< Kutoka 30 >
1 “Tengeneza madhabahu kwa mbao za mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba.
Andrafito kitrely, toem-pañembohañe; mendoraveñe ty itsenea’o aze.
2 Madhabahu hayo yawe mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zitakuwa kitu kimoja nayo.
Ho kiho raike ty andava’e naho kiho raike ty ampohe’e, ho efa-mira, kiho roe ty haabo’e vaho raik’ ama’e o tsifa’eo.
3 Funika hayo madhabahu juu na pande zote na pia pembe zake kwa dhahabu safi, na uifanyizie ukingo wa dhahabu kuizunguka.
Ipakoro am-bolamena ki’e: ty ambone’e naho o ila’e mañarikatok’ azeo naho o tsifa’eo vaho itefeo soñi’e volamena hamahetse aze.
4 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, ziwe mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko itumikayo kuibebea madhabahu.
Anefeo ravake volamena roe ambane’ i soñi’ey, le añ’ila’e roe ty itsenea’o iareo ho fitanañe o bao-pitakonañeo.
5 Tengeneza mipiko kwa miti ya mshita na uifunike kwa dhahabu.
Rafito ami’ty mendoraveñe o bao’eo le ipakoro volamena;
6 Weka hayo madhabahu mbele ya lile pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, lililo mbele ya kiti cha rehema kilicho juu ya Sanduku la Ushuhuda, mahali ambapo nitakutana nawe.
le apoho aolo’ i lamba-fañefe’ i vatam-pañinay aolo’ i toem-pijebañañe fikape’ i fañinay, amy hifañaoñako ama’oiy.
7 “Itampasa Aroni kufukiza uvumba wenye harufu nzuri juu ya madhabahu kila siku asubuhi wakati anapowasha zile taa.
Hañoro emboke mañitse ama’e boa-maraindray t’i Aharone; ie mañalahala jiro ro hañemboke ama’e.
8 Itampasa afukize uvumba tena wakati anapowasha taa wakati wa machweo ili uvumba ufukizwe daima mbele za Bwana kwa vizazi vijavyo.
Hañembok’ ama’e ka t’i Aharone amy fameloman-jiro harivay, le ho nainai’e añatrefa’ Iehovà amo hene tarira’ areo mifandimbeo i embokey.
9 Usifukize uvumba mwingine wowote juu ya madhabahu haya au sadaka nyingine yoyote ya kuteketezwa wala sadaka ya nafaka, wala usimimine sadaka ya kinywaji juu yake.
Ko mañenga emboke ila’e ama’e, ndra enga horoañe, he mahakama, le ko añiliña’o engan-drano.
10 Mara moja kwa mwaka Aroni atafanya upatanisho juu ya pembe za hayo madhabahu. Upatanisho huu wa mwaka lazima ufanywe kwa damu ya sadaka ya upatanisho kwa ajili ya dhambi kwa vizazi vijavyo. Ni takatifu sana kwa Bwana.”
Le hanao fijebańañe amo tsifa’eo boa-taoñe t’i Aharone ami’ty lion-tsoron-kakeo-pijebañañe, indraike boa-taoñe amo tarira’ areo mifandimbe iabio, t’ie ijebañañe. Miava-do’e amy Iehovà izay.
11 Naye Bwana akamwambia Mose,
Le nanao ty hoe amy Mosè t’Iehovà:
12 “Utakapowahesabu Waisraeli, kila mmoja lazima alipe kwa Bwana fidia kwa ajili ya nafsi yake wakati wa kuhesabiwa kwake. Ndipo hakutakuwa na pigo juu yao unapowahesabu.
Ihe mamolily o ana-dahi’ Israeleo ami’ty ia’ iareo, le songa hanolotse ty vilin’ai’e amy Iehovà amy fañiahañey, tsy mone hisilofañ’ angorosy ty amy famoliliañey.
13 Kila mmoja anayekwenda upande wa wale waliokwisha hesabiwa atatoa nusu shekeli, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini. Hii nusu shekeli ni sadaka kwa Bwana.
Sindre hanolotse zao te iaheñe: ty vakin-tsekele amy sekelen-toe-mivakeiy (roapolo gerà ty sekele raike). Ho banabana am’ Iehovà i vakin-tsekeley.
14 Wote wale wanaovuka, wenye umri wa miaka ishirini au zaidi, watatoa sadaka kwa Bwana.
Ze hene niaheñe roapolo taoñe mañambone ro hañenga am’ Iehovà.
15 Matajiri hawatalipa zaidi ya nusu shekeli, nao maskini hawatatoa pungufu wakati mnatoa sadaka kwa Bwana kwa kufanya upatanisho wa nafsi zenu.
Ie mañenga i vilin’ aiñey am’ Iehovà, le tsy hanolotse maro ty mpañaleale vaho tsy hanolotse ambane’ i vakin-tsekeley ty rarake.
16 Utapokea fedha ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli na uzitumie kwa ajili ya huduma ya Hema la Kukutania. Itakuwa ni ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”
Ho rambese’o amo ana’ Israeleo i bogadim-bilin’ aiñey vaho havì’o ho fitoroñañe i kibohom-pamantañañey; le ho tiahy amo ana’ Israeleo añatrefa’ Iehovà, hijebañañe anahareo.
17 Kisha Bwana akamwambia Mose,
Le nanao ty hoe amy Mosè t’Iehovà,
18 “Tengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kwa ajili ya kunawia. Liweke kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, kisha uweke maji ndani yake.
Anefeo fanasàñe torisìke reke-poto’e torisìke, ho fisasàñe, le apoho añivo’ i kibohom-pamantañañey naho i kitreliy izay vaho añiliño rano,
19 Aroni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwa maji yatokayo katika hilo sinia.
le boak’ ama’e ty hanasà’ i Aharone miroanake fitàñe naho fandia.
20 Wakati wowote wanapoingia katika Hema la Kukutania, watanawa kwa maji ili kwamba wasije wakafa. Pia, wanapokaribia madhabahu ili kuhudumu kwa kuleta sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto,
Ie mimoak’ amy kibohom-pamantañañey ndra mañarine i kitreliy hitoroñe, hañoro enga am’ Iehovà, ro hisasa an-drano hey tsy mone hikenkañe;
21 watanawa mikono na miguu yao ili kwamba wasije wakafa. Hii itakuwa ni amri ya kudumu kwa ajili ya Aroni na wazao wake kwa vizazi vijavyo.”
hanasa fitàñe naho fandia tsy mone hivetrake. Ho fañè tsy modo ho a iareo—ho aze naho o hene tarira’e mifandimbeo.
22 Kisha Bwana akamwambia Mose,
Nitsara amy Mosè t’Iehovà, nanao ty hoe:
23 “Chukua vikolezi bora vifuatavyo: shekeli 500 za manemane ya maji, shekeli 250 za mdalasini wenye harufu nzuri, shekeli 250 za miwa yenye harufu nzuri,
Rambeso ty emboke soa jinoboñe: ty ron-drame limanjato naho ty kanely mañitse vaki’ izay: roan-jato tsy limampolo, le varemañitse roan-jato tsy limampolo,
24 shekeli 500 za aina nyingine ya mdalasini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, pia hini ya mafuta ya zeituni.
le ty roi-mañitse limanjato amy sekelen-toe-miavakey vaho menak’ olive hine raike.
25 Vitengeneze vikolezi hivi kuwa mafuta matakatifu ya upako yenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Yatakuwa mafuta matakatifu ya upako.
Le ano menake fañorizañe miavake i raha rey, raha mañitse aharo an-tsata’ o mpanao tsòtseo, ho mena-pañorizañe miavake.
26 Kisha yatumie kupaka hilo Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda,
Ie ty hañoriza’o i kibohom-pamantañañey naho i vatam-pañinay,
27 meza na vifaa vyake vyote, kinara cha taa na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,
i rairaiy naho ze hene fanake naho i fitàn-jiroy naho o harao’eo vaho i kitrelim-pañoroañ’ embokey,
28 madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote na sinia pamoja na kitako chake.
ty kitrelim-pisoroñañe naho o harao’e iabio vaho i fanasàñey rekets’ i foto’ey.
29 Utaviweka wakfu ili viwe vitakatifu sana na kila kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
Atokano ho loho masiñ’ irezay; miavake ze mitsapa aze.
30 “Mtie Aroni na wanawe mafuta na uwaweke wakfu ili waweze kunitumikia katika kazi ya ukuhani.
Le horiza’o ty Aharone naho o ana’eo hamìha’o hitoroñe ahy ho mpisoroko.
31 Waambie Waisraeli, ‘Haya yatakuwa mafuta matakatifu yangu ya upako kwa vizazi vijavyo.
Le ty hoe ty hatao’o amo ana’ Israeleo: Itoy ty mena-pañorizañe miavake amako amo hene tarira’ areo mifandimbeo.
32 Usiyamimine juu ya miili ya wanadamu wala usitengeneze mafuta ya aina nyingine kwa utaratibu huu. Ni mafuta matakatifu na ni lazima myaone kuwa ni matakatifu.
Tsy ailiñe an-tsandri’ ondaty, le tsy tsikombeñe ty fampitraofañe aze, fa miavake, vaho havahe’ areo.
33 Mtu yeyote atakayetengeneza manukato kama hayo na yeyote atakayeyamimina juu ya mtu yeyote ambaye si kuhani atakatiliwa mbali na watu wake.’”
Ze mampilaro manahak’ aze, ndra mañiliñ’ aze am’ondaty ila’e, ro haitoañe am’ondatio.
34 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Chukua vikolezi vyenye harufu nzuri vifuatavyo: natafi, shekelethi, kelbena na uvumba safi vyote vikiwa na vipimo sawa,
Aa hoe t’Iehovà amy Mosè: Rambeso o emboke mañitse zao: sike-mañitse naho sabiba naho taven-tsike; naho tsotse-foty ki’e, i raha mañitse rezay; le ampimirao lanja.
35 pia tengeneza mchanganyiko wa uvumba wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Utiwe chumvi ili upate kuwa safi na mtakatifu.
Le mitsenea emboke, am-pilaroañe, satam-panao emboke, siraeñe, malio naho miavake.
36 Saga baadhi yake kuwa unga na uweke mbele ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, mahali ambapo nitakutana nawe. Itakuwa takatifu sana kwenu.
Lisano ho bo’e ty ila’e, le ano aolo’ i fañinay an-kibohom-pamantañañ’ ao ty ila’e, amy hifañaoñako ama’oy, loho miavake ama’ areo izay.
37 Msitengeneze uvumba mwingine wowote wa namna hii kwa ajili yenu wenyewe; uoneni kuwa ni mtakatifu kwa Bwana.
Le i emboke tsenè’oy, tsy hanoe’ areo ho am-batañe amy filaroa’ey, fa miavake am’ Iehovà ho anahareo izay.
38 Yeyote atakayetengeneza uvumba kama huu ili kufurahia harufu yake nzuri lazima akatiliwe mbali na watu wake.”
Haitoañe am’ondati’eo ze mitsene ty hambañ’ ama’e hañantsoña’e.