< Kutoka 36 >

1 Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
And Bezaleel, and Aholiab, and every wise-hearted man, in whom YHWH has given wisdom and understanding to know to do every work of the service of the holy place, have done according to all that YHWH commanded.
2 Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
And Moses calls to Bezaleel, and to Aholiab, and to every wise-hearted man in whose heart YHWH has given wisdom, everyone whom his heart lifted up, to come near to the work to do it.
3 Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
And they take from before Moses all the raised-offering which the sons of Israel have brought in for the work of the service of the holy place to do it; and still they have brought to him a willing-offering morning by morning.
4 Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
And all the wise men, who are doing all the work of the holy place, each come from his work which they are doing,
5 wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
and speak to Moses, saying, “The people are multiplying to bring in more than sufficient for the service of the work which YHWH commanded [us] to do.”
6 Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
And Moses commands, and they cause a voice to pass over through the camp, saying, “Do not let man or woman make anymore work for the raised-offering of the holy place”; and the people are restrained from bringing,
7 kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
and the work has been sufficient for them, for all the work, to do it, and to leave.
8 Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
And all the wise-hearted ones among the doers of the work make the Dwelling Place; he has made them [with] ten curtains of twined linen, and blue, and purple, and scarlet, [with] cherubim, the work of a designer.
9 Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
The length of one curtain [is] twenty-eight by the cubit, and the breadth of one curtain [is] four by the cubit; one measure [is] for all the curtains.
10 Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
And he joins the five curtains to one another, and the [other] five curtains he has joined to one another;
11 Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
and he makes loops of blue on the edge of one curtain, at the end, in the joining; so he has made in the edge of the outmost curtain, in the joining of the second;
12 Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
he has made fifty loops in the first curtain, and he has made fifty loops in the end of the curtain which [is] in the joining of the second; the loops are taking hold on one another.
13 Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
And he makes fifty hooks of gold, and joins the curtains to one another by the hooks, and the Dwelling Place is one.
14 Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
And he makes curtains of goats’ [hair] for a tent over the Dwelling Place; eleven curtains he has made them;
15 Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
the length of one curtain [is] thirty by the cubit, and the breadth of one curtain [is] four cubits; one measure [is] for the eleven curtains;
16 Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
and he joins the five curtains apart, and the six curtains apart.
17 Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
And he makes fifty loops on the outer edge of the curtain, in the joining; and he has made fifty loops on the edge of the curtain which is joining the second;
18 Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
and he makes fifty hooks of bronze to join the tent—to be one;
19 Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
and he makes a covering for the tent of rams’ skins made red, and a covering of tachashim skins above.
20 Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
And he makes the boards for the Dwelling Place of shittim wood, standing up;
21 Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
ten cubits [is] the length of the [one] board, and a cubit and a half the breadth of the [one] board;
22 zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
two handles [are] to one board, joined to one another; so he has made for all the boards of the Dwelling Place.
23 Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
And he makes the boards for the Dwelling Place; twenty boards for the south side southward;
24 na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
and he has made forty sockets of silver under the twenty boards: two sockets under one board for its two handles, and two sockets under the other board for its two handles.
25 Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
And for the second side of the Dwelling Place, for the north side, he has made twenty boards,
26 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
and their forty sockets of silver: two sockets under one board, and two sockets under the other board;
27 Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
and for the sides of the Dwelling Place westward, he has made six boards;
28 na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
and he has made two boards for the corners of the Dwelling Place, in the two sides;
29 Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
and they have been twins below, and together they are twins at its head, at one ring; so he has done to both of them at the two corners;
30 Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
and there have been eight boards; and their sockets of silver [are] sixteen sockets, two sockets under one board.
31 Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
And he makes bars of shittim wood: five for the boards of the first side of the Dwelling Place,
32 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
and five bars for the boards of the second side of the Dwelling Place, and five bars for the boards of the Dwelling Place, for the sides westward;
33 Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
and he makes the middle bar to enter into the midst of the boards from end to end;
34 Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
and he has overlaid the boards with gold, and he has made their rings of gold, places for bars, and he overlays the bars with gold.
35 Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
And he makes the veil of blue, and purple, and scarlet, and twined linen; he has made it [with] cherubim—the work of a designer;
36 Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
and he makes four pillars of shittim [wood] for it, and overlays them with gold; their pegs [are] of gold; and he casts four sockets of silver for them.
37 Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
And he makes a covering for the opening of the tent, of blue, and purple, and scarlet, and twined linen, the work of an embroiderer,
38 Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.
also its five pillars, and their pegs; and he overlaid their tops and their fillets [with] gold, and their five sockets [are] bronze.

< Kutoka 36 >