente sur la Demeure; on fit onze de ces tentures.
15 Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
La longueur d'une tenture était de trente coudées, et la largeur d'une tenture de quatre coudées; La dimension était la même pour les onze tentures.
16 Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
On joignit à part cinq de ces tentures et les six autres à part.
17 Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
On mit cinquante lacets au bord de la tenture terminant un assemblage, et on mit cinquante lacets au bord de la tenture du second assemblage.
18 Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
On fit cinquante agrafes d'airain pour assembler la tente, afin qu'elle format un seul tout.
19 Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
On fit pour la tente une couverture en peaux de béliers teintes en rouge, et une couverture en peaux de veaux marins, par dessus.
20 Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
On fit aussi les planches pour la Demeure, des planches de bois d'acacia, posées debout.
21 Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
La longueur d'une planche était de dix coudées, et la largeur d'une planche était d'une coudée et demie.
22 zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Il y avait à chaque planche deux tenons, joints l'un à l'autre: on fit de même pour toutes les planches de la Demeure.
23 Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
On fit les planches pour la Demeure: vingt planches pour la face du midi, à droite.
24 na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
On mit sous les vingt planches quarante socles d'argent, deux socles sous chaque planche pour ses deux tenons.
25 Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
Pour le second côté de la Demeure, le côté du nord, on fit vingt planches,
26 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
ainsi que leurs quarante socles d'argent, deux socles sous chaque planche.
27 Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
On fit six planches pour le fond de la Demeure, du côté de l'occident.
28 na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
On fit deux planches pour les angles de la Demeure, dans le fond;
29 Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
elles étaient doubles depuis le bas, formant ensemble un seul tout jusqu'à leur sommet, jusqu'au premier anneau: ainsi fit-on pour toutes les deux, aux deux angles.
30 Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Il y avait ainsi huit planches, avec leurs socles d'argent, seize socles, deux socles sous chaque planche.
31 Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
On fit des traverses de bois d'acacia, cinq pour les planches de l'un des côtés de la Demeure,
32 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
cinq traverses pour les planches du second côté de la Demeure, et cinq traverses pour les planches du côté de la Demeure qui en forme le fond, vers l'occident.
33 Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
La traverse du milieu s'étendait, le long des planches, d'une extrémité à l'autre.
34 Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
On revêtit d'or les planches, et l'on fit d'or leurs anneaux qui recevaient les traverses, et l'on revêtit d'or les traverses.
35 Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
On fit le voile de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi, et de lin retors; on y représenta des chérubins figurés: ouvrage d'un habile tisseur.
36 Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
On fit pour lui quatre colonnes d'acacia, revêtues d'or, avec des crochets d'or; et l'on fondit pour elles quatre socles d'argent.
37 Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
On fit pour l'entrée de la tente un rideau en pourpre violette, pourpre écarlate, cramoisi et lin retors, ouvrage d'un dessin varié.
38 Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.
On fit pour ce rideau cinq colonnes et leurs crochets et l'on revêtit d'or leurs chapiteaux et leurs tringles; leurs cinq socles étaient d'airain.

< Kutoka 36 >