< Kutoka 34 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
Et l'Éternel dit à Moïse: Taille-toi deux tables de pierre comme les premières; et j'écrirai sur ces tables les paroles qui étaient sur les premières tables que tu as brisées.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
Et sois prêt au matin; et monte, dès le matin, sur le mont Sinaï; tiens-toi là devant moi, sur le sommet de la montagne.
3 Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
Mais que personne ne monte avec toi, et même que personne ne paraisse sur toute la montagne; que ni brebis, ni bœufs ne paissent même près de cette montagne.
4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
Moïse donc tailla deux tables de pierre comme les premières, et se leva de bon matin, et monta sur le mont Sinaï, comme l'Éternel le lui avait commandé; et il prit en sa main deux tables de pierre.
5 Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
Et l'Éternel descendit dans la nuée, et se tint là avec lui, et cria le nom de l'Éternel.
6 Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
Et l'Éternel passa devant lui, et cria: L'Éternel, l'Éternel! le Dieu miséricordieux et compatissant, lent à la colère, abondant en grâce et en fidélité,
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
Qui conserve sa grâce jusqu'à mille générations, qui pardonne l'iniquité, le crime et le péché, mais ne tient point le coupable pour innocent; qui punit l'iniquité des pères sur les enfants et sur les enfants des enfants, jusqu'à la troisième et à la quatrième génération.
8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.
Et Moïse s'inclina aussitôt vers la terre et se prosterna;
9 Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
Et il dit: Seigneur, je te prie, si j'ai trouvé grâce à tes yeux, que le Seigneur marche au milieu de nous; car c'est un peuple de cou roide; et pardonne notre iniquité et notre péché, et possède-nous comme ton héritage.
10 Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
Et l'Éternel répondit: Voici, je traite une alliance. Je ferai, devant tout ton peuple, des merveilles qui n'ont point été faites sur toute la terre, ni chez aucune nation; et tout le peuple au milieu duquel tu te trouves, verra l'œuvre de l'Éternel; car ce que je vais faire avec toi, sera une chose terrible.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Prends garde à ce que je te commande aujourd'hui. Voici, je vais chasser de devant toi les Amoréens, les Cananéens, les Héthiens, les Phéréziens, les Héviens, et les Jébusiens.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
Garde-toi de traiter alliance avec les habitants du pays dans lequel tu vas entrer, de peur qu'ils ne soient en piège au milieu de toi.
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
Mais vous démolirez leurs autels, vous briserez leurs statues, et vous couperez leurs emblèmes d'Ashéra.
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
Car tu ne te prosterneras point devant un autre dieu, parce que l'Éternel se nomme le Dieu jaloux; c'est un Dieu jaloux.
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
Garde-toi de traiter alliance avec les habitants du pays, de peur que lorsqu'ils se prostitueront après leurs dieux, et sacrifieront à leurs dieux, quelqu'un ne t'invite, et que tu ne manges de son sacrifice;
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
Et que tu ne prennes de ses filles pour tes fils; et que ses filles, se prostituant à leurs dieux, ne fassent aussi prostituer tes fils à leurs dieux.
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
Tu ne te feras point de dieu de fonte.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
Tu observeras la fête des pains sans levain. Tu mangeras pendant sept jours les pains sans levain, comme je te l'ai commandé, à l'époque du mois des épis; car au mois des épis tu es sorti d'Égypte.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
Tout ce qui naît le premier est à moi, et tout ton bétail mâle, premier-né de taureau et de brebis.
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
Mais tu rachèteras avec un agneau ou un chevreau le premier-né d'un âne. Et si tu ne le rachètes pas, tu lui rompras le cou. Tu rachèteras tout premier-né de tes fils; et l'on ne se présentera point à vide devant ma face.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
Tu travailleras six jours; mais au septième jour tu te reposeras; tu te reposeras, même au temps du labourage et de la moisson.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
Tu célébreras la fête des semaines au temps des premiers fruits de la moisson du froment; et la fête de la récolte, à la fin de l'année.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
Trois fois l'an tous les mâles d'entre vous se présenteront devant le Seigneur, l'Éternel, Dieu d'Israël.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
Car je déposséderai les nations devant toi, et j'étendrai tes frontières; et nul ne convoitera ton pays, lorsque tu monteras pour te présenter, trois fois l'an, devant l'Éternel ton Dieu.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
Tu n'offriras point avec du pain levé le sang de mon sacrifice; et le sacrifice de la fête de la Pâque ne passera point la nuit jusqu'au matin.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
Tu apporteras les prémices des premiers fruits de ta terre à la maison de l'Éternel ton Dieu. Tu ne feras point cuire le chevreau dans le lait de sa mère.
27 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
L'Éternel dit aussi à Moïse: Écris ces paroles; car c'est suivant la teneur de ces paroles que j'ai traité alliance avec toi et avec Israël.
28 Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
Et Moïse fut là avec l'Éternel quarante jours et quarante nuits; il ne mangea point de pain et ne but point d'eau; et l'Éternel écrivit sur les tables les paroles de l'alliance, les dix paroles.
29 Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
Or, lorsque Moïse descendit de la montagne de Sinaï, les deux tables du Témoignage étant dans la main de Moïse, qui descendait de la montagne, Moïse ne savait point que la peau de son visage était devenue rayonnante, pendant qu'il parlait avec Dieu.
30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
Mais Aaron et tous les enfants d'Israël virent Moïse, et voici, la peau de son visage rayonnait, et ils craignirent d'approcher de lui.
31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
Alors Moïse les appela, et Aaron et tous les principaux de l'assemblée revinrent vers lui, et Moïse leur parla.
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
Après cela, tous les enfants d'Israël s'approchèrent, et il leur commanda tout ce que l'Éternel lui avait dit sur le mont Sinaï.
33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
Moïse acheva de parler avec eux; et il mit un voile sur sa face.
34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
Et quand Moïse entrait devant l'Éternel pour parler avec lui, il ôtait le voile jusqu'à ce qu'il sortît; puis il sortait et disait aux enfants d'Israël ce qui lui avait été commandé.
35 waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.
Et les enfants d'Israël voyaient que le visage de Moïse, la peau du visage de Moïse, rayonnait; et Moïse remettait le voile sur son visage, jusqu'à ce qu'il entrât, pour parler avec l'Éternel.

< Kutoka 34 >