< Kutoka 3 >
1 Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Mojsije pasao ovce svoga tasta Jitra, midjanskoga svećenika. Goneći tako stado po pustari, dođe do Horeba, brda Božjega.
2 Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei.
Anđeo mu se Jahvin ukaže u rasplamtjeloj vatri iz jednog grma. On se zagleda: grm sav u plamenu, a ipak ne izgara.
3 Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”
“Hajde da priđem, “reče Mojsije, “i promotrim ovaj čudni prizor: zašto grm ne sagorijeva.”
4 Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!” Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”
Kad je Jahve vidio kako prilazi da razmotri, iz grma ga Bog zovne: “Mojsije! Mojsije!” “Evo me!” - javi se.
5 Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.”
“Ne prilazi ovamo!” - reče. “Izuj obuću s nogu! Jer mjesto na kojem stojiš sveto je tlo.
6 Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.
Ja sam”, nastavi, “Bog tvoga oca; Bog Abrahamov, Bog Izakov, Bog Jakovljev.” Mojsije zakloni lice: bojao se u Boga gledati.
7 Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao.
“Vidio sam jade svoga naroda u Egiptu”, nastavi Jahve, “i čuo mu tužbu na tlačitelje njegove. Znane su mi muke njegove.
8 Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Zato sam sišao da ga izbavim iz šaka egipatskih i odvedem ga iz te zemlje u dobru i prostranu zemlju - u zemlju kojom teče med i mlijeko: u postojbinu Kanaanaca, Hetita, Amorejaca, Perižana, Hivijaca i Jebusejaca.
9 Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.
Vapaji sinova Izraelovih dopriješe do mene. I sam vidjeh kako ih Egipćani tlače.
10 Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”
Zato, hajde! Ja te šaljem faraonu da izbaviš narod moj, Izraelce, iz Egipta.”
11 Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”
“Tko sam ja da se uputim faraonu”, odgovori Mojsije Bogu, “i izvedem Izraelce iz Egipta!”
12 Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”
“Ja ću biti s tobom”, nastavi. “I ovo će ti biti znak da sam te ja poslao: kad izvedeš narod iz Egipta, Bogu ćete iskazati štovanje na ovome brdu.”
13 Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”
Nato Mojsije reče Bogu: “Ako dođem k Izraelcima pa im kažem: 'Bog otaca vaših poslao me k vama', i oni me zapitaju: 'Kako mu je ime?' - što ću im odgovoriti?”
14 Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’”
“Ja sam koji jesam”, reče Bog Mojsiju. Onda nastavi: “Ovako kaži Izraelcima: 'Ja jesam' posla me k vama.”
15 Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
Dalje je Bog Mojsiju rekao: “Kaži Izraelcima ovako: 'Jahve, Bog vaših otaca, Bog Abrahamov, Bog Izakov i Bog Jakovljev, poslao me k vama.' To mi je ime dovijeka, tako će me zvati od koljena do koljena.”
16 “Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri.
“Idi, skupi starješine Izraelaca pa im kaži: 'Jahve, Bog otaca - Bog Abrahamov, Izakov i Jakovljev - objavio mi se i rekao mi: Pohodio sam vas i razabrao što vam se čini u Egiptu.
17 Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’
Odlučio sam vas izvesti iz egipatske bijede u zemlju Kanaanaca, Hetita, Amorejaca, Perižana, Hivijaca i Jebusejaca - u zemlju kojom teče med i mlijeko!'
18 “Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’
Oni će te poslušati. Onda pođi sa starješinama Izraelaca k egipatskom kralju i reci mu: 'Objavio nam se Jahve, Bog Hebreja. Pusti nas da odemo tri dana hoda u pustinju, da ondje prinesemo žrtvu Jahvi, Bogu svojemu.'
19 Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe.
Znam ja da vas egipatski kralj neće pustiti ako ne bude natjeran teškom šakom.
20 Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.
Zato ću ja pružiti svoju šaku i pritisnuti Egipat svakovrsnim čudesima što ću ih u njemu izvesti. Poslije će vas pustiti.
21 “Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu.
Dobro ću raspoložiti Egipćane prema ovome narodu, pa kad pođete, nećete poći praznih ruku.
22 Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”
Svaka će žena zatražiti od svoje susjede i stanarke u svojoj kući nakita srebrnog i zlatnog i odjeće. To stavite na svoje sinove i kćeri. Tako ćete oplijeniti Egipćane.”