< Kutoka 33 >

1 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Ondoka mahali hapa, wewe pamoja na hao watu uliowapandisha kutoka Misri, mpande mpaka nchi niliyomwahidi Abrahamu, Isaki na Yakobo kwa kiapo, nikisema, ‘Nitawapa wazao wenu nchi hii.’
And the Lord spak to Moyses, and seide, Go and stie fro this place, thou, and the puple, whom thou leddist out of the lond of Egipt, in to the lond, which Y haue swore to Abraham, and to Ysaac, and to Jacob, `and Y seide, Y schal yyue it to thi seed.
2 Nitamtuma malaika mbele yenu, naye atawafukuza Wakanaani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
And Y schal sende thi bifore goere an aungel, that Y caste out Cananey, and Amorei, and Ethei, and Ferezei, and Euey, and Jebusey;
3 Pandeni mwende katika nchi itiririkayo maziwa na asali. Lakini mimi sitakwenda pamoja nanyi, kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu, nisije nikawaangamiza njiani.”
and that thou entre in to the lond flowynge with mylk and hony; for Y schal not stye with thee, for `thou art a puple of hard nol, lest perauenture Y leese thee in the weie.
4 Watu waliposikia habari hizo za huzuni, wakaanza kuomboleza wala hakuna mtu aliyevaa mapambo yoyote.
The puple herde this worste word, and morenyde, and noon was clothid with his ournyng bi custom.
5 Kwa kuwa Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu. Kama ningefuatana nanyi hata kwa muda mfupi, ningewaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu, nami nitaamua nitakalowatendea.’”
And the Lord seide to Moises, Spek thou to the sones of Israel, Thou art a puple of hard nol; onys Y schal stie in the myddis of thee, and Y schal do awey thee; riyt now putte awei thin ournyng, that Y wite, what Y schal do to thee.
6 Hivyo Waisraeli wakavua mapambo yao katika Mlima wa Horebu.
Therfor the sones of Israel puttiden awey her ournyng fro the hil of Oreb.
7 Basi Mose alikuwa na desturi ya kuchukua hema na kuliweka wakfu nje ya kambi umbali kiasi, akaliita “Hema la Kukutania.” Kila aliyekuwa akiulizia shauri kwa Bwana, angelikwenda katika Hema la Kukutania nje ya kambi.
And Moises took the tabernacle, and settide fer with out the castels, and he clepide the name therof the tabernacle of boond of pees. And al the puple that hadde ony questioun, yede out to the tabernacle of boond of pees, with out the castels.
8 Wakati wowote Mose alipokwenda kwenye Hema, watu wote waliinuka na kusimama kwenye maingilio ya mahema yao, wakimwangalia Mose mpaka aingie kwenye Hema.
And whanne Moises yede out to the tabernacle, al the puple roos, and ech man stood in the dore of his tente, and thei bihelden `the bak of Moises, til he entride in to the tente.
9 Kila mara Mose alipoingia ndani ya hema, nguzo ya wingu ingeshuka chini na kukaa kwenye ingilio, wakati Mungu akizungumza na Mose.
Sotheli whanne he entride in to the tabernacle of boond of pees, a piler of cloude cam doun, and stood at the dore; and the Lord spak with Moises,
10 Kila mara watu walipoona hiyo nguzo ya wingu ikiwa imesimama kwenye ingilio la hema, wote walisimama wakaabudu, kila mmoja kwenye ingilio la hema lake.
while alle men sien that the piler of cloude stood at the `dore of tabernacle; and thei stoden, and worschipiden bi the dores of her tabernaclis.
11 Bwana angezungumza na Mose uso kwa uso, kama vile mtu azungumzavyo na rafiki yake. Kisha Mose angerudi kambini, lakini msaidizi wake kijana Yoshua mwana wa Nuni hakuondoka mle Hemani.
Forsothe the Lord spak to Moises face to face, as a man is wont to speke to his freend; and whanne he turnede ayen in to `the castels, Josue, his mynystre, the sone of Nun, a child, yede not awey fro the tabernacle.
12 Mose akamwambia Bwana, “Umekuwa ukiniambia, ‘Ongoza watu hawa,’ lakini hujanifahamisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Umesema, ‘Ninakujua wewe kwa jina lako, nawe umepata kibali mbele zangu.’
Forsothe Moises seide to the Lord, Thou comaundist, that Y lede out this puple, and thou `schewist not to me, whom thou schalt sende with me, `most sithen thou seidist, Y knewe thee bi name, and thou hast founde grace bifore me.
13 Ikiwa umependezwa nami, nifundishe njia zako ili nipate kukujua, nami nizidi kupata kibali mbele zako. Kumbuka kuwa taifa hili ni watu wako.”
Therfore if Y haue founde grace in thi siyt, schewe thi face to me, that Y knowe thee, and fynde grace bifor thin iyen; biholde thi puple, and this folk.
14 Bwana akajibu, “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”
And God seide, My face schal go bifor thee, and Y schal yyue reste to thee.
15 Kisha Mose akamwambia, “Kama Uso wako hauendi pamoja nasi, usituondoe hapa.
And Moises seide, If thi silf schalt not go bifore, `lede not vs out of this place;
16 Mtu yeyote atajuaje kuwa mimi pamoja na watu wako tumepata kibali mbele zako, usipokwenda pamoja nasi? Ni nini kingine kitakachoweza kututofautisha mimi na watu wako miongoni mwa watu wengine wote walio katika uso wa dunia?”
for in what thing moun we wite, Y and thi puple, that we han founde grace in thi siyt, if thou schalt not go with vs, that we be glorified of alle puplis that dwellen on erthe?
17 Bwana akamwambia Mose, “Nitakufanyia jambo lile uliloomba, kwa sababu ninapendezwa nawe, nami ninakujua kwa jina lako.”
Forsothe the Lord seide to Moises, Y schal do also this word, which thou hast spoke; for thou hast founde grace bifor me, and Y knewe thi silf bi name.
18 Kisha Mose akasema, “Basi nionyeshe utukufu wako.”
And Moises seide, Schewe thou thi glorie to me.
19 Ndipo Bwana akasema, “Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza Jina langu, Bwana, mbele ya uso wako. Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
God answeride, Y schal schewe al good to thee, and Y schal clepe in the `name of the Lord bifor thee, and Y schal do merci to whom Y wole, and Y schal be merciful on whom it plesith to me.
20 Lakini Mungu akasema, “Hutaweza kuuona uso wangu, kwa kuwa hakuna mtu yeyote awezaye kuniona akaishi.”
And eft God seide, Thou maist not se my face, for a man schal not se me, and schal lyue.
21 Kisha Bwana akasema, “Kuna mahali karibu nami ambapo unaweza kusimama juu ya mwamba.
And eft God seide, A place is anentis me, and thou schalt stonde on a stoon;
22 Utukufu wangu unapopita, nitakuweka gengeni kwenye mwamba na kukufunika kwa mkono wangu mpaka nitakapokwisha kupita.
and whanne my glorie schal passe, Y schal sette thee in the hoole of the stoon, and Y schal kyuere with my riyt hond, til Y passe; and Y schal take awey myn hond,
23 Kisha nitaondoa mkono wangu nawe utaona mgongo wangu; lakini kamwe uso wangu hautaonekana.”
and thou schalt se myn hyndrere partis, forsothe thou mayst not se my face.

< Kutoka 33 >