< Kutoka 35 >

1 Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
Mousese da Isala: ili dunu fi huluane gilisima: ne sia: i. Amalalu, e da ilima amane sia: i, “Hina Gode da dilima amane sia: sa,
2 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
‘Dilia da hialigi amoga eso gafeyale gala amoga dilia da hawa: hamomu da defea. Be eso fesu amo da Na hadigi eso Nama modale ligiagai dagoi. Amo esoga dilia helefima. Nowa da Sa: bade esoga hawa: hamosea, amo fanelegema.
3 Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
Hawa: hamosu maedafa hamoma. Sa: bade esoga, dilia diasu ganodini, lalu mae didima.’”
4 Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
Mousese da Isala: ili dunu huluane ilima amane sia: i, “Hina Gode da dilima amane sia: sa,
5 Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
‘Hina Godema hahawane udigili iasu gaguli misa. Nowa dunu da hanai galea, e da hahawane udigili iasu amo gouli o silifa o balase amo gaguli misa.
6 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
Eno da abula noga: iwane o sibi hinabo mola: ya: i o oga: iyei o yoi. Eno da abula goudi hinabo amoga hamoi.
7 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
Sibi gawali gadofo ulasi, bulamagau gadofo, aga: isia ifa,
8 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
gamali susuligi, hedama: ne fodole nasu amo ilegesu susuligi amola gabusiga: manoma amoga gilisimusa:
9 vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
Eno da ‘ganilia: ne’ amola eno igi noga: idafa amo gobele salasu Ouligisu dunu ea ‘ifode’ amola Bidegi Gaga: su ganodini salimusa:’”
10 “Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
Mousese da Gode Ea sia: eno Isala: ili dunuma amane adole i, “Hawa: hamosu dunu ida: iwane dilia gilisisu ganodini esalebe, ilia da misini amola Gode Ea hamoma: ne sia: i liligi huluane hamomu da defea.
11 Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
Amo da Gode Ea Abula Diasu, ea dedebosu liligi huluane, ea ma: go, abula: ime, bulufalegei dududawalo, golasu ifa, amo ea bai huluane,
12 Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
Gode Ea Gousa: su Sema Gagili, ea gaguli ahoasu ifa, ea ga: lu amola abula amo da Gode Ea Gousa: su Sema Gagili wamolegesu,
13 meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
fafai, ea ifa amola ea liligi huluane, agi ga: gi Godema iasu,
14 kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
gamali bai amola ea liligi, gamali, gamali susuligi,
15 madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
gabusiga: manoma amo gobesisu oloda amola ea gaguli ahoasu ifa, ilegesu susuligi, gabusiga: manoma, Gode Ea Abula Diasu logo holei abula ga: su,
16 madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
gobele salasu oloda, ea balasega hamoi gigiadomai, ea ifa amola liligi huluane, dodofesu ofodo amola ea bai,
17 pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
gagoi gaga: su abula amola ea golasu ifa amola ilia bai huluane, gagoi ea logo holei ga: su abula,
18 vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
Abula Diasu amola Gagoi ilia udidisu ifa sagasu amola efe udidisu,
19 mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
abula ida: iwane gobele salasu dunu da Hadigi Malei Sesei ganodini hawa: hamosea salasu amola hadigi abula Elane amola egefelali sala.” Mousese da amo huluane hamoma: ne sia: i.
20 Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
Isala: ili dunu da yolesili asili,
21 na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
amola huluane da hanai galea, hahawane udigili iasu amo Hina Gode Ea Abula Diasu hahamoma: ne Ema gaguli misi. Ilia da liligi huluane, amo da Hina Godema nodone sia: ne gadomusa: amola gobele salasu dunu ilia abula hamomusa: , amo gaguli misi.
22 Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Nowa da hanai galea, dunu amola uda da nina: hamosu liligi amo gouli gedusu, abula bagedigi, igi noga: i, gouli gisa: gini amola gouli nina: hamosu liligi huluane Hina Godema ima: ne gaguli misi.
23 Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
Nowa da abula noga: iwane o sibi hinabo mola: ya: i o oga: iyei o yoi o goudi hinaboga hamoi abula o sibi gawali gadofo ulasi o bulamagau gadofo amo liligi gagui dialebe, amo gaguli misi.
24 Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
Amola nowa da silifa o balase gagui galea, ilia da ilia hahawane udigili iasu Hina Godema gaguli misi. Amola nowa da aga: isia ifa Hina Gode Ea liligi hahamoma: ne defele gala da amo gaguli misi.
25 Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
Bagade dawa: su hawa: hamosu uda da abula nodomesu efe ahea: ya: i noga: iwane amola nodomesu efe amo mola: ya: i, oga: iyei amola yoi sibi hinabo amo gobiaha: i agoane hamoi amo gaguli misi.
26 Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
Ilia da goudi hinabo amoga efe hamosu.
27 Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
Isala: ili fi asigilai ouligisu dunu da ‘ganilia: ne’ amola igi ida: iwane eno, amo ‘ifode’ amola Bidegi Gaga: su amo ganodini salimusa: gaguli misi.
28 Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
Amola ilia da hedama: ne fodole nasu, gamali susuligi, ligiagasu susuligi amola gabusiga: manoma susuligi gaguli misi dagoi.
29 Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
Nowa Isala: ili dunu da hanai galea da Hina Gode da Mousesema sia: i defele, Ea Abula Diasu hawa: hamomusa: gini, hahawane udigili iasu Hina Godema gaguli misi dagoi.
30 Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
Mousese da Isala: ili dunuma amane sia: i, “Hina Gode da Bisa: liele (Uli egefe amola He ea aowa - Yuda fi dunu) amo ilegei dagoi.
31 naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
E da Ea A: silibu ea gasa Ema i dagoi. E da Gode Ea A: silibu Hadigidafa amo Ea gasa lai dagoiba: le, hawa: hamosu bagade dawa: , amola liligi huluane noga: idafa hamoma: ne e da gasa gala.
32 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
E da gouli, silifa amola balase amoga liligi ida: iwane hamomu dawa: , amola amoga osa: le dedesu hou noga: idafa dawa:
33 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
E da igi ida: iwane gala amo hedofasu hou amola amoga osa: le dedesu hou noga: le dawa: E da ifa oso gasa: su hou noga: le dawa: amola liligi huluane hahamomusa: , e da dawa: lai amola gasa gala.
34 Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
Hina Gode da ema amola Ouhoulia: be (Ahisama: ge ea mano - Da: ne fi dunu) elama bagade dawa: su hou i dagoi. Ela da Hina Gode Ea A: silibu Hadigidafaga gasa lai dagoiba: le, ela da eno dunuma amo hou olelemu defele esala.
35 Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.
Ela da hawa: hamosu huluane hamomusa: gasa bagade gala. Amo da osa: le dedesu hou, hawa: hamomusa: meloa ilegele dedesu, abula amunisu amola sibi hinabo efe mola: ya: i, oga: iyei amola yoi amunasu hou amola abula hou eno. Ilia da hawa: hamosu huluane dawa: , amola liligi hamoma: ne ilegesu dedesu bagade dawa:”

< Kutoka 35 >