< Kutoka 31 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Tazama, nimemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
“Behold, I have called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, from the tribe of Judah,
3 nami nimemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
and I have filled him with the Spirit of God, with wisdom, and understanding, and knowledge in every craft,
4 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
in order to design whatever must be fabricated from gold, and silver, and brass,
5 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi.
from marble, and precious stones, and various woods.
6 Tena nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, ili kumsaidia. Pia mafundi wote nimewapa ustadi wa kutengeneza kila kitu nilichokuamuru wewe:
And I have given to him, as his associate, Oholiab the son of Ahisamach, from the tribe of Dan. And I have placed wisdom in the heart of every artisan, so that they may make everything as I have instructed you:
7 Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda pamoja na kiti cha rehema juu yake, pia na vifaa vyote vya kwenye hema,
the tabernacle of the covenant, and the ark of the testimony, and the propitiatory which is over it, and all the vessels of the tabernacle,
8 meza na vifaa vyake, kinara cha taa cha dhahabu safi na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,
and the table and its vessels, the most pure lampstand with its vessels, and the altars of incense
9 madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, sinia na kinara chake,
and of holocaust and all their vessels, the washtub with its base,
10 pamoja na mavazi matakatifu yaliyofumwa ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe wakati wanahudumu katika kazi ya ukuhani,
the holy vestments for the ministry of Aaron the priest, and for his sons, so that they may execute their office of sacred rites,
11 pia mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri kwa ajili ya Mahali Patakatifu. Watavitengeneza sawasawa kama vile nilivyokuagiza wewe.”
the oil of unction, and the incense of aromatics in the Sanctuary. All the things that I have instructed you, they shall make.”
12 Kisha Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
13 “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni lazima mzishike Sabato zangu. Hii itakuwa ni ishara kati yangu na ninyi kwa ajili ya vizazi vijavyo, ili mpate kujua kwamba Mimi Ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.
“Speak to the sons of Israel, and you shall say to them: See that you keep my Sabbath. For it is a sign between me and you among your generations, so that you may know that I am the Lord, who sanctifies you.
14 “‘Mtaishika Sabato, kwa sababu ni takatifu kwenu. Yeyote atakayeinajisi lazima auawe, yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima akafie mbali na watu wake.
Keep my Sabbath, for it is holy to you. Whoever will have polluted it, shall die a death. Whoever will have done any work in it, his soul shall perish from the midst of his people.
15 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba ni Sabato ya kupumzika, takatifu kwa Bwana. Yeyote afanyaye kazi yoyote siku ya Sabato ni lazima auawe.
For six days you shall do work. On the seventh day, it is the Sabbath, a rest sanctified by the Lord. All who will have done work on this day shall die.
16 Waisraeli wataishika Sabato, kuiadhimisha kwa vizazi vijavyo kuwa Agano la milele.
Let the sons of Israel keep the Sabbath, and let them celebrate it throughout their generations. It is an everlasting covenant
17 Itakuwa ishara kati yangu na Waisraeli milele, kwa kuwa kwa muda wa siku sita Bwana aliumba mbingu na dunia, na siku ya saba akaacha kufanya kazi, akapumzika.’”
between me and the sons of Israel, and a perpetual sign. For in six days the Lord made heaven and earth, and in the seventh he ceased from work.”
18 Bwana alipomaliza kusema na Mose juu ya Mlima Sinai, Mungu akampa vile vibao viwili vya Ushuhuda, vibao vya mawe vilivyoandikwa kwa kidole cha Mungu.
And the Lord, having completed speaking in this way on Mount Sinai, gave to Moses two stone tablets of testimony, written with the finger of God.