< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
But also thou schalt do this, that thei be sacrid to me in preesthod; take thou a calf of the droue, and twei rammes with out wem,
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
and therf looues, and a cake with out sour dow, whiche be spreynt to gidere with oile, and therf paast sodun in watir, `bawmed, ether fried, with oile; thou schalt make alle thingis of whete flour,
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
and thou schalt offre tho put in a panyere. Forsothe thou schal presente the calfe,
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
and twey rammes, and Aaron and his sones, at the dore of tabernacle of witnessyng; and whanne thou hast waische the fadir and the sones in watir,
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
thou schalt clothe Aaron with hise clothis, that is, the lynnen cloth, `and coote, and the cloth on the schuldris, `and the racional, which thou schalt bynde with a girdil.
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
And thou schalt sette the mytre on his heed, and the hooli plate on the mytre,
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
and thou schalt schede the oile of anoyntyng on his heed; and bi this custom he schal be sacrid.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
Also thou schalt presente hise sones, and thou schalt clothe with lynnun cootis,
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
and thou schalt girde Aaron and hise sones with a girdil; and thou schalt sette mytris on hem; and thei schulen be my preestis bi euerlastynge religioun. After that thou hast halewid `the hondis of hem,
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
also thou schalt presente the calf bifore the tabernacle of witnessyng; and Aaron and hise sones schulen sette hondis `on the heed therof;
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
and thou schalt sle it in the siyt of the Lord, bisidis the dore of the tabernacle of witnessyng.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
And thou schalt take the blood of the calf, and schalt putte with thi fyngur on the corneris of the auter. Forsothe thou schalt schede the `tothir blood bisidis the foundement therof.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
And thou schalt take al the fatnesse that hilith the entrailis, and the calle of the mawe, and twey kidneris, and the fatnesse which is on hem; and thou schalt offere encense on the auter.
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
Forsothe thou schalt brenne with out the castels the `fleischis of the calf, and the skyn, and the dung, for it is for synne.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Also thou schalt take a ram, on whos heed Aaron and hise sones schulen sette hondis;
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
and whanne thou hast slayn that ram, thou schalt take of `his blood, and schalt schede aboute the auter.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
Forsothe thou schalt kitte thilk ram in to smale gobetis, and thou schalt putte hise entrailis waischun, and feet on the fleischis koruun, and on his heed;
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
and thou schalt offre al the ram in to encence on the auter; it is an offryng to the Lord, the swettest odour of the slayn sacrifice of the Lord.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
And thou schalt take the tothir ram, on whos heed Aaron and hise sones schulen sette hondis;
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
and whanne thou hast offrid that ram, thou schalt take of his blood, and schalt `putte on the last part of the riyt eere of Aaron, and of hise sones, and on the thombis of her hond; and of her riyt foot; and thou schalt schede the blood on the auter, `bi cumpas.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
And whanne thou hast take of the blood, which is on the auter, and of oile of anoynting, thou schalt sprenge Aaron and hise clothis, the sones and her clothis. And whanne thei and the clothis ben sacrid,
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
thou schalt take the ynnere fatnesse of the ram, and the tayl, and the fatnesse that hilith the entrailis, and the calle of the mawe, and twey kideneris, and the fatnesse that is on tho; and thou schalt take the riyt schuldur, for it is the ram of consecracioun;
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
and thou schalt take a tendur cake of o loof, spreynd with oile, paast sodun in watir, and after fried in oile, of the panyer of therf looues, which is set in `the siyt of the Lord.
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And thou schalt putte alle `thingis on the hondis of Aaron and of hise sones, and schalt halewe hem, and reise bifor the Lord.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And thou schalt take alle thingis fro `the hondis of hem, and schalt brenne on the autir, in to brent sacrifice, `swettist odour in the siyt of the Lord, for it is the offryng of the Lord.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
Also thou schalt take the brest of the ram, bi which Aaron was halewid, and thou schalt halewe it reisid bifor the Lord; and it schal turne in to thi part.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
And thou schalt halewe also the brest sacrid, and the schuldur which thou departidist fro the ram,
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
bi which Aaron was halewid, and hise sones; and tho schulen turne in to the part of Aaron, and of hise sones, bi euerlastinge riyt, of the sones of Israel; for tho ben the firste thingis, and the bigynnyngis of the pesible sacrifices of hem, whiche thei offren to the Lord.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
Forsothe the sones of Aaron schulen haue aftir hym the hooli cloth, which Aaron schal vse, that thei be anoyntid ther ynne, and her hondis be sacrid.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
`Thilke, that of hise sones schal be maad bischop for hym, schal vse that cloth seuene daies, and which sone schal entre in to the tabernacle of witnessyng, that he mynystre in the seyntuarie.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
Sotheli thou schalt take the ram of consecracioun, and thou schalt sethe hise fleischis in the hooli place,
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
whiche fleischis Aaron and his sones schulen ete, and thei schulen ete the looues, that ben in the panyere, in the porche of the tabernacle of witnessyng,
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
that it be a pleasaunt sacrifice, and that the hondis of the offreris be halewid. An alien schal not ete of tho, for tho ben hooli.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
That if ony thing leeueth of the fleischis halewid, ether of the looues, til the morewtid, thou schalt brenne the relifs by fier, thou schulen not be etun, for tho ben halewid.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
Thou schalt do on Aaron, and hise sones, alle thingis whiche I comaunde to thee. Seuene daies thou schalt sacre `the hondis of hem,
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
and thou schalt offre a calf for synne bi ech day to clense; and thou schalt clense the auter, whanne thou hast offrid the sacrifice of clensyng, and thou schalt anoynte the auter in to halewyng.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
Seuene daies thou shalt clense and halewe the auter, and it schal be the hooli of hooli thingis; ech man that schal touche it schal be halewid.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
This it is, that thou schalt do in the auter, twei lambren of o yeer contynueli bi ech dai,
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
o lomb in the morewtid, and the tothir in the euentid;
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
`thou schalt do in o lomb the tenthe part of flour spreynt with oyle, powned, that schal haue a mesure, the fourthe part of hyn, and wyn of the same mesure, to make sacrifice.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Sotheli thou schalt offre the tother lomb at euentid, bi the custom of the offryng at the morewtid, and bi tho thingis, whiche we seiden, in to the odour of swetnesse;
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
it is a sacrifice to the Lord bi euerlastynge offryng in to youre generaciouns, at the dore of the tabernacle of witnessyng bifor the Lord, where Y schal ordeyne that Y speke to thee;
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
and there Y schal comaunde to the sones of Israel; and the auter schal be halewid in my glorie.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
Y schal halewe also the tabernacle of witnessyng with the auter, and Aaron with hise sones, that thei be set in presthod to me.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
And Y schal dwelle in the myddis of the sones of Israel, and Y schal be God to hem;
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
and thei schulen wite, that Y am her Lord God, which ledde hem out of the lond of Egipt, that Y schulde dwelle among hem; for Y am her Lord God.

< Kutoka 29 >