< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Therfor whanne al the cumpanye of the sones of Israel was gaderid, Moises seide to hem, These thingis it ben, whiche the Lord comaundide to be doon.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Sixe daies ye schulen do werk, the seuenthe dai schal be hooli to you, the sabat and reste of the Lord; he that doith werk in the sabat schal be slayn.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Ye schulen not kyndle fier in alle youre dwellyng places bi the `dai of sabat.
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
And Moises seide to al the cumpeny of the sones of Israel, This is the word which the Lord comaundide, and seide,
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Departe ye at you the firste fruytis to the Lord; ech wilful man and of redi wille offre tho to the Lord, gold, and siluer, and bras,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
and iacynct, and purpur, and reed selk twies died, and bijs, heeris of geet,
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
and skynnys of rammes maad reed, and of iacynt,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
trees of Sechym, and oile to liytis to be ordeyned, and that the oynement be maad, and encense moost swete,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
stoonus of onochyn and gemmes, to the ournyng of the `cloth on the schuldris, and of the racional.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
Who euer of you is wijs, come he, and make that, that the Lord comaundide,
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
that is, the tabernacle, and the roof therof, and the hilyng; ryngis, and bildyngis of tablis, with barris, stakis, and foundementis;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
the arke, and barris; the propiciatorie, and the veil, which is hangid byfore it;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
the bord with barris, and vesselis, and with looues of settyng forth;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
the candilstike to susteyne liytis, the vesselis, and lanternes therof, and oile to the nurschyngis of fyris; the auter of encense, and the barris;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
the oile of anoyntyng, and encense of swete smellynge spiceries; the tente at the dore of the tabernacle;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
the auter of brent sacrifice, and his brasun gridele, with hise barris, and vessels; the `greet waischyng vessel, and `his foundement;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
the curteyns of the large street, with pileris and foundementis; the tente in the doris of the porche;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
the stakis of the tabernacle and of the large street, with her coordis;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
the clothis, whose vss is in `the seruyce of seyntuarie; the clothis of Aaron bischop, and of hise sones, that thei be set in preesthod to me.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
And al the multitude of the sones of Israel yede out of `the siyt of Moises,
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
and offride with moost redi soule and deuout the firste thingis to the Lord, to make the werk of the tabernacle of witnessyng, what euer was nedeful to the ournyng, and to hooli clothis.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Men and wymmen yauen bies of the armes, and eeryngis, ryngis, and ournementis of `the arm niy the hond; ech goldun vessel was departid in to the yiftis of the Lord.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
If ony man hadde iacynt, and purpur, and `reed selk twies died, bijs, and the heeris of geet, skynnes of rammes maad reed, and of iacynt,
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
metals of siluer, and of bras, thei offeryden to the Lord, and trees of Sechym in to dyuerse vsis.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
But also wymmen tauyt yauen tho thingis, whiche thei hadden spunne, iacynt, purpur, and vermyloun,
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
and bijs, and the heeris of geet; and yauen alle thingis by her owne fre wille.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
Forsothe princes offeriden stoonys of onychyn and iemmes, to the `cloth on the schuldris, and to the racional, and swete smellynge spiceries,
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
and oyle to the liytis to be ordeyned, and to make redi oynement, and to make the encense of swettist odour.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Alle men and wymmen offeriden yiftis with deuout soule, that the werkis schulden be maad, whiche the Lord comaundide bi the hond of Moyses; alle the sones of Israel halewiden wilful thingis to the Lord.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
And Moises seide to the sones of Israel, Lo! the Lord hath clepid Beseleel bi name, the sone of Hury, sone of Hur, of the lynage of Juda;
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
and the Lord hath fillid hym with the spirit of God, of wisdom, and of vndurstondyng, and of kunnyng, and with al doctryn,
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
to fynde out and to make werk in gold, and siluer, and bras, and in stoonys to be grauun,
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
and in werk of carpentrie; what euer thing may be foundun craftili,
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
the Lord yaf in his herte; and the Lord clepide Ooliab, the sone of Achymasech, of the lynage of Dan;
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
the Lord tauyte bothe `with wisdom, that thei make the werkis of carpenter, of steynour, and of broiderere, of iacynt, and purpur, and of `reed selk, and of bijs, and that thei make alle thingis, and fynde alle newe thingis.

< Kutoka 35 >