< Kutoka 35 >
1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Moïse ayant convoqué toute l’assemblée d’Israël, leur dit: « Voici les choses que Yahweh a ordonné de faire:
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Tu travailleras six jours, mais le septième sera pour vous un jour consacré; un jour de repos complet en l’honneur de Yahweh. Quiconque fera un travail ce jour-là sera puni de mort.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Vous n’allumerez de feu dans aucune de vos demeures le jour du sabbat. »
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Moïse parla à toute l’assemblée des enfants d’Israël, en disant: « Voici ce que Yahweh a ordonné:
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Prélevez sur vos biens une offrande pour Yahweh. Tout homme au cœur bien disposé apportera en offrande à Yahweh de l’or, de l’argent et de l’airain,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
de la pourpre violette, de la pourpre écarlate, du cramoisi, du fin lin et du poil de chèvre,
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
des peaux de béliers teintes en rouge et des peaux de veaux marins, et du bois d’acacia,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
de l’huile pour le chandelier, des aromates pour l’huile d’onction et pour le parfum d’encensement,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
des pierres d’onyx et d’autres pierres à enchâsser pour l’éphod et pour le pectoral.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
Que tous ceux d’entre vous qui ont de l’habileté viennent et exécutent tout ce que Yahweh a ordonné:
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
la Demeure, sa tente et sa couverture, ses anneaux, ses ais, ses traverses, ses colonnes et ses socles;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
l’arche et ses barres; le propitiatoire et le voile de séparation;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
la table avec ses barres et tous ses ustensiles, et les pains de proposition;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
le chandelier avec ses ustensiles, ses lampes et l’huile pour le chandelier;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
l’autel des parfums et ses barres; l’huile d’onction et le parfum pour l’encensement: la tenture de la porte pour l’entrée de la Demeure;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
l’autel des holocaustes, sa grille d’airain, ses barres et tous ses ustensiles; la cuve avec sa base;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
les rideaux du parvis, ses colonnes, ses socles et la tenture de la porte du parvis;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
les pieux de la Demeure, les pieux du parvis avec leurs cordages;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
les vêtements de cérémonie pour le service dans le sanctuaire, les vêtements sacrés pour le grand prêtre Aaron, et les vêtements de ses fils pour les fonctions du sacerdoce. »
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
Toute l’assemblée des enfants d’Israël étant sortie de devant Moïse,
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
tous ceux que leur cœur y portait et tous ceux dont l’esprit était bien disposé vinrent et apportèrent une offrande à Yahweh pour la construction de la tente de réunion, pour tout son service et pour les vêtements sacrés.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Les hommes vinrent aussi bien que les femmes; tous ceux dont le cœur était bien disposé apportèrent des boucles, des anneaux, des bagues, des bracelets, toutes sortes d’objets d’or; chacun présenta l’offrande d’or qu’il avait destinée à Yahweh.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Tous ceux qui avaient chez eux de la pourpre violette, de la pourpre écarlate et du cramoisi, du fin lin et du poil de chèvre, des peaux de béliers teintes en rouge et des peaux de veaux marins, les apportèrent.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Tous ceux qui avaient prélevé une offrande d’argent et d’airain, apportèrent l’offrande à Yahweh. Tous ceux qui avaient chez eux du bois d’acacia pour tous les ouvrages destinés au culte, l’apportèrent.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
Toutes les femmes qui avaient de l’habileté, filèrent de leurs mains, et elles apportèrent leur ouvrage: de la pourpre violette, de la pourpre écarlate, du cramoisi et du fin lin.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
Toutes les femmes que leur cœur y portait, et qui avaient de l’habileté, filèrent du poil de chèvre.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
Les principaux du peuple apportèrent des pierres d’onyx et d’autres pierres à enchâsser pour l’éphod et le pectoral;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
des aromates et de l’huile pour le chandelier, pour l’huile d’onction et pour le parfum odoriférant.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Tous les enfants d’Israël, hommes et femmes, qui étaient disposés de cœur à contribuer à tout ouvrage que Yahweh avait commandé de faire par l’organe de Moïse, apportèrent à Yahweh des offrandes volontaires.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Moïse dit aux enfants d’Israël: « Sachez que Yahweh a choisi Béseléel, fils d’Uri, fils de Hur, de la tribu de Juda.
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
Il l’a rempli de l’esprit de Dieu, de sagesse, d’intelligence et de savoir pour toutes sortes d’ouvrages,
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
pour faire des inventions, pour travailler l’or, l’argent et l’airain,
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
pour graver les pierres à enchâsser, pour tailler le bois et exécuter toutes sortes d’ouvrages d’art.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
Il a mis aussi dans son cœur le don d’enseignement, de même qu’en Ooliab, fils d’Achisamech, de la tribu de Dan.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
Il les a remplis d’intelligence pour exécuter tous les ouvrages de sculpture et d’art, pour tisser d’un dessin varié la pourpre violette, la pourpre écarlate, le cramoisi et le fin lin, pour exécuter toute espèce de travaux et pour faire des inventions.