< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
And Moses assembled all the congregation of the children of Israel, and said to them, These [are] the words which the LORD hath commanded, that [ye] should do them.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Six days shall work be done; but on the seventh day there shall be to you a holy day, a sabbath of rest to the LORD: whoever doth work therein shall be put to death.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Ye shall kindle no fire throughout your habitations upon the sabbath-day.
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
And Moses spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, This [is] the thing which the LORD commanded, saying,
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Take ye from among you an offering to the LORD: whoever [is] of a willing heart, let him bring it, an offering of the LORD; gold, and silver, and brass,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
And blue, and purple, and scarlet, and fine linen, and goats' [hair],
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
And rams' skins dyed red, and badgers' skins, and shittim wood,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
And oil for the light, and spices for anointing oil, and for the sweet incense,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
And onyx stones, and stones to be set for the ephod, and for the breast-plate.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
And every wise-hearted among you shall come, and make all that the LORD hath commanded;
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
The tabernacle, its tent, and its covering, its buttons, and its boards, its bars, its pillars, and its sockets,
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
The ark, and its staffs, [with] the mercy-seat, and the vail of the covering,
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
The table, and its staffs, and all its vessels, and the show-bread,
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
The candlestick also for the light, and its furniture, and its lamps, with the oil for the light,
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
And the incense-altar, and its staffs, and the anointing oil, and the sweet incense, and the hanging for the door at the entrance of the tabernacle,
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
The altar of burnt-offering, with its brazen grate, its staffs, and all its vessels, the laver and its foot,
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
The hangings of the court, its pillars, and their sockets, and the hanging for the door of the court,
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
The pins of the tabernacle, and the pins of the court, and their cords,
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
The clothes of service, to do service in the holy [place], the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
And all the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
And they came, every one whose heart excited him, and every one whom his spirit made willing, [and] they brought the LORD'S offering to the work of the tabernacle of the congregation, and for all his service, and for the holy garments.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
And they came, both men and women, as many as were willing-hearted, [and] brought bracelets, and ear-rings, and rings, and tablets, all jewels of gold; and every man that offered, [offered] an offering of gold to the LORD.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
And every man, with whom was found blue, and purple, and scarlet, and fine linen, and goats' [hair], and red skins of rams, and badgers' skins, brought [them].
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Every one that offered an offering of silver and brass brought the LORD'S offering: and every man with whom was found shittim wood for any work of the service, brought [it].
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
And all the women that were wise-hearted spun with their hands, and brought that which they had spun, [both] of blue, and of purple, [and] of scarlet, and of fine linen.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
And all the women whose heart moved them in wisdom spun goats' [hair].
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
And the rulers brought onyx stones, and stones to be set, for the ephod, and for the breast-plate;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
And spice, and oil for the light, and for the anointing oil, and for the sweet incense.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
The children of Israel brought a willing offering to the LORD, every man and woman, whose heart made them willing to bring for all manner of work, which the LORD had commanded to be made by the hand of Moses.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
And Moses said to the children of Israel, See, the LORD hath called by name Bezaleel, the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah;
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
And he hath filled him with the spirit of God, in wisdom, in understanding, and in knowledge, and in all manner of workmanship;
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
And to devise curious works, to work in gold, and in silver, and in brass,
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
And in the cutting of stones, to set [them], and in carving of wood, to make any manner of curious work.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
And he hath put in his heart that he may teach, [both] he and Aholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
Them hath he filled with wisdom of heart, to work all manner of work, of the engraver, and of the skillful workmen, and of the embroiderer, in blue, and in purple, in scarlet, and in fine linen, and of the weaver, [even] of them that do any work, and of those that devise curious work.

< Kutoka 35 >