< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
And this [is] the thing that thou shalt do to them to hallow them, to minister to me in the priest's office: Take one young bullock, and two rams without blemish,
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
And unleavened bread, and cakes unleavened tempered with oil, and wafers unleavened anointed with oil; [of] wheat flour shalt thou make them.
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
And thou shalt put them into one basket, and bring them in the basket, with the bullock and the two rams.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And Aaron and his sons thou shalt bring to the door of the tabernacle of the congregation, and shalt wash them with water.
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
And thou shalt take the garments, and put upon Aaron, the coat, and the robe of the ephod, and the ephod, and the breast-plate, and gird him with the curious girdle of the ephod:
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
And thou shalt put the miter upon his head, and put the holy crown upon the miter.
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
Then shalt thou take the anointing oil, and pour [it] upon his head, and anoint him.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
And thou shalt bring his sons, and put coats upon them.
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
And thou shalt gird them with girdles (Aaron and his sons) and put the bonnets on them; and the priest's office shall be theirs for a perpetual statute: and thou shalt consecrate Aaron and his sons.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
And thou shalt cause a bullock to be brought before the tabernacle of the congregation; and Aaron and his sons shall put their hands upon the head of the bullock.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
And thou shalt kill the bullock before the LORD, [by] the door of the tabernacle of the congregation.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
And thou shalt take of the blood of the bullock, and put [it] upon the horns of the altar with thy finger, and pour all the blood beside the bottom of the altar.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
And thou shalt take all the fat that covereth the inwards, and the caul [that is] above the liver, and the two kidneys, and the fat that [is] upon them, and burn [them] upon the altar.
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
But the flesh of the bullock, and his skin, and his dung shalt thou burn with fire without the camp: it [is] a sin-offering.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Thou shalt also take one ram; and Aaron and his sons shall put their hands upon the head of the ram.
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
And thou shalt slay the ram, and thou shalt take his blood, and sprinkle [it] around upon the altar.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
And thou shalt cut the ram in pieces, and wash the inwards of him, and his legs, and put [them] to his pieces, and to his head.
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And thou shalt burn the whole ram upon the altar: it [is] a burnt-offering to the LORD: it [is] a sweet savor, an offering made by fire to the LORD.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
And thou shalt take the other ram; and Aaron and his sons shall put their hands upon the head of the ram.
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
Then shalt thou kill the ram, and take of his blood, and put [it] upon the tip of the right ear of Aaron, and upon the tip of the right ear of his sons, and upon the thumb of their right hand, and upon the great toe of their right foot, and sprinkle the blood upon the altar round about.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
And thou shalt take of the blood that [is] upon the altar, and of the anointing oil, and sprinkle [it] upon Aaron, and upon his garments, and upon his sons, and upon the garments of his sons with him: and he shall be hallowed, and his garments, and his sons, and his sons garments with him.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
Also thou shalt take of the ram the fat and the rump, and the fat that covereth the inwards, and the caul [above] the liver, and the two kidneys, and the fat that [is] upon them, and the right shoulder; for it [is] a ram of consecration:
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
And one loaf of bread, and one cake of oiled bread, and one wafer out of the basket of the unleavened bread, that [is] before the LORD.
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And thou shalt put all in the hands of Aaron, and in the hands of his sons; and shalt wave them [for] a wave-offering before the LORD.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And thou shalt receive them from their hands, and burn [them] upon the altar for a burnt-offering, for a sweet savor before the LORD: it [is] an offering made by fire to the LORD.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
And thou shalt take the breast of the ram of Aaron's consecration, and wave it [for] a wave-offering before the LORD: and it shall be thy part.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
And thou shalt sanctify the breast of the wave-offering, and the shoulder of the heave-offering, which is waved, and which is heaved up of the ram of the consecration, [even] of [that] which [is] for Aaron, and of [that] which is for his sons:
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
And it shall be Aaron's and his sons' by a statute for ever, from the children of Israel: for it [is] a heave-offering: and it shall be a heave-offering from the children of Israel of the sacrifice of their peace-offerings, [even] their heave-offering to the LORD.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
And the holy garments of Aaron shall be his sons' after him, to be anointed therein, and to be consecrated in them.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
[And] that son, that is priest in his stead, shall put them on seven days, when he cometh into the tabernacle of the congregation to minister in the holy [place].
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
And thou shalt take the ram of the consecration, and seethe his flesh in the holy place.
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
And Aaron and his sons shall eat the flesh of the ram, and the bread that [is] in the basket, [by] the door of the tabernacle of the congregation.
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
And they shall eat those things with which the atonement was made, to consecrate [and] to sanctify them: but a stranger shall not eat [of them], because they [are] holy.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
And if aught of the flesh of the consecration, or of the bread, shall remain till the morning, then thou shalt burn the remainder with fire: it shall not be eaten, because it [is] holy.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
And thus shalt thou do to Aaron, and to his sons, according to all [things] which I have commanded thee: seven days shalt thou consecrate them.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
And thou shalt offer every day a bullock [for] a sin-offering for atonement; and thou shalt cleanse the altar, when thou hast made an atonement for it, and thou shalt anoint it, to sanctify it.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
Seven days thou shalt make an atonement for the altar, and sanctify it; and it shall be an altar most holy: whatever toucheth the altar shall be holy.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
Now this [is that] which thou shalt offer upon the altar; two lambs of the first year, day by day continually.
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
The one lamb thou shalt offer in the morning; and the other lamb thou shalt offer at evening.
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
And with the one lamb a tenth-portion of flour mingled with the fourth part of a hin of beaten oil; and the fourth part of a hin of wine [for] a drink-offering.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And the other lamb thou shalt offer at evening, and shalt do thereto according to the meat-offering of the morning, and according to the drink-offering thereof, for a sweet savor, an offering made by fire to the LORD.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
[This shall be] a continual burnt-offering throughout your generations [at] the door of the tabernacle of the congregation before the LORD: where I will meet you to speak there to thee.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
And there I will meet with the children of Israel, and [the tabernacle] shall be sanctified by my glory.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
And I will sanctify the tabernacle of the congregation, and the altar: I will sanctify also both Aaron and his sons, to minister to me in the priest's office.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
And I will dwell among the children of Israel, and will be their God.
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
And they shall know that I [am] the LORD their God, that brought them forth out of the land of Egypt, that I may dwell among them: I [am] the LORD their God.

< Kutoka 29 >