< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
И сия суть, яже сотвориши им: освятиши я, яко священнодействовати им Мне: да возмеши же телца единаго от говяд и овна два непорочна:
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
и хлебы пресны смешены с елеем, и опресноки помазаны елеем: из муки пшеничны сотвориши я:
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
и да вложиши я в кош един, и принесеши я в коши, и телца и два овна.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
И Аарона и сыны его приведеши пред двери скинии свидения, и измыеши я водою:
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
и взем ризы святыя, облечеши Аарона брата твоего, и в хитон подир, и в ризу верхнюю, и в слово: и совокупиши ему слово к нарамнику:
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
и возложиши на главу его клобук: и возложиши дщицу освящение на увясло:
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
и да возмеши от елеа помазания, и да возлиеши и на главу его и помажеши его.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
И сыны его приведеши и облечеши я в ризы:
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
и опояшеши я поясы, и возложиши на них клобуки, и будет ими священство мне во веки: и совершиши руце Аарони и руце сынов его.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
И да приведеши телца пред двери скинии свидения, и возложат Аарон и сынове его руце свои на главу телца пред Господем у дверий скинии свидения.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
И да заколеши телца пред Господем у дверий скинии свидения:
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
и да возмеши от крове телчи и помажеши на рогах олтаревых перстом твоим: останок же весь крове пролиеши у стояла олтарнаго:
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
и да возмеши весь тук, иже на утробе, и препонку печени, и обе почки, и тук иже на них, и возложиши на олтарь:
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
мяса же телча, и кожу, и мотыла да сожжеши на огни вне полка: за грех бо есть.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
И овна да поймеши единаго, и да возложат Аарон и сынове его руки своя на главу овню:
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
и заколеши его, и взем кровь пролиеши у олтаря окрест:
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
и овна да разсечеши на уды и измыеши внутренняя и ноги в воде, и возложиши на разсеченныя части со главою:
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
и вознесеши всего овна на олтарь, всесожжение Господу в воню благоухания: жертва Господу есть.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
И да поймеши овна втораго, и возложит Аарон и сынове его руки своя на главу овню:
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
и заколеши его, и возмеши от крове его, и возложиши на край ушесе Аароня деснаго и на край руки десныя и на край ноги десныя, и на край ушес сынов его десных и на край рук их десных и на край ног их десных:
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
и да возмеши от крове, яже на олтари, и от елеа помазания, и да воскропиши на Аарона и на ризу его, и на сыны его и на ризы сынов его с ним: и освятится сам и ризы его, и сыны его и ризы сынов его с ним: кровь же овню да пролиеши у олтаря окрест.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
И да возмеши от овна тук его, и тук покрывающий утробу его, и препонку печени, и обе почки, и тук иже на них, и рамо десное: есть бо совершение сие:
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
и хлеб един с елеем, и опреснок един от коша опресноков, предложенных пред Господем:
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
и возложиши вся на руки Аарони и на руки сынов его, и отделиши я отделение пред Господем:
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
и да возмеши я от рук их, и вознесеши на олтарь всесожжения в воню благоухания пред Господем: приношение есть Господу.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
И да возмеши грудь от овна совершения, яже есть Аарону, и отделиши ю отделение пред Господем, и будет тебе в часть:
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
и освятиши грудь отделение, и рамо отлучения, еже отделися, и яже отяся от овна совершения от Аарона и от сынов его,
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
и будет Аарону и сыном его законно вечно от сынов Израилевых: есть бо отделение сие, и отятие будет от сынов Израилевых от жертв спасителных сынов Израилевых, отделение Господу.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
И ризы святы, яже суть Аарону, да будут сыном его по нем, помазатися им в них и совершити руки своя.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
Седмь дний да облачится в ня иерей великий, иже вместо его от сынов его, иже внидет в скинию свидения служити во святилищи.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
И овна совершения да возмеши и испечеши мяса на месте святе,
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
и да ядят Аарон и сынове его мяса овня, и хлебы, яже в коши у дверий скинии свидения:
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
да ядят сия, имиже освятишася в них, совершити руки своя, освятити я: и иноплеменник да не снест от них, суть бо свята.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
Аще же останется от мяс жертвы совершения и от хлебов до утрия, да сожжеши останки огнем: да не снедятся, освящение бо есть.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
И сотвориши Аарону и сыном его тако по всем, елика заповедах тебе: седмь дний совершиши руце их.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
И телца греха ради да сотвориши в день очищения: и да очистиши олтарь, егда освящаеши на нем: и помажеши его, яко освятити его.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
Седмь дний очистиши олтарь и освятиши его, и будет олтарь святая святых: всяк прикасаяйся олтарю освятится.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
И сия суть, яже сотвориши на олтари: агнца единолетна непорочна два на всяк день на олтари присно жертву непрестанную:
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
агнца единаго да сотвориши рано, и втораго агнца да сотвориши в вечер:
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
и десятую часть муки пшеничны с елеем смешены, в четвертую часть ина, и возлияние четвертую часть меры ина вина единому овну.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
И агнца втораго да сотвориши в вечер, якоже утреннюю жертву, и возлияние его: сотвориши в воню благоухания приношение Господу.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
Жертву всегдашнюю в слухи и в роды вашя пред дверми скинии свидения пред Господем, в нихже познан буду тебе тамо, якоже глаголати к тебе.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
И завещаю тамо сыном Израилевым, и освящуся во славе Моей,
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
и освящу скинию свидения и олтарь, и Аарона и сыны его освящу, священнодействовати Мне,
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
и нарекуся в сынех Израилевых, и буду им Бог:
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
и уведят, яко Аз есмь Господь Бог их, изведый их из земли Египетския, нарещися им и быти им Бог.

< Kutoka 29 >