< Kutoka 34 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
And the LORD said to Moses, Hew thee two tables of stone like the first; and I will write upon [these] tables the words that were in the first tables which thou didst break.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
And be ready in the morning, and come up in the morning to mount Sinai, and present thyself there to me on the top of the mount.
3 Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
And no man shall come up with thee, neither let any man be seen throughout all the mount: neither let the flocks nor herds feed before that mount.
4 Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
And he hewed two tables of stone, like the first; and Moses rose up early in the morning, and went up to mount Sinai, as the LORD had commanded him, and took in his hand the two tables of stone.
5 Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
And the LORD descended in the cloud, and stood with him there, and proclaimed the name of the LORD.
6 Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
And the LORD passed by before him, and proclaimed, The LORD, The LORD God, merciful and gracious, long-suffering, and abundant in goodness and truth.
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
Keeping mercy for thousands, forgiving iniquity and transgression and sin, and that will by no means clear [the guilty]; visiting the iniquity of the fathers upon the children, and upon the children's children, to the third and to the fourth [generation].
8 Mara Mose akasujudu na kuabudu.
And Moses made haste, and bowed his head towards the earth, and worshiped.
9 Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
And he said, If now I have found grace in thy sight, O LORD, let my Lord, I pray thee, go among us (for it [is] a stiff-necked people) and pardon our iniquity and our sin, and take us for thy inheritance.
10 Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
And he said, Behold, I make a covenant: before all thy people I will do wonders, such as have not been done in all the earth, nor in any nation: and all the people among which thou [art], shall see the work of the LORD: for it [is] a terrible thing that I will do with thee.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Observe thou that which I command thee this day: Behold, I drive out before thee the Amorite, and the Canaanite, and the Hittite, and the Perizzite, and the Hivite, and the Jebusite.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
Take heed to thyself, lest thou make a covenant with the inhabitants of the land whither thou goest, lest it be for a snare in the midst of thee:
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
But ye shall destroy their altars, break their images, and cut down their groves.
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
For thou shalt worship no other god: for the LORD, whose name [is] Jealous, [is] a jealous God:
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
Lest thou make a covenant with the inhabitants of the land, and they go astray after their gods, and do sacrifice to their gods, and [one] call thee, and thou eat of his sacrifice;
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
And thou take of their daughters to thy sons, and their daughters go astray after their gods, and make thy sons go astray after their gods.
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
Thou shalt make thee no molten gods.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
The feast of unleavened bread shalt thou keep. Seven days shalt thou eat unleavened bread, as I commanded thee, in the time of the month Abib: for in the month Abib thou camest out of from Egypt.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
Every first-born [is] mine: and every firstling among thy cattle, [whether] ox or sheep, [that is male].
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
But the firstling of an ass thou shalt redeem with a lamb: and if thou shalt not redeem him, then shalt thou break his neck. All the first-born of thy sons thou shalt redeem. And none shall appear before me empty.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
Six days thou shalt work, but on the seventh day thou shalt rest: in time of plowing and in harvest thou shalt rest.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
And thou shalt observe the feast of weeks, of the first-fruits of wheat-harvest, and the feast of in-gathering at the year's end.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
Thrice in the year shall all your male children appear before the LORD GOD, the God of Israel.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
For I will drive out the nations before thee, and enlarge thy borders: neither shall any man desire thy land, when thou shalt go up to appear before the LORD thy God, thrice in the year.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
Thou shalt not offer the blood of my sacrifice with leaven, neither shall the sacrifice of the feast of the passover be left until the morning.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
The first of the first-fruits of thy land thou shalt bring to the house of the LORD thy God. Thou shalt not seethe a kid in his mother's milk.
27 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
And the LORD said to Moses, Write thou these words: for after the tenor of these words I have made a covenant with thee, and with Israel.
28 Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
And he was there with the LORD forty days and forty nights; he neither ate bread nor drank water: and he wrote upon the tables the words of the covenant, the ten commandments.
29 Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
And it came to pass when Moses came down from mount Sinai (with the two tables of testimony in Moses's hand, when he came down from the mount) that Moses knew not that the skin of his face shone, while he talked with him.
30 Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
And when Aaron and all the children of Israel saw Moses, behold, the skin of his face shone, and they were afraid to come nigh him.
31 Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
And Moses called to them; and Aaron and all the rulers of the congregation returned to him; and Moses talked with them.
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
And afterward all the children of Israel came nigh: and he gave them in commandment all that the LORD had spoken with him in mount Sinai.
33 Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
And [till] Moses had done speaking with them, he put a vail on his face.
34 Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
But when Moses went in before the LORD to speak with him, he took the vail off, until he came out. And he came out and spoke to the children of Israel [that] which he was commanded.
35 waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.
And the children of Israel saw the face of Moses, that the skin of Moses's face shone: and Moses put the vail upon his face again, until he went in to speak with him.

< Kutoka 34 >