< Kutoka 34 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
Et ensuite: Taille-toi, dit-il, deux tables de pierre à l’instar des premières, et j’écrirai dessus les paroles que contenaient les tables que tu as rompues.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
Sois prêt dès le matin, pour monter aussitôt sur la montagne de Sinaï, et tu te tiendras avec moi sur le sommet de la montagne.
3 Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
Que nul ne monte avec toi, et que personne ne soit vu sur toute la montagne; que les bœufs même et les brebis ne paissent point contre.
4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
Il tailla donc deux tables de pierre, comme celles qui avaient été auparavant; et se levant de nuit, il monta sur la montagne de Sinaï, comme lui avait ordonné le Seigneur, portant avec lui les tables.
5 Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
Et lorsque le Seigneur fut descendu dans la nuée. Moïse se tint avec lui, invoquant le nom du Seigneur.
6 Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
Et le Seigneur passant devant lui, Moïse dit: Dominateur, Seigneur Dieu, miséricordieux et clément, patient et d’une abondante miséricorde, et très véritable,
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
Qui gardez votre miséricorde pour des milliers de créatures; qui effacez l’iniquité, les crimes et les péchés, et nul auprès de vous n’est innocent par lui-même; qui rendez l’iniquité des pères aux fils et aux petits-fils, jusqu’à la troisième et la quatrième génération.
8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.
Et aussitôt Moïse se prosterna incliné vers la terre, et adorant,
9 Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
Dit: Si j’ai trouvé grâce en votre présence. Seigneur, je vous conjure de marcher avec nous (car Ce peuple est d’un cou roide), d’effacer nos iniquités et nos péchés, et de nous prendre en possession.
10 Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
Le Seigneur répondit: Moi, je ferai alliance, tous le voyant, je ferai des signes, qui n’ont jamais été vus sur la terre, ni dans aucune nation, afin qu’il voie, ce peuple au milieu duquel tu es, l’œuvre terrible du Seigneur que je dois faire.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Observe tout ce qu’aujourd’hui je te commande; moi-même, je chasserai devant ta face l’Amorrhéen, le Chananéen, l’Héthéen, le Phérézéen aussi, l’Hévéen et le Jébuséen.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
Prends garde de ne jamais lier des amitiés avec les habitants de cette terre, lesquelles soient pour toi une ruine;
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
Mais détruis leurs autels, brise leurs statues et coupe leurs bois sacrés.
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
N’adore point de dieu étranger. Le Seigneur, son nom est: jaloux; Dieu est jaloux.
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
Ne fais point d’alliance avec les hommes de ces pays-là, de peur que lorsqu’ils auront forniqué avec leurs dieux, et qu’ils auront adoré leurs simulacres, quelqu’un ne t’invite à manger des victimes immolées.
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
Tu ne prendras point de femmes d’entre leurs filles pour tes fils, de peur qu’après qu’elles-mêmes auront forniqué, elles ne fassent forniquer aussi tes fils avec leurs dieux.
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
Tu ne feras point de dieux jetés en fonte.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
Tu garderas la solennité des azymes. Pendant sept jours tu mangeras des azymes, comme je t’ai ordonné, au temps du mois des nouveaux fruits; car c’est au mois du printemps que tu es sorti de l’Egypte.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
Tout mâle qui ouvre un sein, sera à moi. Le premier-né d’entre tous les animaux, tant des bœufs que des brebis, sera à moi.
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
Tu rachèteras le premier-né de l’âne avec une brebis; mais si tu ne donnes pas de rançon pour lui, il sera tué. Tu rachèteras le premier-né de tes fils; et tu ne paraîtras point devant moi les mains vides.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
Pendant six jours tu travailleras; au septième jour, tu cesseras de labourer et de moissonner.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
Tu feras la solennité des semaines, à l’époque des prémices des fruits de ta moisson de froment, et la solennité de la récolte, quand, le temps de l’année revenant, tout se serre.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
À trois époques de l’année tous tes mâles paraîtront en la présence du tout-puissant Seigneur Dieu d’Israël.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
Car lorsque j’aurai enlevé les nations de devant ta face, et que j’aurai étendu tes limites, nul ne cherchera à surprendre ta terre, toi montant, et paraissant en la présence du Seigneur ton Dieu trois fois l’année.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
Tu ne sacrifieras point sur du levain le sang de mon hostie, et il ne restera pas le matin de la victime de la solennité de la Pâque.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
Tu offriras les prémices des fruits de ta terre dans la maison du Seigneur ton Dieu. Tu ne feras point cuire un chevreau dans le lait de sa mère.
27 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
Le Seigneur dit encore à Moïse: Ecris pour toi ces paroles par lesquelles j’ai fait alliance et avec toi et avec Israël.
28 Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
Il fut donc là avec le Seigneur quarante jours et quarante nuits: il ne mangea point de pain et il ne but point d’eau, et il écrivit sur les tables les dix paroles de l’alliance.
29 Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
Et lorsque Moïse descendait de la montagne de Sinaï, il tenait les deux tables du témoignage, et il ignorait que sa face était rayonnante de lumière, depuis l’entretien du Seigneur avec lui.
30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
Or Aaron et les enfants d’Israël, voyant la face de Moïse rayonnante, craignirent de s’approcher.
31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
Mais appelés par lui, ils revinrent, tant Aaron que les princes de la synagogue. Et après qu’il leur eut parlé,
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
Vinrent aussi vers lui tous les enfants d’Israël, auxquels il ordonna toutes les choses qu’il avait entendues du Seigneur sur la montagne de Sinaï.
33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
Et, ces discours achevés, il mit un voile sur sa face.
34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
Entré auprès du Seigneur, et parlant avec lui, il ôtait ce voile jusqu’à ce qu’il en sortît, et c’est alors qu’il disait aux enfants d’Israël toutes les choses qui lui avaient été commandées.
35 waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.
Ceux-ci voyaient que la face de Moïse rayonnait, lorsqu’il sortait, mais lui la voilait de nouveau, s’il avait à leur parler.

< Kutoka 34 >