< Kutoka 34 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
Yahvé dit à Moïse: « Cisèle deux tables de pierre comme les premières. J'écrirai sur ces tablettes les paroles qui étaient sur les premières tablettes, que tu as brisées.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
Prépare-toi dès le matin, monte sur le mont Sinaï et présente-toi là devant moi, au sommet de la montagne.
3 Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
Personne ne montera avec toi et on ne te verra nulle part sur la montagne. Ne laisse pas les troupeaux paître devant cette montagne. »
4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
Il cisela deux tables de pierre comme la première. Moïse se leva de bon matin et monta sur la montagne du Sinaï, comme Yahvé le lui avait ordonné, et il prit dans sa main deux tables de pierre.
5 Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
Yahvé descendit dans la nuée, se tint là avec lui, et proclama le nom de Yahvé.
6 Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
Yahvé passa devant lui, et il proclama: « Yahvé! Yahvé, Dieu de miséricorde et de bonté, lent à la colère, abondant en bonté et en vérité,
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
gardant la bonté pour des milliers de personnes, pardonnant l'iniquité, la désobéissance et le péché, et qui ne pardonne nullement les coupables, visitant l'iniquité des pères sur les enfants, et sur les enfants des enfants, sur la troisième et la quatrième génération. »
8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.
Moïse se précipita, inclina sa tête vers la terre et se prosterna.
9 Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
Il dit: « Si maintenant j'ai trouvé grâce à tes yeux, Seigneur, laisse l'Éternel aller au milieu de nous, même si c'est un peuple à la nuque raide; pardonne notre iniquité et notre péché, et prends-nous pour ton héritage. »
10 Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
Il dit: « Voici, je fais une alliance: devant tout ton peuple, je ferai des merveilles, telles qu'il n'en a jamais été fait dans toute la terre ni dans aucune nation; et tout le peuple au milieu duquel tu es verra l'œuvre de Yahvé, car c'est une chose redoutable que je fais avec toi.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Observez ce que je vous ordonne aujourd'hui. Voici, je vais chasser devant toi l'Amoréen, le Cananéen, le Héthien, le Phérézien, le Hévien et le Jébusien.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
Prenez garde que vous ne fassiez une alliance avec les habitants du pays où vous allez, de peur que ce ne soit un piège pour vous;
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
mais vous démolirez leurs autels, vous briserez leurs colonnes et vous abattrez leurs mâts d'Astarté;
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
car vous ne vous prosternerez pas devant un autre dieu, car Yahvé, dont le nom est Jalous, est un Dieu jaloux.
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
« Ne fais pas d'alliance avec les habitants du pays, de peur qu'ils ne se prostituent à leurs dieux, qu'ils n'offrent des sacrifices à leurs dieux, que l'un d'eux ne t'appelle et que tu ne manges de son sacrifice;
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
et que tu ne prennes de leurs filles pour tes fils, que leurs filles ne se prostituent à leurs dieux et que tes fils ne se prostituent à leurs dieux ».
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
« Vous ne vous ferez pas d'idoles en fonte.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
« Vous célébrerez la fête des pains sans levain. Pendant sept jours, vous mangerez des pains sans levain, comme je vous l'ai ordonné, à l'époque fixée au mois d'Abib, car c'est au mois d'Abib que vous êtes sortis d'Égypte.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
« Tout ce qui ouvre le ventre de la mère m'appartient, ainsi que tout votre bétail mâle, le premier-né des vaches et des brebis.
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
Tu rachèteras le premier-né de l'âne par un agneau. Si tu ne veux pas le racheter, tu lui briseras le cou. Tu rachèteras tous les premiers-nés de tes fils. Personne ne se présentera devant moi à vide.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
« Tu travailleras six jours, mais le septième jour, tu te reposeras: au moment des labours et de la moisson, tu te reposeras.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
« Vous observerez la fête des semaines avec les prémices de la récolte du blé, et la fête de la moisson à la fin de l'année.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
Trois fois par an, tous vos mâles se présenteront devant le Seigneur Yahvé, le Dieu d'Israël.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
Car je chasserai des nations devant toi et j'élargirai tes frontières; aucun homme ne voudra de ton pays quand tu monteras te présenter devant Yahvé, ton Dieu, trois fois par an.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
« Tu n'offriras pas le sang de mon sacrifice avec des pains levés. Le sacrifice de la fête de la Pâque ne sera pas laissé au matin.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
« Tu apporteras les premiers fruits de ton sol à la maison de Yahvé ton Dieu. « Tu ne feras pas bouillir un chevreau dans le lait de sa mère. »
27 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
Yahvé dit à Moïse: « Écris ces paroles, car c'est en fonction de ces paroles que j'ai conclu une alliance avec toi et avec Israël. »
28 Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
Il resta là avec Yahvé quarante jours et quarante nuits; il ne mangea pas de pain et ne but pas d'eau. Il écrivit sur les tables les paroles de l'alliance, les dix commandements.
29 Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
Lorsque Moïse descendit de la montagne du Sinaï avec les deux tables de l'alliance dans sa main, Moïse ne savait pas que la peau de son visage brillait parce qu'il lui parlait.
30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
Lorsqu'Aaron et tous les enfants d'Israël virent Moïse, voici que la peau de son visage brillait, et ils eurent peur de s'approcher de lui.
31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
Moïse les appela, et Aaron et tous les chefs de l'assemblée revinrent vers lui; et Moïse leur parla.
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
Ensuite, tous les enfants d'Israël s'approchèrent, et Moïse leur donna tous les commandements dont Yahvé lui avait parlé sur la montagne de Sinaï.
33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
Lorsque Moïse eut fini de leur parler, il mit un voile sur son visage.
34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
Mais lorsque Moïse entrait devant Yahvé pour lui parler, il ôtait le voile jusqu'à ce qu'il sorte; puis il sortait et disait aux enfants d'Israël ce qu'on lui avait ordonné.
35 waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.
Les enfants d'Israël virent le visage de Moïse, et la peau de son visage resplendit; aussi Moïse remit-il le voile sur son visage, jusqu'à ce qu'il entrât pour lui parler.

< Kutoka 34 >