< Kutoka 32 >

1 Watu walipoona kuwa Mose amekawia sana kushuka kutoka mlimani, walimkusanyikia Aroni na kumwambia, “Njoo, tutengenezee miungu itakayotutangulia. Kwa maana huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatujui jambo lililompata.”
Cependant le peuple voyant le retard que mettait Moïse à descendre de la montagne, et s’étant assemblé contre Aaron, dit: Lève-toi, fais-nous des dieux qui nous précèdent; car pour Moïse, cet homme qui nous a retirés de la terre d’Egypte, nous ignorons ce qui lui est arrivé.
2 Aroni akawajibu, “Vueni vipuli vya dhahabu ambavyo wake zenu, wana wenu na binti zenu wamevaa, mkaniletee.”
Et Aaron leur répondit: Otez les pendants d’or des oreilles de vos femmes, de vos fils et de vos filles, et apportez-les-moi.
3 Kwa hiyo watu wote wakavua vipuli vyao, wakavileta kwa Aroni.
Et le peuple fit ce qu’il avait commandé, portant les pendants d’oreilles à Aaron.
4 Akavichukua vile vitu walivyomkabidhi, akavifanyiza kwa kusubu sanamu yenye umbo la ndama, akaichonga kwa kutumia chombo. Kisha wakasema, “Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
Lorsque celui-ci les eut reçus, il les jeta en fonte, et il en fit un veau de fonte: alors ils dirent: Voici tes dieux, ô Israël, qui t’ont retiré de la terre d’Egypte.
5 Aroni alipoona hili, akajenga madhabahu mbele ya yule ndama na kutangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa Bwana.”
Ce qu’ayant vu Aaron, il bâtit un autel devant le veau, et il cria par la voix d’un héraut: Demain est une solennité du Seigneur.
6 Kwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha katika sherehe.
Et, se levant le matin, ils offrirent des holocaustes et des hosties pacifiques, et le peuple s’assit pour manger et pour boire, et ils se levèrent pour jouer.
7 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Shuka, kwa sababu watu wako, uliowatoa Misri, wamepotoka.
Mais le Seigneur parla à Moïse, disant: Va, descends: il a péché, ton peuple que tu as retiré de la terre d’Egypte.
8 Wamekuwa wepesi kugeuka na kuacha niliyowaamuru, na wamejitengenezea sanamu ya kuyeyusha yenye umbo la ndama. Wameisujudia na kuitolea dhabihu, nao wamesema, ‘Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli iliyokupandisha kutoka Misri.’”
Ils se sont bientôt écartés de la voie que tu leur as montrée: ils se sont fait un veau de fonte, et ils l’ont adoré; puis lui immolant des hosties, ils ont dit: Voici tes dieux, ô Israël, qui t’ont retiré de la terre d’Egypte.
9 Bwana akamwambia Mose, “Nimeona watu hawa, nao ni watu wenye shingo ngumu.
Et de nouveau le Seigneur dit à Moïse; Je vois que ce peuple est d’un cou roide;
10 Sasa niache ili hasira yangu ipate kuwaka dhidi yao, nami nipate kuwaangamiza. Kisha nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa.”
Laisse-moi, afin que ma fureur s’irrite contre eux, et que je les extermine; et je te ferai chef d’une grande nation.
11 Lakini Mose akamsihi Bwana Mungu wake, akasema, “Ee Bwana, kwa nini hasira yako iwake dhidi ya watu wako, wale uliowatoa Misri kwa uweza mkuu na mkono wenye nguvu?
Mais Moïse priait le Seigneur son Dieu, disant: Pourquoi, Seigneur, votre fureur s’indigne-telle contre votre peuple que vous avez retiré de la terre d’Egypte, avec une grande puissance, et une main forte?
12 Kwa nini Wamisri waseme, ‘Ni kwa nia mbaya aliwatoa Misri, ili awaue milimani na kuwafuta usoni mwa dunia’? Achilia mbali hasira yako kali, waonee huruma na usilete maafa juu ya watu wako.
Que les Egyptiens, je vous prie, ne disent pas: C’est par ruse qu’il les a retirés, afin de les tuer sur les montagnes, et les exterminer de la terre: que votre colère s’apaise et laissez-vous fléchir sur la méchanceté de votre peuple.
13 Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaki na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe: ‘Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa wazao wako nchi hii yote ambayo niliwaahidia, nayo itakuwa urithi wao milele.’”
Souvenez-vous d’Abraham, d’Isaac et d’Israël vos serviteurs auxquels vous avez juré par vous-même, disant: Je multiplierai votre postérité comme les étoiles du ciel; et toute cette terre dont je vous ai parlé, je la donnerai à votre postérité, et vous la posséderez toujours.
14 Kisha Bwana akawaonea huruma, wala hakuleta juu ya watu wake maafa aliyokuwa amekusudia.
Et le Seigneur s’apaisa, et il ne fit pas à son peuple le mal qu’il avait dit.
15 Mose akageuka, akashuka kutoka mlimani akiwa na vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake. Vilikuwa vimeandikwa pande zote mbili, mbele na nyuma.
Ainsi, Moïse retourna de la montagne, portant en sa main les deux tables du témoignage écrites des deux côtés,
16 Vibao hivyo vilikuwa kazi ya Mungu; maandishi yalikuwa mwandiko wa Mungu, yaliyochorwa kama muhuri juu ya vibao.
Et faites par l’œuvre de Dieu; l’écriture aussi, gravée sur les tables, était de Dieu.
17 Yoshua aliposikia sauti za watu wakipiga kelele, akamwambia Mose, “Kuna sauti ya vita kambini.”
Or, Josué entendant le tumulte du peuple qui vociférait, dit à Moïse: On entend des cris de combat dans le camp.
18 Mose akajibu: “Si sauti ya ushindi, wala si sauti ya kushindwa; ni sauti ya kuimba ninayosikia.”
Moïse répondit: Ce n’est point là le cri de ceux qui s’exhortent au combat, ni les vociférations de ceux qui poussent leurs ennemis à la fuite; mais c’est la voix de gens qui chantent, que moi j’entends.
19 Mose alipoikaribia kambi na kuona yule ndama na ile michezo, hasira yake ikawaka, akatupa vile vibao vilivyokuwa mikononi mwake, akavipasua vipande vipande pale chini ya mlima.
Et lorsqu’il se fut approché du camp, il vit le veau et les danses; alors très irrité, il jeta les tables qu’il tenait à la main, et les rompit au pied de la montagne;
20 Kisha akamchukua yule ndama waliokuwa wamemtengeneza na kumchoma kwenye moto, kisha akamsaga kuwa unga, akanyunyiza kwenye maji na kuwafanya Waisraeli wanywe.
Puis saisissant le veau qu’ils avaient fait, il le brûla, et le brisa jusqu’à le réduire en poudre, qu’il répandit dans l’eau, et il donna de cette poudre à boire aux enfants d’Israël.
21 Mose akamwambia Aroni, “Watu hawa walikufanyia nini, hata ukawaongoza kufanya dhambi kubwa hivyo?”
Il dit ensuite à Aaron: Que t’a fait ce peuple, pour que tu attirasses sur lui un très grand péché?
22 Aroni akamwambia, “Usikasirike bwana wangu. Unajua jinsi watu hawa walivyo tayari kwa maovu.
Aaron lui répondit: Que mon Seigneur ne soit pas indigné; car tu connais ce peuple; tu sais qu’il est porté au mal:
23 Wao waliniambia, ‘Tufanyie miungu itakayotuongoza. Kwa kuwa huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatufahamu yaliyompata.’
Ils m’ont dit: Fais-nous des dieux qui nous précèdent; car pour ce Moïse qui nous a retirés de la terre d’Egypte, nous ne savons ce qui lui est arrivé.
24 Kwa hiyo nikawaambia, ‘Yeyote aliye na kito chochote cha dhahabu avue.’ Kisha wakanipa hiyo dhahabu, nami nikaitupa motoni, akatokea huyu ndama!”
Moi, je leur ai dit: Qui de vous a de l’or? Ils l’ont apporté et me l’ont donné; et je l’ai jeté dans le feu, et il en est sorti ce veau.
25 Mose akaona kuwa watu wameasi, kwa kuwa Aroni alikuwa amewaacha waasi, na hivyo kuwa kichekesho kwa adui zao.
Moïse voyant donc que le peuple avait été mis nu (car Aaron l’avait dépouillé pour une ignominie d’ordure, et l’avait mis nu au milieu de ses ennemis),
26 Kwa hiyo Mose akasimama kwenye ingilio la kambi, akasema, “Yeyote aliye upande wa Bwana, aje upande wangu.” Walawi wote wakamjia.
Et se tenant à la porte du camp, dit: Si quelqu’un est au Seigneur, qu’il se joigne à moi. Et tous les enfants de Lévi se réunirent auprès de lui;
27 Ndipo alipowaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Kila mmoja wenu ajifunge upanga wake kiunoni aende huku na huko kambi yote mwisho hadi mwisho mwingine, kila mmoja amuue ndugu yake, na rafiki yake na jirani yake.’”
Il leur dit: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d’Israël: Que chaque homme mette un glaive sur sa cuisse: allez et revenez d’une porte à l’autre au travers du camp, et que chacun lue son frère, son ami, et celui qui lui est le plus proche.
28 Walawi wakafanya kama Mose alivyoamuru, siku ile wakafa watu wapatao 3,000.
Et les fils de Lévi firent selon la parole de Moïse, et il tomba en ce jour-là environ vingt-trois mille hommes.
29 Kisha Mose akasema, “Leo mmewekwa wakfu kwa Bwana, kwa kuwa mlikuwa kinyume na wana wenu wenyewe na ndugu zenu, naye Mungu amewabariki leo.”
Alors Moïse dit: Vous avez consacré aujourd’hui vos mains au Seigneur, chacun sur son fils et sur son frère, afin que vous soit donnée une bénédiction.
30 Siku iliyofuata Mose akawaambia watu, “Mmefanya dhambi kubwa. Lakini sasa nitapanda juu kwa Bwana, labda nitaweza kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
Mais le jour suivant arrivé, Moïse parla au peuple, disant: Vous avez commis un très grand péché; je monterai vers le Seigneur, pour voir si je pourrai en quelque manière détourner le châtiment de votre crime.
31 Hivyo Mose akarudi kwa Bwana na kumwambia, “Lo! Hawa watu wamefanya dhambi kubwa namna gani! Wamejitengenezea miungu ya dhahabu.
Et étant retourné vers le Seigneur, il dit: Je vous conjure, ce peuple a commis un très grand péché, ils se sont fait des dieux d’or: ou remettez-leur cette faute,
32 Lakini sasa nakusihi, wasamehe dhambi yao; lakini kama sivyo, basi nifute kutoka kwenye kitabu ulichoandika.”
Ou, si vous ne le faites pas, effacez-moi de votre livre que vous avez écrit.
33 Bwana akamjibu Mose, “Yeyote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta kutoka kwenye kitabu changu.
Le Seigneur lui répondit: Celui qui aura péché contre moi, je l’effacerai de mon livre:
34 Sasa nenda, uongoze hao watu mpaka mahali nilipokuambia, naye malaika wangu atakutangulia. Pamoja na hayo, wakati utakapofika wa mimi kuwaadhibu, nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi yao.”
Mais toi, va, et conduis ce peuple où je t’ai dit: mon ange te précédera. Pour moi, au jour de la vengeance, je visiterai ce péché qu’ils ont commis.
35 Ndipo Bwana akawapiga watu kwa ugonjwa wa tauni kwa sababu ya yale waliyoyafanya kwa ndama yule ambaye alitengenezwa na Aroni.
Le Seigneur frappa donc le peuple pour le crime du veau qu’avait fait Aaron.

< Kutoka 32 >