< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
«مراسم تقدیس هارون و پسرانش به مقام کاهنی به این ترتیب برگزار شود: یک گوساله و دو قوچ بی‌عیب،
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
نان بدون خمیرمایه، قرصهای نان بدون خمیرمایهٔ روغنی و قرصهای نازک نان بدون خمیرمایهٔ روغن مالی شده، که از آرد نرم گندم مرغوب پخته شده باشد، فراهم‌آور.
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
نانها را در یک سبد بگذار و آنها را با گوساله و دو قوچ، به دم در خیمۀ عبادت بیاور.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
سپس هارون و پسران او را دم مدخل خیمۀ ملاقات با آب غسل بده.
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
آنگاه لباس کاهنی هارون را که شامل پیراهن، ردا، ایفود و سینه‌پوش است، به او بپوشان و بند کمر را روی ایفود ببند.
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
دستار را با نیم تاج طلا بر سرش بگذار.
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
بعد روغن مسح را بر سرش ریخته، او را مسح کن.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
سپس لباسهای پسرانش را به ایشان بپوشان
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
و کلاهها را بر سر ایشان بگذار. بعد شال کمر را به کمر هارون و پسرانش ببند. مقام کاهنی همیشه از آن ایشان و فرزندانشان خواهد بود. بدین ترتیب هارون و پسرانش را برای کاهنی تقدیس کن.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
«گوساله را نزدیک خیمۀ ملاقات بیاور تا هارون و پسرانش دستهای خود را بر سر آن بگذارند
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
و تو گوساله را در حضور خداوند در برابر در خیمۀ ملاقات ذبح کن.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
خون گوساله را با انگشت خود بر شاخهای مذبح بمال و بقیه را در پای آن بریز.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
سپس همهٔ چربیهای درون شکم گوساله، سفیدی روی جگر، قلوه‌ها و چربی دور آنها را بگیر و بر مذبح بسوزان،
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
و بقیه لاشهٔ گوساله را با پوست و سرگین آن بیرون از اردوگاه ببر و همه را به عنوان قربانی گناهان در همان جا بسوزان.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
«آنگاه هارون و پسرانش دستهای خود را بر سر یکی از قوچها بگذارند.
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
سپس آن قوچ را ذبح کرده، خونش را بر چهار طرف مذبح بپاش.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
قوچ را قطعه قطعه کن و قسمتهای درونی و پاچه‌هایش را بشوی و آنها را با کله و سایر قطعه‌های قوچ قرار بده.
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
سپس قوچ را تماماً روی مذبح بسوزان. این قربانی سوختنی که به خداوند تقدیم می‌شود، هدیه‌ای خوشبو و مخصوص برای خداوند است.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
«بعد قوچ دوم را بگیر تا هارون و پسرانش دستهای خود را بر آن بگذارند.
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
و آن را نیز ذبح کن و مقداری از خونش را بردار و بر نرمهٔ گوش راست هارون و پسرانش و بر شست دست راست و شست پای راست آنها بمال. بقیهٔ خون را بر چهار طرف مذبح بپاش.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
آنگاه مقداری از خونی که روی مذبح است بردار و با روغن مسح بر هارون و پسران او و بر لباسهایشان بپاش. بدین وسیله خود آنان و لباسهایشان تقدیس می‌شوند.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
«آنگاه چربی، دنبه، چربی داخل شکم، سفیدی روی جگر، قلوه‌ها و چربی دور آنها و ران راست قوچ را بگیر،
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
و از داخل سبد نان بدون خمیرمایه که در حضور خداوند است یک نان و یک قرص نان روغنی و یک نان نازک بردار،
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
و همهٔ آنها را به دستهای هارون و پسرانش قرار بده تا به عنوان هدیهٔ مخصوص در حضور خداوند تکان دهند.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
سپس آنها را از دست ایشان بگیر و بر مذبح همراه با قربانی سوختنی بسوزان. این قربانی هدیه‌ای خوشبو و مخصوص برای خداوند است.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
آنگاه سینهٔ قوچی را که برای انتصاب هارون است به دست بگیر و آن را به نشانهٔ هدیهٔ مخصوص در حضور خداوند تکان بده و آنگاه آن را برای خود بردار.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
«قسمتهایی از قوچ انتصابی را که مال هارون و پسرانش است، کنار بگذار، یعنی سینه و رانی را که به نشانهٔ هدیهٔ مخصوص در حضور خداوند تکان داده شد.
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
در آینده، هرگاه بنی‌اسرائیل قربانیهای سلامتی تقدیم کنند، قسمتی از آن باید برای هارون و پسرانش کنار گذاشته شود. این است حق دائمی ایشان که هدیه‌ای مقدّس از جانب بنی‌اسرائیل به خداوند می‌باشد.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
«لباسهای مقدّس هارون باید برای پسرانش و نسلهای بعد که جانشین او هستند نگاهداری شوند تا هنگام برگزاری مراسم مسح و تقدیس آنها را بپوشند.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
فرزند پسری که به جای او به مقام کاهنی می‌رسد تا در خیمۀ ملاقات و قدس مشغول خدمت شود، باید هفت روز آن لباس را بر تن کند.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
«گوشت قوچ مخصوص مراسم تقدیس را بگیر و آن را در یک جای مقدّس در آب بپز.
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
هارون و پسرانش باید گوشت قوچ را با نانی که در سبد است در مدخل خیمهٔ ملاقات بخورند.
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
آنها باید تنها خودشان آن قسمتهایی را که در موقع اجرای مراسم، برای تقدیس و کفارهٔ ایشان منظور شده است، بخورند؛ افراد معمولی نباید از آن بخورند چون مقدّس است.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
اگر چیزی از این گوشت و نان تا صبح باقی بماند آن را بسوزان، نباید آن را خورد زیرا مقدّس می‌باشد.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
«به این طریق مراسم تقدیس هارون و پسرانش برای مقام کاهنی اجرا شود. مدت این مراسم باید هفت روز باشد.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
در این هفت روز، روزی یک گوساله برای کفارهٔ گناهان، روی مذبح قربانی کن. با این قربانی، مذبح را طاهر ساز و با روغن زیتون آن را تدهین کن تا مقدّس شود.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
برای مدت هفت روز، هر روز برای مذبح کفاره کن تا مذبح تقدیس شود. به این ترتیب، مذبح، جایگاه بسیار مقدّسی می‌شود و هر کسی نمی‌تواند به آن دست زند.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
«هر روز دو برهٔ یک ساله روی مذبح قربانی کن.
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
یک بره را صبح و دیگری را عصر قربانی کن.
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
با برهٔ اول یک کیلو آرد مرغوب که با یک لیتر روغن زیتون مخلوط شده باشد تقدیم کن. یک لیتر شراب نیز به عنوان هدیهٔ نوشیدنی تقدیم نما.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
برهٔ دیگر را هنگام عصر قربانی کن و با همان مقدار هدیۀ آردی و نوشیدنی تقدیم کن. این قربانی، هدیه‌ای خوشبو و مخصوص برای خداوند خواهد بود.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
«این قربانی سوختنی، همیشگی خواهد بود و نسلهای آیندهٔ شما نیز باید در کنار در خیمۀ ملاقات، آن را به حضور خداوند تقدیم کنند. در آنجا من شما را ملاقات نموده، با شما سخن خواهم گفت.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
در آنجا بنی‌اسرائیل را ملاقات می‌کنم و خیمۀ عبادت از حضور پرجلال من تقدیس می‌شود.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
بله، خیمۀ ملاقات، مذبح، و هارون و پسرانش را که کاهنان من هستند تقدیس می‌کنم.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
من در میان بنی‌اسرائیل ساکن شده، خدای ایشان خواهم بود
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
و آنها خواهند دانست که من خداوند، خدای ایشان هستم که آنها را از مصر بیرون آوردم تا در میان ایشان ساکن شوم. من خداوند، خدای آنها هستم.

< Kutoka 29 >