< Kutoka 3 >

1 Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Forsothe Moises kepte the scheep of Jetro, `his wyues fadir, preest of Madian; and whanne he hadde dryue the floc to the ynnere partis of deseert, he cam to Oreb, the hil of God.
2 Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei.
Forsothe the Lord apperide to hym in the flawme of fier fro the myddis of the buysch, and he seiy that the buysch brente, and was not forbrent.
3 Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”
Therfor Moyses seide, Y schal go and schal se this greet siyt, whi the buysch is not forbrent.
4 Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!” Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”
Sotheli the Lord seiy that Moises yede to se, and he clepide Moises fro the myddis of the buysch, and seide, Moyses! Moises! Which answeride, Y am present.
5 Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.”
And the Lord seide, Neiye thou not hidur, but vnbynde thou the scho of thi feet, for the place in which thou stondist is hooli lond.
6 Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.
And the Lord seide, Y am God of thi fadir, God of Abraham, and God of Isaac, and God of Jacob. Moises hidde his face, for he durste not biholde ayens God.
7 Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao.
To whom the Lord seide, Y seiy the affliccion of my puple in Egipt, and Y herde the cry therof, for the hardnesse of hem that ben souereyns of werkis.
8 Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
And Y knew the sorewe of the puple, and Y cam down to delyuere it fro the hondis of Egipcians, and lede out of that lond in to a good lond and brood, into a lond that flowith with milk and hony, to the places of Cananey, and of Ethei, of Amorrey, and of Feresei, of Euey, and of Jebusei.
9 Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.
Therfor the cry of the sones of Israel cam to me, and Y seiy the turment of hem, bi which thei ben oppressid of Egipcians.
10 Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”
But come thou, I schal sende thee to Farao, that thou lede out my puple, the sones of Israel, fro Egipt.
11 Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”
And Moises seide to hym, Who am Y, that Y go to Farao, and lede out the sones of Israel fro Egipt?
12 Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”
And the Lord seide to Moises, Y schal be with thee, and thou schalt haue this signe, that Y haue sent thee, whanne thou hast led out my puple fro Egipt, thou schalt offre to God on this hil.
13 Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”
Moises seide to God, Lo! Y schal go to the sones of Israel, and Y schal seie to hem, God of youre fadris sente me to you; if thei schulen seie to me, what is his name, what schal Y seie to hem?
14 Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’”
The Lord seide to Moises, Y am that am. The Lord seide, Thus thou schalt seie to the sones of Israel, He that is sente me to you.
15 Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
And eft God seide to Moises, Thou schalt seie these thingis to the sones of Israel, The Lord God of youre fadris, God of Abraham, and God of Isaac, and God of Jacob, sente me to you; this name is to me with outen ende, and this is my memorial in generacioun and in to generacioun.
16 “Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri.
Go thou, gadere thou the eldere men, that is, iugis, of Israel, and thou schalt seie to hem, The Lord God of youre fadris apperide to me, God of Abraham, and God of Ysaac, and God of Jacob, and seide, Y visitynge haue visitid you, and Y seiy alle thingis that bifelden to you in Egipt;
17 Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’
and Y seide, that Y lede out you fro the affliccioun of Egipt in to the lond of Cananey, and of Ethei, and of Amorrei, and of Ferezei and of Euei, and of Jebusei, to the lond flowynge with mylk and hony.
18 “Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’
And thei schulen here thi vois; and thou schalt entre, and the eldere men of Israel to the kyng of Egipt, and thou schalt seie to hym, The Lord God of Ebrews clepide vs; we schulen go the weie of thre daies in to wildirnesse, that we offre to oure Lord God.
19 Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe.
But Y woot, that the kyng of Egipt schal not delyuere you that ye go, but bi strong hond;
20 Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.
for Y schal holde forthe myn hond, and I schal smyte Egipt in alle my marueils, whiche Y schal do in the myddis of hem; aftir these thingis he schal delyuere you.
21 “Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu.
And Y schal yyue grace to this puple bifore Egipcians, and whanne ye schulen go out, ye schulen not go out voide;
22 Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”
but a womman schal axe of hir neiyboresse and of her hoosteesse siluerne vesselis, and goldun, and clothis, and ye schulen putte tho on youre sones and douytris, and ye schulen make nakid Egipt.

< Kutoka 3 >