< Kutoka 35 >
1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Et Moïse réunit toute l’assemblée des fils d’Israël, et leur dit: Ce sont ici les choses que l’Éternel a commandé de faire:
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Pendant six jours le travail se fera, mais le septième jour sera pour vous un [jour] saint, un sabbat de repos [consacré] à l’Éternel: quiconque fera une œuvre ce jour-là, sera mis à mort.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Vous n’allumerez point de feu, dans toutes vos habitations, le jour du sabbat.
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Et Moïse parla à toute l’assemblée des fils d’Israël, en disant: Voici ce que l’Éternel a commandé, disant:
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Prenez, de ce qui est à vous, une offrande pour l’Éternel; que tout homme qui a un esprit libéral apporte l’offrande élevée de l’Éternel: de l’or, et de l’argent, et de l’airain;
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
et du bleu, et de la pourpre, et de l’écarlate, et du coton blanc, et du poil de chèvre;
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
et des peaux de béliers teintes en rouge, et des peaux de taissons, et du bois de sittim;
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
et de l’huile pour le luminaire, et des aromates pour l’huile de l’onction et pour l’encens des drogues odoriférantes;
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
et des pierres d’onyx, et des pierres à enchâsser pour l’éphod et pour le pectoral.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
– Et que tous les hommes intelligents parmi vous viennent, et fassent tout ce que l’Éternel a commandé:
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
le tabernacle, sa tente, et sa couverture, ses agrafes, et ses ais, ses traverses, ses piliers, et ses bases;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
l’arche et ses barres, le propitiatoire, et le voile qui sert de rideau;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
la table et ses barres, et tous ses ustensiles, et le pain de proposition;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
et le chandelier du luminaire, et ses ustensiles, et ses lampes, et l’huile du luminaire;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
et l’autel de l’encens et ses barres; et l’huile de l’onction, et l’encens des drogues odoriférantes; et le rideau de l’entrée, pour l’entrée du tabernacle;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
l’autel de l’holocauste et la grille d’airain qui lui appartient, ses barres et tous ses ustensiles; la cuve et son soubassement;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
les tentures du parvis, ses piliers, et ses bases, et le rideau de la porte du parvis;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
les pieux du tabernacle, et les pieux du parvis, et leurs cordages;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
les vêtements de service pour servir dans le lieu saint, les saints vêtements pour Aaron, le sacrificateur, et les vêtements de ses fils pour exercer la sacrificature.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
Et toute l’assemblée des fils d’Israël sortit de devant Moïse.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
Et tout homme que son cœur y porta, et tous ceux qui avaient un esprit libéral, vinrent et apportèrent l’offrande de l’Éternel pour l’œuvre de la tente d’assignation, et pour tout son service, et pour les saints vêtements.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Et les hommes vinrent avec les femmes: tout homme qui offrit une offrande tournoyée d’or à l’Éternel, tous ceux qui avaient un esprit libéral apportèrent des anneaux de nez, et des pendants d’oreille, et des anneaux, et des colliers, toutes sortes d’objets d’or.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Et tout homme chez qui se trouva du bleu, et de la pourpre, et de l’écarlate, et du coton blanc, et du poil de chèvre, et des peaux de béliers teintes en rouge, et des peaux de taissons, les apporta.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Tout [homme] qui offrit une offrande élevée d’argent et d’airain, apporta l’offrande de l’Éternel; et tout [homme] chez qui se trouva du bois de sittim pour toute l’œuvre du service, l’apporta.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
Et toute femme intelligente fila de sa main, et apporta ce qu’elle avait filé: le bleu, et la pourpre, et l’écarlate, et le fin coton;
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
et toutes les femmes habiles que leur cœur y porta filèrent du poil de chèvre.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
Et les princes apportèrent les pierres d’onyx et les pierres à enchâsser pour l’éphod et pour le pectoral;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
et les aromates, et l’huile pour le luminaire, et pour l’huile de l’onction, et pour l’encens des drogues odoriférantes.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Les fils d’Israël, tout homme et toute femme qui eurent un esprit libéral pour apporter pour toute l’œuvre que, par Moïse, l’Éternel avait commandé de faire, apportèrent une offrande volontaire à l’Éternel.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Et Moïse dit aux fils d’Israël: Voyez, l’Éternel a appelé par nom Betsaleël, fils d’Uri, fils de Hur, de la tribu de Juda;
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
et il l’a rempli de l’esprit de Dieu, en sagesse, en intelligence, et en connaissance, et pour toute espèce d’ouvrages;
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
et pour faire des inventions, pour travailler en or, et en argent, et en airain;
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
et pour tailler des pierres à enchâsser, et pour tailler le bois, afin d’exécuter des dessins en toutes sortes d’ouvrages;
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
et à lui et à Oholiab, fils d’Akhisamac, de la tribu de Dan, il a mis au cœur d’enseigner;
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
il les a remplis de sagesse de cœur pour faire tout ouvrage de graveur et d’inventeur, et de brodeur en bleu et en pourpre, en écarlate et en fin coton, et [tout ouvrage] de tisserand, faisant toute espèce de travail, et inventant des dessins.