< Kutoka 35 >
1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
And Moses gathered together all the congregation of the children of Israel, and said unto them, These are the things which the Lord hath commanded, that ye should do them.
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
Six days shall work be done, but on the seventh day there shall be to you a holy day, a sabbath of rest to the Lord: whosoever doth work thereon shall be put to death.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Ye shall not kindle any fire throughout your habitations upon the sabbath day.
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
And Moses said unto all the congregation of the children of Israel, as followeth, This is the thing which the Lord hath commanded, saying,
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
Take ye from among you an offering unto the Lord; whosoever is of a willing heart, let him bring it, an offering of the Lord: Gold, and silver, and copper,
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
And blue, and purple, and scarlet yarn, and linen thread, and goats' hair,
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
And rams' skills dyed red, and badgers' skins, and shittim wood,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
And oil for the lighting, and spices, for the anointing oil, and for the incense of spices,
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
And onyx stones, and stones for setting, for the ephod, and for the breastplate.
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
And all the wise-hearted among you shall come, and make all that which the Lord hath commanded:
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
The tabernacle, its tent, and its covering, its hooks, and its boards, its bars, its pillars, and its sockets;
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
The ark, and its staves, [with] the mercy-seat, and the vail of the separation;
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
The table, and its staves, and all its vessels, and the showbread;
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
And the candlestick for the lighting, and its vessel, and its lamps, with the oil for the lighting;
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
And the altar of incense, and its staves, and the anointing oil, and the incense of spices, and the hanging for the door at the entrance of the tabernacle;
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
The altar of burnt-offering, with its grating of copper, its staves, and all its vessels, the laver and its foot;
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
The hangings of the court, its pillars, and its sockets, and the hanging for the door of the court;
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
The pins of the tabernacle, and the pins of the court, and their cords;
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
The cloths of service, to do service therewith in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in as priests.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
And all the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
And they came, every man whose heart stirred him up; and every one whom his spirit made willing, brought the Lord's offering for the work of the tabernacle of the congregation, and for all its service, and for the holy garments.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
And they came, the men with the women; whoever was willing-hearted, brought bracelets, and earrings, and finger-rings, and tablets, all kinds of ornaments of gold, and every man that offered an offering of gold unto the Lord.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
And every man, with whom was found blue, and purple, and scarlet yarn, and linen thread, and goats' hair, and rams' skins dyed red, and badgers' skins, brought them.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Every one that did offer an offering of silver and copper brought it as the Lord's offering; and every one with whom was found shittim wood for any work of the service, brought it.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
And all the women that were wise-hearted spun with their hands, and they brought that which they had spun, of the blue, and of the purple, and of the scarlet yarn, and of the linen thread.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
And all the women whose heart stirred them up in wisdom spun the goats' hair.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
And the princes brought the onyx stones, and the stones for setting, for the ephod, and for the breastplate;
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
And the spice and the oil, for lighting, and for the anointing oil, and for the incense of spices.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Every man and woman, whose heart made them willing to bring for all manner of work, which the Lord had commanded to be made, by the hand of Moses, even that brought the children of Israel as a free-will offering unto the Lord.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
And Moses said unto the children of Israel, See, the Lord hath called by name Bezalel the son of Uri, the son of Chur, of the tribe of Judah;
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
And he hath filled him with the spirit of God, in wisdom, in understanding, and in knowledge, and in all manner of workmanship;
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
And to devise works of art, to work in gold, and in silver, and in copper,
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
And in the cutting of stones, to set them, and in the carving of wood, to make any manner of work of art.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
And to teach hath he put in his heart, both to him, and to Aholiab, the son of Achissamach, of the tribe of Dan.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
He hath filled them with wisdom of heart, to execute all manner of work, of the engraver, and of the designing weaver, and of the embroiderer, in blue, and in purple, in scarlet yarn, and in linen thread, and of the weaver, of those that do every species of work, and of those that devise works of art.